Friday, January 24, 2020

MHE. MKUCHIKA AKUTANA NA MAKAMISHNA WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA KUJADILIANA NAMNA YA KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO KATIKA MASUALA YA UTAWALA BORA




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akizungumzia namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora waliomtembelea ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma.
Baadhi ya Makamishna na Viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) wakati wa kikao kilichofanyika ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma leo kuzungumzia namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora.
Kaimu Katibu Mtendaji, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bi. Fatuma Muya akitoa maoni yake wakati wa kikao kazi cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) na Makamishna wa Tume hiyo kilichofanyika ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma leo kilichokuwa na lengo la kujadiliana namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) (wa tatu kutoka kushoto mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na baadhi ya watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora mara baada ya kikao kilichofanyika ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma leo kilichokuwa na lengo la kujadiliana namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akiagana na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bw. Mohamed Hamad baada ya kikao na Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kilichofanyika ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma leo. Kikao hicho kilikuwa na lengo la kujadiliana namna ya kufanya kazi kwa ushirikiano katika masuala ya utawala bora.

No comments:

Post a Comment