Friday, January 24, 2020

ELIMU YA MANUFAA YA HATIMILIKI ZA KIMILA ITOLEWE KWA WALENGWA WA MKURABITA


Naibu Waziri  Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa akizungumza na  wanakijiji wa Ntandabala kata ya Masoko Wilayani RUNGWE katika ziara ya kikazi ya kukagua mradi wa kurasimisha raslimali za wanyonge ( MKURABITA).

Baadhi ya Wazee na Vijana wa kijiji cha Ntandabala kilichopo Kata ya Masoko Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya wakimsikiliza, Naibu Waziri  Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa  alipokuwa akitoa ufafanuzi juu ya uamuzi wa serikali kuanzisha mpango wa kurasimisha raslimali za wanyonge (MKURABITA) na faida zake kwa wanufaika.

Baadhi ya akina Mama wa Kijiji cha Ntandabala kilichopo kata ya Masoko Wilayani Rungwe wakimshukuru  Naibu Waziri  Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa kwa kufanya ziara kijijini hapo na kutoa  maelekezo yatakayowasaidia kutatuliwa kero zao za kurasimishiwa maeneo yao na kunufaika na mikopo katika taasisi za fedha.

No comments:

Post a Comment