Tuesday, December 20, 2022

SERIKALI HAITOMVUMILIA KIONGOZI YEYOTE ATAKAYESHINDWA KUSIMAMIA VIZURI RASILIMALIWATU KWA USTAWI WA TAIFA

 Na. James K. Mwanamyoto-Kilosa

Tarehe 20 Disemba, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama amesema Serikali ya Awamu ya Sita haitosita kumchukulia hatua za kinidhamu na kisheria kiongozi yeyote atakayeshindwa kusimamia vizuri rasilimaliwatu kwa ajili ya ustawi wa taifa.

Mhe. Jenista amesema hayo, wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa umma katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro kilicholenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi katika halmashauri hiyo.

Mhe. Jenista amesema, hatomuonea aibu wala huruma kiongozi yeyote aliyepewa dhamana ya kusimamia rasilimaliwatu ambaye atabainika kukiuka sheria na taratibu za usimamizi wa rasilimaliwatu.

Mhe. Jenista ameongeza kuwa, viongozi wenye dhamana ya kusimamia rasilimaliwatu wanapaswa kuiheshimu, kuithamini na kuhakikisha inakuwa kwenye mikono salama kwasababu inategemewa na Serikali kwa kiasi kikubwa katika ustawi na maendeleo ya taifa.

“Rasilimaliwatu ambayo ndio watumishi wa umma ikisimamiwa vizuri itaisaidia Serikali kutimiza lengo la kutoa huduma bora kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kutekeleza mipango na mikakati ya maendeleo katika taifa,” Mhe. Jenista amefafanua.

Mhe. Jenista amesisitiza kuwa, watumishi wa umma ndio wanategemewa kutoa huduma bora za afya, kuboresha huduma za maji, kuboresha huduma za elimu, kuboresha huduma za miundombinu pamoja na kilimo. 

Akizungumza kwa niaba ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Kilosa, Mwalimu Richard Shagungu ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoongozwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kulipa kila mwezi madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi katika Halmashauri hiyo na kuomba waajiri wasizalishe madai mapya ili Serikali iyamalize madai yaliyopo sasa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama amefanya ziara ya kikazi ya siku moja katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ili kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma pamoja na kukagua utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika Halmashauri hiyo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro, wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi katika halmashauri hiyo.


Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi hao.


Mbunge wa Jimbo la Kilosa, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akitoa salaam za wananchi wa jimbo lake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa.


Mbunge wa Jimbo la Mikumi, Mhe. Dennis Londo akitoa salaam za wananchi wa jimbo lake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa.


Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Kilosa, Mwalimu Richard Shagungu akitoa shukrani kwa niaba ya Watumishi wa Kilosa kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kulipa madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiimba Wimbo wa Taifa na viongozi wengine walio meza kuu kabla ya kuzungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro, wakati ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi katika halmashauri hiyo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana baadhi ya viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, mara baada ya kuwasili Wilayani humo ili kuzungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri hiyo, wakati ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi walio katika halmashauri hiyo.



No comments:

Post a Comment