Wednesday, October 17, 2018

SERIKALI YAWATAKA WAKUU WA IDARA ZA UTAWALA NA RASILIMALIWATU SERIKALINI KUSIMAMIA VIZURI RASILIMALIWATU ILI KUWEZESHA UTOAJI HUDUMA BORA KWA WANANCHI




Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro akiendesha kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Rasilimaliwatu kinachofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP) jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro akifungua rasmi  kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Rasilimaliwatu kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) kinachofanyika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP) jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakuu wa Idara za Utawala na Rasilimaliwatu serikalini wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi cha watendaji hao  kinachofanyika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP) jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi.Dorothy Mwaluko akizungumza na Wakuu wa Idara za Utawala na Rasilimaliwatu waliohudhuria kikao kazi kinachofanyika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP) jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakuu wa Idara za Utawala na Rasilimaliwatu wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi.Dorothy Mwaluko (hayupo pichani) wakati akiwasilisha mada kuhusu Wajibu na Majukumu ya Wakuu wa Idara za Utawala na  Rasilimaliwatu katika kikao kazi cha watendaji hao kinachofanyika katika  ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP) jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt. Zainab  Chaula akizungumza na Wakuu wa Idara za Utawala na Rasilimaliwatu kuhusu masuala ya kiutumishi katika kikao kazi kinachofanyika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP) jijini Dodoma.


No comments:

Post a Comment