Wednesday, October 29, 2025
WATENDAJI WAKUU OFISI YA RAIS-UTUMISHI WAPIGA KURA, KATIBU MKUU MKOMI ATOA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA NA WANANCHI KUJITOKEZA KUTIMIZA HAKI YAO YA KIKATIBA
Na. Antonia Mbwambo na Veronica Mwafisi -Dodoma
Tarehe 29 Oktoba, 2025
Watendaji Wakuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora leo tarehe 29.10.2025 wameshiriki zoezi la kupiga kura katika
Vituo mbalimbali na kuchagua Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani.
Akishiriki zoezi hilo katika Kituo cha Kupiga Kura cha Msangalale
Mashariki, Kata ya Dodoma Makulu, jijini Dodoma, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi ametoa wito kwa Watumishi wa
Umma na Wananchi kujitokeza kuchagua viongozi wanaowahitaji kwa maendeleo ya Taifa.
“Namshukuru Mungu nimeshikiri salama zoezi hili muhimu la Kikatiba, nipende
kutoa wito kwa Watumishi wa Umma na Wananchi kwa ujumla kushikiriki pia kwani
ni haki yao ya msingi.” Bw. Mkomi amesisitiza.
Amesema hali katika Kituo hicho ni ya utulivu na wananchi wamekua
wakimiminika kwenda kupiga kura hivyo amewasisitiza kila mwenye haki ya
kushiriki zoezi hilo afanye hivyo.
Aidha, Bw. Mkomi amewapongeza Waratibu wa zoezi hilo katika Kituo hicho
kwa kuonyesha ushirikiano kwa wananchi wanaoenda kushiriki katika zoezi hilo na
kuhakikisha kila mwenye sifa anashiriki kikamilifu.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi
ameshiriki zoezi hili muhimu katika Kituo cha Mwatano, Kata ya Miyuji, Jijini
Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiweka
fomu ya kupiga Kura katika sanduku la Kura mara baada ya kushiriki zoezi hilo
la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi
katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Dodoma
Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akiweka fomu ya kupiga Kura katika sanduku la Kura
mara baada ya kushiriki zoezi hilo la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya
Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa
wa Mwatano jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akipokea fomu ya kushiriki
kupiga Kura kutoka kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na
Madiwani leo tarehe 29 Oktoba,
2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (aliyesimama) akisubiri kupatiwa fomu ya kushiriki kupiga Kura kutoka kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akionesha jina lake katika orodha ya wapiga Kura iliyobandikwa katika
kituo hicho kabla ya kushiriki kupiga kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale
jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akishiriki kupiga Kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi
ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa
wa Mwatano jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akionesha kadi yake ya kupiga Kura kabla
ya kushiriki zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika
Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akihakiki jina na picha yake kwenye daftari la kudumu
kabla ya kushiriki zoezi la kupiga Kura katika Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya
Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa
wa Mwatano jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akipakwa wino mara baada ya
kushiriki kupiga Kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi kwenye ngazi ya Rais, Wabunge na
Madiwani leo tarehe 29 Oktoba,
2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (wa kwanza kushoto) akipokea fomu ya
kushiriki kupiga Kura kutoka kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika zoezi la
Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi
ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini
Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akionesha
kidole kilichopakwa wino mara baada ya kushiriki kupiga Kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi kwenye ngazi ya Rais, Wabunge na
Madiwani leo tarehe 29 Oktoba,
2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.
Monday, October 27, 2025
OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAWAPONGEZA WASTAAFU WA OFISI HIYO KWA KULITUMIKIA TAIFA KIKAMILIFU
Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 28 Oktoba, 2025
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora imewapongeza Watumishi wa Ofisi hiyo waliofikia ukomo katika
Utumishi wa Umma kutokana na utumishi uliotukuka kwa kutekeleza majukumu yao
kwa ufanisi ambao umechangia kutolewa kwa huduma bora katika Idara walizokuwa
wakifanyia kazi.
Akitoa pongezi hizo kwa niaba ya Katibu Mkuu, Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, leo tarehe 27 Oktoba, 2025, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi amesema kufikisha umri wa
miaka 60 sio mchezo, ni jambo la kumshukuru Mungu.
“Hongereni sana, mmeondoka katika Utumishi wa
Umma mkiwa na sifa nzuri katika kulitumikia taifa na mkiwa na afya njema ni
mfano mzuri wa kuigwa na tunaoendelea kufanya kazi,” amesema SACP. Mahumi.
SACP. Mahumi amemshukuru Katibu Mkuu-UTUMISHI
kupitia Idara ya Utawala kwa kuanzisha utamaduni wa kukutana kila Jumatatu na
kuwa na ubunifu mbalimbali wa kuwaweka watumishi pamoja kwa lengo la kuboresha
utendaji.
“Tangu jambo hili la kukutana pamoja kila siku ya
Jumatatu kupata elimu ya kuboresha utendaji kumekuwa na mabadiliko makubwa ya
kiutendaji, nawasihi tuendelee kuyatumia mafunzo haya kuboresha utendaji
zaidi.” Amesisitiza.
Akitoa neno la shukrani, Mtumishi Mstaafu wa Ofisi
hiyo, Bw. Jerome Nchimbi amesema, ndani ya miaka 8 aliyofanya kazi katika ofisi
hiyo amejfunza masuala mengi ya Kiutumishi pamoja na kufundishwa upendo, ushirikiano
na kuwajali watu.
Kwa upande wake, Mstaafu mwingine, Bi. Godliver
Byemerwa ametoa wito kwa Watumishi wa ofisi hiyo kuendelea kuwahudumia Wananchi
kwa moyo wa upendo na ufanisi mkubwa kwa kuwa ofisi hiyo ni kioo cha jamii.
Aidha, Ofisi hiyo
imewapongeza Watumishi waliozaliwa mwezi Oktoba na kuwatakia heri katika maisha
yao ya Utumishi wa Umma ili kuwatumikia wananchi pamoja na kuongeza tija katika
utendajikazi.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa
Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi (wakwanza
kulia) akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa
Watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya
Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
wakimsikiliza Mkurugenzi
wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya
Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakiwasikiliza Watumishi wastaafu
Bw. Jerome Nchimbi na Bi. Godliver
Byemerwa (hawapo pichani) wa ofisi hiyo walipokuwa wakitoa
shukrani kwa Viongozi na Watumishi mara baada ya kufikia ukomo katika Utumishi
wa Umma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifurahia jambo wakati Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa Watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa
wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha kwa niaba ya
Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa Watumishi hao katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali
Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo
waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo
iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na
Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mtumishi Mstaafu wa Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, Bw. Jerome Nchimbi akitoa neno la shukrani kwa Wakurugenzi na
Watumishi wa ofisi hiyo baada ya kuhitimisha Utumishi wake wa Umma.
Sehemu ya Wakurugenzi na
Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Mkurugenzi wa
Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya
Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha
Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini
Dodoma.
Mtumishi Mstaafu wa Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, Bi. Godliver Byemerwa akitoa neno la shukrani kwa Wakurugenzi
na Watumishi wa ofisi hiyo baada ya kuhitimisha Utumishi wake wa Umma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa
Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Monday, October 20, 2025
WATUMISHI WA OFISI YA RAIS – UTUMISHI WAPATIWA MAFUNZO JUU YA MABADILIKO YA MTAZAMO KWENYE ENEO LA KAZI.
Na Eric Amani, Mtumba Dodoma,
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi amesema Serikali inaendelea kuweka mkazo katika kujenga utamaduni wa kazi unaozingatia maadili, ubunifu, na mabadiliko ya fikra miongoni mwa watumishi wa umma.
“Mabadiliko ya kweli katika utumishi wa umma yanaanza kwenye fikra na mitazamo ya mtumishi mmoja mmoja. Tunapaswa kubadilika ili tuwe chachu ya mageuzi katika utoaji wa huduma kwa wananchi,” alisema Bw. Daudi.
Leo Oktoba 20, 2025 Watumishi wa Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wamepatiwa mafunzo maalum yanayolenga kubadilisha mitazamo na mienendo yao katika mazingira ya kazi ili kuongeza ufanisi na ubora wa huduma kwa umma.
Mafunzo hayo ambayo hutolewa kila jumatatu yalihusisha mada mbalimbali zikiwemo mbinu za kujitambua, umuhimu wa kuwa na mtazamo chanya, ushirikiano kazini, na namna ya kujenga nidhamu na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu ya kila siku ikiwa kwa lengo la kuwajengea uwezo watumishi hao ili kuboresha Utendaji kazi.
Aidha Bw. Daudi amewasisitiza watumishi wa umma kushiriki kikamilifu kwa wale wote ambao waliojiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura kwa ajili ya zoezi la Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025 kwaajili ya kuchagua viongozi sahihi kuanzia ngazi ya Rais, Ubunge na Udiwani.
Kwa upande mwezeshaji, Mosses Raymond, wakati akiwasilisha mada mbalimbali amesema mafunzo hayo yanalenga kuwasaidia watumishi wa umma kuelewa umuhimu wa kujiwekea malengo binafsi na kushirikiana kwa karibu zaidi na wenzao ili kuboresha utendaji wa taasisi.
![]() |
| Mwezeshaji Ndg. Mosses Raymond akitoa mafunzo kuhusu mabadiliko ya mtazamo kwenye eneo la kazi kwa watumishi wa Ofisi wa Rais - UTUMISHI leo oktoba 20, 2025 Mtumba Jijini Dodoma. |
![]() |
| Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais -UTUMISHI wakimsikiliza kwa makini mwezeshaji Ndg Mosses Raymond (aliyesimama) wakati akifundisha juu ya mabadiliko ya mtazamo kwenye eneo la kazi Mtumba, Dodoma leo Oktoba 20, 2025 |
![]() |
| Msaidizi wa Masjala Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bi. Mariam Sadik akiongoza sala kabla ya kufungua mafunzo maalum kwa ajili ya watumishi wa Ofisi hiyo yanayolenga kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo Oktoba 20, 2025. |
Tuesday, October 14, 2025
Monday, October 13, 2025
WITO WATOLEWA KWA WATUMISHI WA UMMA KUBADILIKA KIMTAZAMO KATIKA UTENDAJI ILI KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050
Na Antonia Mbwambo- Dodoma.
Tarehe 13/10/2025
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye
ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi ametoa wito kwa Watumishi
wa Umma nchini kubadilika kimtazamo katika utendaji ili kufikia malengo ya Dira
ya Taifa ya Maendeleo 2050 ikiwemo matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano (TEHAMA).
Kaimu Katibu Mkuu Bw. Daudi amesema, Watumishi
wa Umma kubadilika kimtazamo katika utendaji ni jambo muhimu kwani kunakuwa na
ufanisi wa wa kazi unaowezesha kuwa na Taifa jumuishi lenye ustawi, haki na
linalojitegemea.
“Ninatoa wito kwenu, msitekeleze majukumu yenu
kwa mazoea, kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, mbadilike kiutendaji ili
kuendana na mabadiliko yakiwemo ya kidijiti kwa kuleta ubunifu na mawazo chanya
yatakayoiwezesha serikali kufikia malengo yake ya kutoa huduma bora kwa
wananchi kupitia matumizi sahihi ya mifumo ya TEHAMA,” Bw. Daudi alisema.
Kwa upande wake Meneja Mawasiliano Serikalini
kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo wakati akiwasilisha mada
kwa watumishi hao kuhusu Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, amesema mabadiliko
makubwa ya Sayansi na Teknolojia ni kichocheo kikubwa cha maendeleo katika
Taifa letu ambapo Dira hii imelenga kuwa kufikia mwaka 2050, asilimia 70 ya Watanzania
watakuwa wanatumia mifumo ya TEHAMA na asilimia 80 ya huduma mbalimbali za kiserikali zitakuwa zikitolewa
kidiji ili kuleta Ufanisi katika Utendaji.
Wakurugenzi wa Idara na vitengo mbalimbali kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na mwezeshaji ambaye ni
Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus
Kaguo (hayupo pichani) leo tarehe13/10/2025 katika mafunzo ambayo hutolewa kila
siku ya jumatatu kwenye Ofisi hiyo iliyopo Mtumba
jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (aliyesimama mbele) akizungumza na watumishi wa Ofisi hiyo baada ya wasilisho la mada ya Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 lililotolewa leo tarehe13/10/2025 na Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo katika mafunzo ya kuwajengea watumishi wa Ofisi hiyo uwezo wa kiutendaji, ambayo hutolewa kila siku ya jumatatu kwenye Ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.
Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka
Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo (aliyesimama mbele) akiwasilisha mada
ya Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika
mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI,yaliyofanyika leo tarehe 13/10/2025 katika Ofisi hiyo iliyopo
Mtumba jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (wa
kwanza kushoto aliyevaa miwani) akifurahia jambo alipokuwa akifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo
wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo ambayo hufanyika kila siku ya jumatatu
katika Ofisi hiyo Mtumba Dodoma.
Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada
iliyokuwa ikiwasilishwa na mwezeshaji ambaye ni Meneja Mawasiliano Serikalini
kutoka Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo (hayupo pichani) kwenye
mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo ambayo
hufanyika kila siku ya jumatatu katika Ofisi hiyo Mtumba Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi
akiteta jambo na Mkurugenzi wa Mipango wa Ofisi hiyo Bw. Cosmas Ngangaji wakati
wa mafunzo ya kuwajengea watumishi wa Ofisi hiyo uwezo wa kiutendaji
yaliyofanyika katika eneo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Idara na vitengo pamoja na
watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia mada iliyokuwa
ikiwasilishwa na mwezeshaji ambaye ni Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume
ya Taifa ya Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo (hayupo pichani) leo
tarehe13/10/2025 katika mafunzo ambayo hutolewa kila siku ya jumatatu kwenye
Ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.
Meneja Mawasiliano Serikalini kutoka Tume ya Taifa ya
Mipango (NPC), Bw. Titus Kaguo (aliyesimama mbele, mwenye miwani) akitoa
ufafanuzi na majibu ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa na watumishi baada ya kuhitimisha
wasilisho la mada ya Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 lililotolewa
katika eneo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI leo tarehe 13/10/2025 jijini Dodoma.















