Tuesday, July 18, 2017

MAMLAKA ZA AJIRA NCHINI ZAAGIZWA KUREKEBISHA TAARIFA ZA WATUMISHI WA UMMA WANAOTARAJIA KUSTAAFU ILI WAPATE STAHILI ZAO KWA WAKATI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na viongozi na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo - Kata ya Ubungo alipofanya ziara ya kikazi katika Kata hiyo ili kupokea maoni, ushauri na kusikiliza kero za watumishi wa umma leo Jijini Dar es Salaam. 
Sehemu ya watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo - Kata ya Ubungo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) (Hayupo pichani) wakati wa kikao kazi na watumishi hao kilichofanyika leo Jijini Dar es Salaam.


Afisa TEHAMA wa Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Dotto Namkaa akiwasilisha mada kuhusu namna ya kujisajili katika Tovuti ya Watumishi (Watumishi Portal) wakati wa kikao kazi cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo -Kata ya Ubungo kilichofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Maji (Water Institute), Dkt. Shija Kazumba akiwasilisha hoja mbalimbali zinazowahusu watumishi wa umma kutoka taasisi anayoiongoza wakati wa kikao kazi cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo - Kata ya Ubungo kilichofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akifafanua hoja mbalimbali alizopokea kutoka kwa watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo - Kata ya Ubungo (hawapo pichani) wakati wa kikao kazi na watumishi hao leo Jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Kisare Makori na kushoto kwake ni Meya wa Manispaa ya Ubungo, Mhe. Boniface Jacob.




No comments:

Post a Comment