Friday, August 4, 2023

MHE. WAZIRI SIMBACHAWENE AWATAKA MAKATIBU TAWALA WA WILAYA KUSIMAMIA SUALA LA NIDHAMU KWA WATUMISHI WAO

 Na. Veronica Mwafisi-Kwimba

Tarehe 04 Agosti, 2023

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amewataka Makatibu Tawala wa Wilaya kutekeleza majukumu yao kikamilifu ikiwepo kusimamia suala la nidhamu ili kutenda haki na kuondoa changamoto za kiutumishi.

Mhe. Simbachawene amesema hayo alipokuwa akizungumza na watumishi wa umma wa Wilaya ya Kwimba, Mkoa wa Mwanza wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuhimiza uwajibikaji na kutatua kero na changamoto zinazowakabili watumishi wa umma katika Wilaya hiyo.

“Makatibu Tawala, msidhani ya kuwa mamlaka ya nidhamu hayapo kwenu, mmechaguliwa kuwa viongozi kwa lengo la kuondoa changamoto kati ya waajiri na waajiriwa, hivyo mna jukumu kubwa la kusimamia suala hilo” amesisitiza Mhe. Simbachawene.

Aidha, Mhe. Simbachawene amesema ni vema viongozi wa Wilaya wakafahamu changamoto mbalimbali za watumishi na wananchi na kuzishughulikia ili kuondoa tabia ya baadhi ya watumishi kutaka kuchukua majukumu ambayo hawahusiki nayo.

Akitoa neno la shukrani, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Mhe. Ng’wilabuzu Ludigija amemshukuru Waziri Simbachawene kwa kufanya ziara ya kikazi katika Wilaya yake na kuzungumza na watumishi kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji ambapo ameahidi kwa kushirikiana na watumishi wa wilaya hiyo watatekeleza maelekezo yote ambayo amewaagiza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene yupo katika ziara ya kikazi mkoani Mwanza yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma pamoja na kukagua utekelezaji wa Miradi ya TASAF.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na watumishi wa Wilaya ya Kwimba, mkoani Mwanza wakati wa ziara yake ya kikazi   iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma.


Sehemu ya watumishi wa Wilaya ya Kwimba, mkoa wa Mwanza wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa Wilaya hiyo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Amos Makalla mara baada ya kuwasili katika ofisi za Mkuu wa Mkoa huyo wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Simbachawene iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, mara baada ya kuwasili katika ofisi hizo wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa Wilaya hiyo.


Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (aliyeshika kipaza sauti) alipokuwa akizungumza na watumishi hao wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa Wilaya hiyo.


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba, mkoani Mwanza, Bi. Hapiness Msanga akiwasilisha taarifa ya hali ya Watumishi katika Wilaya yake kabla ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na watumishi wa Wilaya ya Kwimba, mkoani Mwanza wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma.


Mtumishi wa Wilaya ya Kwimba, Bi. Lyidia Bitaliho akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo mkoani Mwanza iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi hao.




 

No comments:

Post a Comment