Friday, June 24, 2016

KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2016 , DODOMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akitoa ufafanuzi kuhusu hoja zilizowasilishwa na Watumishi wa Umma mkoani Dodoma wakati wwa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2016 
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Mathias B. Kabunduguru (kushoto) akijadili jambo wakati wa kikao na Menejimenti ya Mkoa wa Dodoma. Kulia ni Waziri wa Nchi-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angellah Kariuki (Mb), na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana

KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2016 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akihutubia Watumishi wa Umma mkoani Dodoma.

KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2016 -MATUKIO,-DODOMA. Watumishi wa Umma mkoani Dodoma wakisikiliza Hotuba ya Waziri wa Nchi-Utumishi na Utawala Bora (hayupo pichani)

KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2016 -MATUKIO,-DODOMA. Watumishi wa Umma mkoani Dodoma wakisikiliza Hotuba ya Waziri wa Nchi-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki (Mb) 

Thursday, June 23, 2016

MATUKIO KATIKA PICHA:SIKU YA KILELE CHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2016 ,OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA

Afisa Malalamiko wa Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. James Katubuka (kulia) akihudumia mteja katika Siku ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2016 iliyofanyika Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma. 
Wateja wakihudumiwa katika Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ikiwa ni Siku ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2016.

UTUMISHI YAWAAGA WATAALAMU 7 WA KUJITOLEA KUTOKA JAPANI WALIOMALIZA MUDA WA KUTOA HUDUMA NCHINI

Mtaalamu wa kujitolea kutoka nchini Japan, Bi.Yuka ITO, akielezea namna alivyofanya kazi katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara (Ligula) wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wataalam wa kujitolea kutoka nchini Japan waliomaliza muda wao. Hafla hiyo ilifanyika ukumbi wa Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo. 
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- Utumishi, Bw.Mick Kiliba (kulia) akifuatilia maelezo ya Bi. Yuka ITO ya namna alivyofanya kazi katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara (Ligula) wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wataalam wa kujitolea kutoka nchini Japan waliomaliza muda wao iliyofanyika  ukumbi wa Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo.

Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Mick Kiliba (kushoto) akikabidhi zawadi kwa Mtaalam wa Kujitolea kutoka nchini Japani Bw. Kosuke MATSUDA aliyemaliza muda wake wa kutoa huduma nchini  katika hafla fupi ya kuwaaga wataalam hao iliyofanyika ukumbi wa Ofisi ya Rais-Utumishi mapema leo.