Thursday, November 24, 2022

TASAF YATEKELEZA MAELEKEZO YA MHE. RAIS YA KUJENGA BARABARA KWA GHARAMA NAFUU KIJIJI CHA NANGOSE AMBAZO HAZIKUWAHI KUJENGWA TANGU TAIFA LIPATE UHURU

Na. James K. Mwanamyoto-Masasi

Tarehe 24 Novemba, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama amesema, Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) umetekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya kujenga barabara zenye urefu wa kilometa 1.6 kwa gharama nafuu katika Kijiji cha Nangose, Kata ya Temeke, Halmashauri ya Mji wa Masasi ambazo hazikuwahi kujengwa tangu taifa lipate uhuru. 

Mhe. Jenista amesema hayo wakati akizungumza na walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na wananchi wa Kijiji cha Nangose mara baada ya kukagua barabara hizo zilizojengwa na TASAF kupitia mradi wa ajira za muda. 

Mhe. Jenista amesema, Serikali ya Awamu ya Sita imeweza kujenga barabara zenye urefu wa Kilometa 1.6 katika Kijiji cha Nangose, ambapo tangu nchi ipate uhuru hakukuwa na barabara zaidi ya kuwepo na njia za miguu ambazo zilikuwa ni kikwazo cha kijiji hicho kupata maendeleo. 

“Barabara hizi zimejengwa kupitia mradi wa ajira za muda kwa gharama nafuu sana ambayo ni kiasi cha shilingi milioni 3.6, ambapo fedha hiyo ililipwa kwa walengwa wa TASAF waliokuwa wakifanya kazi kwenye mradi wa ujenzi wa barabara hizo,” Mhe. Mhagama amefafanua. 

Katika kuhakikisha barabara hizo zinakuwa na tija kwa maendeleo ya wananchi katika kijiji hicho, Mhe. Mhagama amemtaka Meneja wa TARURA Halmashauri ya Mji Masasi kuimarisha barabara hizo ili zitumike kwa muda mrefu na kuwa chachu ya maendeleo katika Kijiji cha Nangose. 

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Mhe. Claudia Kitta amesema kuwa wananchi wa Kijiji cha Nangose ambao ni walengwa wa TASAF wamefanya kazi ya ujenzi wa barabara hizo zenye urefu wa kilomita 1.6 kupitia mradi wa ajira za muda, na kuongeza kuwa katika Halmashauri ya Mji Masasi zipo barabara 40 ambazo zimejengwa na TASAF kupitia mradi huo wa ajira za muda. 

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Kijiji cha Nangose, Diwani wa Kata ya Temeke kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe. Frank Malanjila amesema kabla ya TASAF kuwezesha ujenzi wa barabara katika kata yake, kulikuwa na changamoto kubwa lakini kwasasa barabara zilizojengwa zimeunganisha vijiji na kuwawezesha wananchi kutoka eneo moja kwenda jingine, ikiwa ni pamoja na kusafirisha bidhaa na mazao yao kwa urahisi tofauti na ilivyokuwa hapo awali. 

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi huo wa TASAF wa ajira za muda, Mtendaji wa Kijiji cha Nangose, Bi. Salma Ngatimwa amesema, mradi ulibuniwa na wananchi na kutekelezwa kwa kipindi cha miezi sita kuanzia Septemba 2021 hadi Februari 2022 na kuongeza kuwa, walengwa walianza kutekeleza mradi huo wa ujenzi wa barabara kwa kusafisha eneo, kung’oa miti na kutengeneza mifereji.

 

1.  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akikagua barabara iliyojengwa na walengwa wa TASAF kupitia mradi wa ajira za muda katika Kijiji cha Nangose Kata ya Temeke, Halmashauri ya Mji Masasi wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani Masasi


1. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na wananchi wa Kijiji cha Nangose Kata ya Temeke, Halmashauri ya Mji Masasi wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani Masasi.


1. Sehemu ya Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na Wananchi wa Kijiji cha Nangose Kata ya Temeke Halmashauri ya Mji Masasi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF Wilayani Masasi


1.  Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Mhe. Claudia Kitta akitoa neno la utangulizi kuhusiana na utekelezaji wa miradi ya TASAF katika wilaya yake kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama kuzungumza na walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na wananchi wa Kijiji cha Nangose Kata ya Temeke Halmashauri ya Mji Masasi wakati wa ziara ya kikazi ya Mhe. Jenista ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani Masasi.  


1. Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Nangose Kata ya Temeke, Halmashauri ya Mji Masasi, Bi. Salma Ngatimwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wa Kijiji cha Nangose kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF Wilayani Masasi.


1. Diwani wa Kata ya Temeke kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe. Frank Malanjila akiishukuru Serikali kwa kujenga barabara kupitia TASAF wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika kata yake. 


1.  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Diwani wa Kata ya Temeke kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe. Frank Malanjila (hayupo pichani) alipokuwa akiishukuru Serikali kwa kujenga barabara kupitia TASAF katika kata yake wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Jenista iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani Masasi. 


1.    Mwananchi wa Kijiji cha Nangose, Kata ya Temeke, Halmashauri ya Mji Masasi, Bw. Daniel Maulana akiwasilisha hoja kuhusiana na utekelezaji wa miradi ya TASAF kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Jenista iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani Masasi.


1.  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na watendaji wa Wilaya ya Masasi alipowasili wilayani humo kwa ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani humo.


 

No comments:

Post a Comment