Wednesday, June 24, 2015

KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2015 CHAFANA

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Utumishi Bw. HAB Mkwizu (kushoto) akihutubia wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2015 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam jana.

Moja kati ya washindi wa tuzo za Wiki ya Utumishi wa Umma 2015 wakifurahia tuzo waliyoipata wakati wa kilele za Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2015 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam jana.

Baadhi ya Watumishi wa Umma na wananchi waliohudhuria kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2015 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam wakimsikiliza mgeni rasmi Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Pili Mh. Ali Hassan Mwinyi (hayupo pichani) jana.

Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Pili Mh. Ali Hassan Mwinyi  (wa pili kutoka kushoto) akitembelea mabanda katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2015  katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam jana. Anayemuongoza ni Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Utumishi Bw. HAB Mkwizu (watatu kutoka kushoto).

Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Pili Mh. Ali Hassan Mwinyi (kushoto) akimkabidhi tuzo mmoja wa wawakilishi wa taasisi zilizopata tuzo wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2015 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam jana.

Tuzo zilizokabidhiwa Siku ya Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma jana tarehe 23 Juni, 2015.

Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Pili Mh. Ali Hassan Mwinyi  (wa pili kutoka kushoto) akitembelea mabanda katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2015  katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam jana. Anayemuongoza ni Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Utumishi Bw. HAB Mkwizu (watatu kutoka kushoto).

No comments:

Post a Comment