Monday, July 10, 2017

Waziri Kairuki akutana na Watumishi Halmashauri ya Wilaya ya Temeke Kuboresha Utendaji Kazi na Kushughulikia Kero za Watumishi

Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki akizungumza na Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke pamoja na baadhi ya watumishi kutoka katika wilaya hiyo (hawapo pichani) alipofanya ziara leo katika Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam kuadhimisha wiki ya utumishi wa umma iliyofanyika tarehe 16 hadi 23 Juni, 2017 na kupokea taarifa ya wilaya hiyo pamoja na kero za watumishi.


Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Felix J. Lyaniva akitoa taarifa ya wilaya yake kwa Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (hayupo pichani) wakati wa ziara yake wilayani hapo leo Jijini Dar es Salaam 
Baadhi ya watumishi kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Temeke wakifuatilia kwa makini yaliyokua yakiendelea wakati wa ziara ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki katika Halmashauri ya Wilaya ya Temeke leo Jijini Dar es Salaam kuhitimisha wiki ya utumishi wa umma iliyofanyika tarehe 16 hadi 23 Juni, 2017 na kupokea taarifa ya wilaya pamoja na kero za watumishi.


Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke Bw. Thabit Matha akichangia mada wakati wa ziara ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki katika Halmashauri ya Wilaya ya Temeke leo Jijini Dar es Salaam kuhitimisha wiki ya utumishi wa umma iliyofanyika tarehe 16 hadi 23 Juni, 2017 na kupokea taarifa ya wilaya pamoja na kero za watumishi.




Watumishi Halmashauri ya Wilaya ya Temeke wametakiwa kuzingatia mkataba wa huduma kwa mteja pale wanapohudumia wateja na kushughulikia kero za wananchi kwa wakati ili waweze kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano.
Rai hiyo imetolewa na Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Temeke katika kuadhimisha wiki ya utumishi wa umma iliyofanyika tarehe 16 hadi 23 Juni, 2017 na kupokea taarifa ya wilaya hiyo pamoja na kero za watumishi leo Jijini Dar es Salaam.
Katika kuboresha maslahi ya watumishi Mhe. Kairuki ametoa wito kwa waajiri kurekebishe taarifa za watumishi wote waliokaribia kustaafu na wale ambao wamepandishwa vyeo bila kulipwa stahili zoa ili waweze kulipwa stahili hizo kabla ya kustaafu, huku akiwataka wale waliokwisha staafu wakiwa na barua za kupandishwa vyeo kujaza fomu kupitia kwa waajiri wao ili waweze kupata stahili zoa kwani hakuna haki na stahili ya mtumishi wa umma itakayopotea.
Aidha mhe. Kairuki amewataka watumishi wote wa umma kujisajiri katika tovuti ya watumishi (watumishi portal) ili wawe na uwezo wa kuona taarifa zao za kiutumishi na kuweza kufuatilia masuala yao ya kiutumishi yamefikia katika hatua gani.
“Maafisa utumishi na ofisi ya katibu tawala hakikisheni kuwa taarifa zote za kwenye mfumo zinakua ni taarifa safi na zilizo kamilika kwa kuhakikisha kwamba watumishi wana tarehe kamili na sahihi za kuzaliwa, tarehe zao za ajira, tarehe zao za kila mara walipopandishwa vyeo, taarifa zao za mifuko kwenye hifadhi ya majii, sifa zao za kielimu, vyeo walivyonavyo pamoja na masuala mengine” Amesema Mhe. Kairuki
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Felix J. Lyaniva amemhakikishia Mhe.  Kairuki kuwa Halmashauri yake imejitahidi kusimamia kwa karibu watendaji wake jambo ambalo limeboresha utoaji wa huduma kwa wateja kwa wakati lakini pia kuhakikisha kuwa watumishi wake wanafiki ofisini mapema kwa kuwahamasisha kuishi maeneo ya karibu na kituo chao cha kazi.
Akichangia mada wakati wa ziara hiyo Mwalimu Mkuu kutoka shule ya Msingi Yombo Dovya Bw. Godwin Jerome Mselle amemuomba Mhe. Kairuki kuangalia namna ambavyo walimu wote watakavyowezeshwa kupata mafunzo kazini ili waweze kwenda sambamba na mitaala mipya tofauti na inavyofanywa kwa sasa kwa kupeleka walimu wachache kupata mafunzo hayo na kuja kufundisha walimu wengine jambo ambalo halifanywi kwa ufasaha kama ambavyo walimu wote wangepata mafunzo hayo kwa pamoja kutoka kwa wataalamu.


No comments:

Post a Comment