Sunday, January 29, 2023

WATUMISHI OFISI YA RAIS-UTUMISHI KUPATIWA MAFUNZO YA AKILI YA KUHIMILI HISIA BINAFSI NA ZA WATEJA ILI WAWEZE KUTOA HUDUMA BORA

 

Na. James K. Mwanamyoto-Dodoma

Tarehe 29 Januari, 2023

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro amesema katika kuunga mkono kwa vitendo azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi, ofisi yake inaandaa mafunzo ya akili ya kuhimili hisia binafsi na za wateja kwa watumishi wa ofisi yake ili kuwawezesha kutoa huduma bora.

Dkt. Ndumbaro amesema hayo jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa ofisi yake kilicholenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili wakati wa kutoa huduma kwa wadau na wananchi.

Dkt. Ndumbaro amewahimiza watumishi wa ofisi yake kuyatumia vizuri mafunzo ya kutoa huduma kwa kumjali mteja (customer care) waliyopatiwa ili kubadilika kiutendaji na kuwa na tija katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na maendeleo ya taifa kwa ujumla.                 

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi ameungana na Dkt. Laurean Ndumbaro kwa kuwakumbusha watumishi wa ofisi yake kuwa, wanalo jukumu kubwa la kuwahudumia vizuri wananchi na wadau wa Utumishi wa Umma hivyo hawana budi kuitekeleza kwa vitendo dhana ya utoaji wa huduma kwa kumjali mteja.

Bw. Daudi amesisitiza kuwa, watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wanapaswa kuwa vinara wa kutoa huduma nzuri na bora kwa wateja, kwani ndiyo ofisi iliyokasimiwa jukumu la kusimamia utumishi wa umma nchini hivyo ndio kimbilio la utatuzi wa changamoto za watumishi wote wa umma pamoja na wananchi wanaofuata huduma katika taasisi za umma.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Musa Magufuli amesema, mafunzo ya huduma ya kumjali mteja waliyopatiwa wameyapokea vizuri na watayatumia kikamilifu katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wadau na wananchi.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imepewa jukumu la usimamizi wa Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa mujibu wa Hati ya Mgawanyo wa madaraka iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tangazo la Serikali Na. 534 la tarehe 02 Julai, 2021. 

 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro (katikati) akizungumza na watumishi wa ofisi yake jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na watumishi hao kilicholenga kutatua changamoto zinazowakabili na kuhimiza uwajibikaji ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wadau na wananchi. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu UTUMISHI Bw. Xavier Daudi (kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Musa Magufuli (kulia).


 

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao kazi cha Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro kilicholenga kutatua changamoto zinazowakabili na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi akizungumza na watumishi wa ofisi yake wakati wa kikao kazi cha Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro na watumishi wa ofisi yake kilicholenga kutatua changamoto zinazowakabili na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao. Katikati ni Katibu Mkuu UTUMISHI Dkt. Laurean Ndumbaro na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Musa Magufuli (kulia).

 

 

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Musa Magufuli akieleza namna watumishi walivyoyapokea mafunzo ya customer care na kuahidi kuyatumia kikamilifu katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wadau na wananchi.


 

Mmoja wa watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Mariam Salim akiwasilisha hoja kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro wakati wa kikao kazi cha Katibu Mkuu huyo na watumishi hao kilicholenga kutatua changamoto zinazowakabili na kuhimiza uwajibikaji.


 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro (katikati) akisikiliza hoja zinazowasilishwa na watumishi wa ofisi yake wakati wa kikao kazi chake na watumishi hao kilicholenga kutatua changamoto zinazowakabili na kuhimiza uwajibikaji. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu UTUMISHI Bw. Xavier Daudi (kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Musa Magufuli (kulia).


 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro (katikati) akitoa ufafanuzi wa hoja zilizowasilishwa na watumishi wa ofisi yake wakati wa kikao kazi chake na watumishi hao kilicholenga kutatua changamoto zinazowakabili na kuhimiza uwajibikaji. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu UTUMISHI Bw. Xavier Daudi (kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Musa Magufuli (kulia).


 


No comments:

Post a Comment