Tuesday, June 21, 2016

WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2016 : MATUKIO KATIKA PICHA MKOANI KILIMANJARO

Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza na watumishi wa umma wa Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa ni muendelezo wa ziara zake katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma 2016. 
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza na Menejimenti ya Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2016 Mkoani Kilimanjaro. Mhe. Kairuki amesisitiza Maafisa Rasilimaliwatu wafanye kazi kwa weledi na watakaoshindwa hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yao.

Baadhi ya Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Kilimanjaro wakimsikiliza Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (hayupo pichani) wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2016 Mkoani Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment