Friday, June 17, 2016

WAZIRI KAIRUKI AZINDUA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KWA KUFANYA VIKAO KAZI NA WATUMISHI WA MKOA WA SINGIDA

WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2016: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mh. Angellah Kairuki (Mb) akitoa maelekezo kwa Watendaji wa Mkoa wa Singida wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Sehemu ya Watumishi wa Umma mkoani Singida wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mh. Angellah Kairuki (Mb), (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2016, mkoani Singida.

Mkurugenzi wa Utawala katika Utumishi wa Umma, Bw. Nyakimura Muhoji akifafanua masuala yanayohusu Utumishi wa Umma wakati wa kikao kazi na Watumishi wa Umma mkoano Singida. Kikao hicho ni moja ya matukio ya Wiki ya Utumishi wa Umma inayoendelea hadi Tarehe 23 Juni.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akipokea Ripoti ya Utendaji wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Tawi la Singida kutoka kwa Kaimu Mtendaji Mkuu wa chuo hicho Dkt. Henry Mambo, wanaoshuhudia ni Kaimu Mkurugenzi wa Mipango, Fedha na Utawala wa TPSC Bw. Rajabu Mirambo na Mkurugenzi wa TPSC Tawi la Singida Bw. Ramadhani Marijani (kushoto mwisho)

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mh. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza na Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Singida (hawapo pichani) katika siku ya kwanza ya Wiki yaUtumishi wa Umma mwaka 2016, mkoani Singida, kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Mathew Mtigumwe, Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Angelina Lutambi na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhe. Saidi Amanzi

PICHA YA PAMOJA TPSC: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma naUtawala Bora, Mh. Angellah Kairuki (Mb) (wa pili kulia aliyekaa) katika picha ya pamoja na Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tawi la mkoani Singida mara baada ya kikao kazi na watumishi hao ikiwa ni moja ya matukio katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2016.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (MB.) amewataka Watumishi wa Umma nchini waliopewa dhamana serikalini kutekeleza majukumu yao kwa weledi mkubwa ili kuepuka malalamiko yasiyo ya lazima kwa wanaowahudumia.

Waziri Kairuki aliyasema hayo jana alipokuwa akizindua Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2016 mkoani Singida.

“Najua miongoni mwa watumishi wa umma wapo watumishi waliopewa dhamana lakini utoaji wao wahuduma unatiliwa shaka. Hawapendi kusikiliza matatizo ya wateja wa ndani yaani watumishi wenzao,” Mhe. Kairuki alisema.
Amewataka watumishi wenye tabia hizo kuacha mara moja na kuishi maisha ya kazi kama Mkataba wa Huduma kwa Mteja unavyowaongoza katika kutoa huduma kwa kiwango kwa wateja wote wa ndani na nje ya taasisi.

Aidha, Mhe. Kairuki amewataka Watendaji kutenga muda wa kukaa na watumishi wao ili kusikiliza kero na changamoto zinazowakabili kwa lengo la kuzitafutia ufumbuzi.

“Uzoefu unaonyesha kuwa watumishi wanaposhirikishwa katika masuala yanayowagusa kama tulivyo hapa basi huduma kwa wananchi na wadau wengine zitaboreka na kazi kufanyika kwa ari na hivyo kuongeza tija na ufanisi kazini,” Waziri Kairuki aliongeza.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kairuki alifanya ziara katika Chuo cha Utumishi wa Umma tawi la Singida na kuzungumza na watumishi wa chuo hicho ambapo aliwataka watumishi hao kuwa wabunifu katika kutekeleza majukumu yao na kuwajibika ili kuleta matokeo bora kwa taifa.

“Tuwewabunifu, tuangalievipaumbele, tufundishe kozi ambazo hazifundishwi sehemu nyingine ili kuweza kupata soko zuri zaidi,” Waziri Kairuki alisisitiza.
Aliwasisitiza watumishi hao kuwa na ushirikiano na vyuo mbalimbali hasa katika nyanja za utafiti, mafunzo na masuala mengine ya maendeleo ili kuboresha chuo hicho.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo hufanyika kuanzia tarehe 16-23 Juni, kila mwaka, kwa mwaka 2016 yanafanyika kwa namna tofautia mbapo Viongozi na Watendaji wanakutana na wateja wao wa ndani na nje ya taasisi zao kwa lengo na kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi.

Katika kutekeleza hilo, Mhe. Kairuki amezindua maadhimisho hayo kwakufanya vikao kazi na watumishi wa mkoa wa Singida kutoka katika kada mbalimbali za utumishi wa umma.

Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Barani Afrika kwa mwaka 2016 ni “Uongozi wa Umma kwa ukuajiJumuishi: kuelekea katika Afrika tunayoitaka.”


Kaulimbiu hiyo inaambatana na kaulimbiu ndogo ambazo ni: Mchango wa Utumishi wa Umma katika Ukuaji wa Uchumi Barani Afrika na Mchango wa Utumishi wa Umma katika Kuiwezesha Ajenda ya Afrika ya 2063 ambayo inaweka mkazo katika Maendeleo ya Afrika na Haki za Wanawake.

No comments:

Post a Comment