Tuesday, December 12, 2023

MHE. KIKWETE ASEMA USHIRIKIANO UTABORESHA OFISI YA NYARAKA ZANZIBAR

 MHE. KIKWETE ASEMA USHIRIKIANO UTABORESHA OFISI YA NYARAKA ZANZIBAR


Na. Lusungu Helela- Dar es Salaam 


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amewahakikishia Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi  Zanzibar  kuwa    Idara ya  Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa   ipo tayari kushirikiana na Ofisi ya Nyaraka Zanzibar inaboreshwa kwa maslahi mapana ya pande zote mbili  za Muungano.


Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Desemba 12, 2023 wakati akizungumza na Wajumbe wa Kamati hiyo walipotembelea ofisi za Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Kanda ya Mashariki zilizopo Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Kikwete ameeleza lengo la ziara ya Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi  Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi  Zanzibar kwenye ofisi za Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dar es Salaam ni kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kutunza na kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu za Taifa kwa maslahi ya vizazi vijavyo.


 “Tupo tayari kushirikiana nanyi ili kuhakikisha kumbukumbu na nyaraka za Waasisi wa Taifa letu zinalindwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya kutusaidia kufanya uamuzi wenye mwelekeo sahihi na kulinda maslahi ya  kizazi cha sasa na cha baadaye’’ amesisitiza Mhe. Kikwete


Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu, Jamal Kassim Ali ameiomba Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa kuunga mkono jitihada mbalimbali zitakazofanywa na Ofisi ya Nyaraka Zanzibar kwa lengo la kuiboresha na kuhakikisha kumbukumbu na Nyaraka za Viongozi Wakuu wa Zanzibar zinatunzwa na kuhifadhiwa kwa maslahi mapana ya Taifa.

“Ofisi yetu ni changa na hivi karibuni tutasherehekea miaka 60 ya mapinduzi, hivyo tuomba ushirikiano wenu wa namna bora ya kutunza kumbukumbu za viongozi mbalimbali hususani kumbukumbu za Hayati Abeid Aman Karume” alisema Mhe. Jamal Kassim Ali.


Naye, Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Machano Othman Said amesema kuwa utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka za taifa ni shughuli muhimu sana katika maendeleo ya nchi. Hivyo,
Mhe. Machano ameisihi Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa kuwa tayari kutoa elimu, vifaa na uzoefu wa namna bora ya kutumia teknolojia katika uendeshaji wa  Ofisi ya Nyaraka Zanzibar.


Naibu Waziri  Ofisi ya Rais,  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza   Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi  Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi  Zanzibar  waliofanya zaira leo katika   Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Kanda ya Mashariki Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kutunza na kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu



Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi  Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi  Zanzibar wakimsikiliza Mkurugenzi wa Vituo vya Kumbukumbu, Gasper Kileo wakati akiwaonesha baadhi ya Nyaraka na Kumbukuku muhimu zinazopatikana katika Ofisi hiyo  leo wakati walipotembelea  Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Kanda ya Mashariki Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kutunza na kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu


 Mwenyekiti  wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi  Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Machano Said   akizungumza na    Wajumbe wa Kamati  hiyo ya  Baraza la Wawakilishi  Zanzibar  waliofanya ziara  mara baada ya Naibu Waziri  Ofisi ya Rais,  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete kuwakaribisha  katika   Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Kanda ya Mashariki Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kutunza na kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu

Mwenyekiti  wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi  Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Machano Said   akiwa kwenye picha na  baadhi ya wajumbe wa  timu ya menejimenti ya Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa pamoja na   Wajumbe wa Kamati  hiyo ya  Baraza la Wawakilishi  Zanzibar  mara baada ya kufanya ziara  katika   Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Kanda ya Mashariki Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kutunza na kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu,  wa pili kulia ni Naibu Waziri  Ofisi ya Rais,  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete

 


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwaonesha baadhi ya  Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi  Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar baadhi ya hotuba ya  Baba wa Taifa  Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyoitoa wakati wa harakati za kudai uhuru wa Tanganyika  wakati Wajumbe  walipofanya ziara  leo ya kutembelea Ofisi ya Rais,  Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Kanda ya Mashariki Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kutunza na kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu,   

Mkurugenzi Mkuu  Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Firmin Msiangi    akiwaonesha Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi  Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi  Zanzibar baadhi ya Nyaraka muhimu zinazopatikana  katika   Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Kanda ya Mashariki Jijini Dar es Salaam wakati  Wajumbe wa Kamati hiyo wakati  wakifanya  ziara kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kutunza na kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu.


Naibu Waziri  Ofisi ya Rais,  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na  Mkurugenzi Mkuu  Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Firmin Msiangi mara baada ya kuwasili      katika   Ofisi ya Rais, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Kanda ya Mashariki Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kukutana na   Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi  Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi  Zanzibar  waliofanya ziara  leo Jijini Dar es Salaam


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiangalia baadhi ya  Wajumbe wa Kamati ya Kusimamia Ofisi za Viongozi  Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar baadhi ya hotuba ya  Baba wa Taifa  Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyoitoa wakati wa harakati za kudai uhuru wa Tanganyika  wakati Wajumbe  walipofanya ziara  leo ya kutembelea Ofisi ya Rais,  Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Kanda ya Mashariki Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kutunza na kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu,   

No comments:

Post a Comment