Monday, September 16, 2024

MHE. SIMBACHAWENE AWAASA WAHITIMU KUSHIKA ELIMU KWA UJENZI WA TAIFA ENDELEVU.

 Na. Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amewaasa wahitimu wa darasa la Saba kushika elimu kwa kuwa elimu ni msingi wa maisha na inajenga taifa endelevu.

Mhe. Simbachawene alisema kuwa, Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua umuhimu wa elimu kwa taifa, hivyo, amewekeza zaidi katika elimu ikiwa ni jitihada za kuendelea kupambana na maadui watatu wa Taifa ambao ni ujinga, umasikini na maradhi.

Aidha, aliwakumbusha kuwa msomi ni mtu yeyote ambaye amefuta ujinga, anaweza kusoma na kuandika na kutanzua mambo yanayomkabili, hivyo elimu ni muhimu na ndiyo mana Serikali ya Awamu ya Sita imeamua kutoa elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha sita.

“Ninawasihi musome kwa bidii ili msije mkajuta hapo baadae katika maisha yenu, ukiwa na elimu utaishi maisha ya kufuata Sheria za nchi, utaheshimu watu, utakuwa na hekima na busara ya kutawala maisha yanayokuzunguka” alisistiza Mhe. Simbachawene.

Katika hotuba yake kwa wahitimu hao wa darasa la saba kwenye Mahafali ya 60 ya Shule ya Msingi Kaloleni iliyopo Kata ya Majengo Jijini Dodoma, Mhe. Simbachawene aliwataka wahitimu hao kutokatishwa tamaa na watu wasiopenda elimu kwa kuwa elimu ni msingi wa utendaji kazi na maendeleo.

Pia, alisema watu wengi wanapotosha sana dhana ya elimu na hivyo kuwakatisha tamaa vijana kuendelea na masomo. Alifafanua kuwa hakuna uhusiano kati ya kusoma na kuwa na pesa, hata wasiosoma wana haki ya kuwa na pesa, suala la maisha mazuri ni bahati na mipango ya mtu binafsi, hakuna uhusiano na elimu.

“Ukiwa na elimu unaweza kuwa na njia bora za kwenda kwenye maisha mazuri kwa sababu anaweza kufanya uamuzi kwa usahihi kuliko yule ambaye hajasoma na wenye pesa wanatumia wasomi kupata pesa zaidi hususani katika masuala ya uvuvi, kilimo, ufugaji na biashara kwa jumla” aliongeza Mhe. Simbachawene.

Vilevile, amewapongeza walimu wote Tanzania kwa kufanya kazi vyema ya kufundisha vema na ameahidi kusimamia na kuangalia maslahi ya walimu hao kwa kuwa wanafanya kazi kubwa sana ya kujenga taifa la kesho.

Katika risala  ya wahitimu ilibainisha kuwa, shule ya msingi Kaloleni inamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100, ilianzishwa mwaka 1958 ina walimu 18 kati yao wakiume 5 wakike 13. Idadi ya wanafunzi ni 845 wavulana 441 wasichana 404. Hivyo, jumla ya wanafunzi 104 wamehitimu darasa la Saba ikiwa wavulana 48 na wasichana 56.

Hali kadhalika, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Mwl. Emmanuel S. Enock alimshukuru Waziri Mhe. George Simbachawene kwa kujumuika na familia ya Kaloleni kwenye mahafali ya 60 licha ya kuwa na majukumu mengi ya kijamii na kitaifa.

Mwl. Emmanuel aliongeza kuwa Shule ya Msingi Kaloleni ni eneo salama kwa malezi ya watoto, kwani inaandaa watoto vyema kinadharia na kivitendo kutokana na umahiri mkubwa wa walimu wenye uwezo wa kufundisha, moyo wa upendo, huruma na uchu wa kuelimisha watoto ili kupata taifa imara na lenye wasomi.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akizungumza na Wahitimu wa Darasa la Saba na Wazazi (hawapo pichani) wakati wa Mahafali ya 60 ya Shule ya Msingi Kaloleni Jijini Dodoma.

Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kaloleni wakifuatilia matukio ya Mahafali ya 60 ya Darasa la Saba katika Shule ya Msingi Kaloleni Jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akimkabidhi cheti na zawadi mmoja wa Wahitimu wa Darasa la Saba wakati wa Mahafali ya 60 ya Shule ya Msingi Kaloleni Jijini Dodoma.

Baadhi ya Wazazi wakifuatilia matukio kwenye Mahafali ya 60 ya Darasa la Saba katika Shule ya Msingi Kaloleni Jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu wa Darasa la Saba wa Shule ya Msingi Kaloleni wakati wa Mahafali ya 60 ya Shule ya Msingi Kaloleni Jijini Dodoma.








Tuesday, September 10, 2024

MHE. SIMBACHAWENE AMTEMBELEA MAMA SITTI MWINYI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amemtembelea Mama Sitti Mwinyi nyumbani kwake Mikocheni Jijini Dar es Salaam leo Septemba 10, 2024.

“Rais, amenielekeza kuwafikishia salaam zake na amesema yuko pamoja nanyi na ndio mana amenituma kufika hapa nyumbani na kuwajulia hali, kusikiliza changamoto zilizopo na kuzitafutia ufumbuzi” amesema Mhe. Simbachawene.

Mhe. Simbachawene amesema Rais Mhe. Dkt. Samia anathamini sana mchango wa Viongozi Wakuu wa Kitaifa waliomtangulia na ataendelea kusimamia na kutunza familia hizo kwa mujibu wa Katiba na Sheria.

Aidha, Mama Sitti amemshukuru Mhe. Simbachawene kwa kupata nafasi ya kumtembelea na kumjulia hali na amempongeza Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuijali familia yake wakati wote bila kuchoka na amemuombea kwa Mungu aendelee kutumia hekima na busara katika kuiongoza Tanzania.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Mama Sitti Mwinyi wakati alipomtembelea nyumbani kwake Mikocheni Jijini Dar es Salaam Septemba 10, 2024



Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na Mama Sitti Mwinyi wakati alipomtembelea nyumbani kwake Mikocheni Jijini Dar es Salaam Septemba 10, 2024


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akisalimiana na Mama Sitti Mwinyi wakati alipomtembelea nyumbani kwake Mikocheni Jijini Dar es Salaam Septemba 10, 2024


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na Mama Sitti Mwinyi wakati alipomtembelea nyumbani kwake Mikocheni Jijini Dar es Salaam Septemba 10, 2024


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene wakifuatilia jambo na Mama Sitti Mwinyi wakati alipomtembelea nyumbani kwake Mikocheni Jijini Dar es Salaam Septemba 10, 2024


 

MHE. SIMBACHAWENE ATETA NA RAIS KIKWETE

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene leo amemtembelea na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya M. Kikwete nyumbani kwake Kawe Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo, Mhe. Simbachawene amefikisha salaam za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ameahidi kuendelea kuwa pamoja na Viongozi Wakuu Wastaafu wa Kitaifa kwa maendeleo ya taifa.

Mhe. Simbachawene amesema Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ina jukumu la kutunza Viongozi Wakuu Wastaafu Kitaifa na Wenza wao, hivyo yuko tayari kuendelea kutekeleza jukumu hilo alilopewa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ufanisi.

Hali kadhalika, Mhe. Dkt. Kikwete amemshukuru Mhe. Simbachawene kwa ujio huo na kupongeza utaratibu uliopo wa kuwatembelea Wiongozi Wakuu Wastaafu wa Kitaifa kwa kuwa unawapa faraja, unaonesha thamani na mchango wao kwa maendeleo ya taifa.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiteta na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete nyumbani kwake Kawe Jijini Dar es Salaam.








Thursday, September 5, 2024

MHE. SANGU: UADILIFU NI MSINGI WA USALAMA WA TANZANIA

Na. Mwandishi Wetu

Septemba 5, 2024

“Tuwawajibishe au kuachana na watumishi wasiokuwa waadilifu kwa kuwa sisi ndio tunaotakiwa kusimamia uadilifu lakini miongoni mwetu tunakuwa na watu wasiokuwa waadilifu”

Maneno hayo yamesemwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu wakati akiongea na viongozi na watumishi wa TAKUKURU makao makuu Dodoma.

Amewakumbusha Viongozi na watumishi hao kuwa suala la uadilifu limeandikwa hata katika vitabu vya dini zote ambapo likizingatiwa kwa usahihi amani na utulivu hutamalaki miongoni mwa wananchi.

Alisema, TAKUKURU ni taasisi muhimu na nyeti katika taifa la Tanzania na msingi wake ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lengo ikiwa ni kuzuia na kupambana na rushwa katika jamii. Hivyo, Viongozi na watumishi wote wa Umma wakiongozwa na TAKUKURU hawanabudi kumuunga mkono Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mapambano hayo.

Mhe. Sangu ametoa rai kwa TAKUKURU kuangalia kwa kwa makini eneo la Ununuzi wa Umma ambapo zaidi ya asilimia 70 ya bajeti ya Serikali inaelekezwa katika eneo hilo. Hivyo, eneo hilo lazima litazamwe na kupewa kipaumbele ili kuziba mianya ya rushwa.

Aliongeza kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepeleka fedha nyingi kwenye miradi ya maendeleo Tanzania nzima, hivyo ameielekeza TAKUKURU kufuatilia na kusimamia vyema miradi hiyo ili kuhakikisha inatekelezwa kwa mujibu wa mikataba.

Naye, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Ikulu Bw. Mululi Majula Mahendeka amesema TAKUKURU ni muhimu kwa usalama wa nchi hasa katika kuzuia na kupambana na rushwa.

“Rushwa ikishamili na usalama wa nchi unateteleka kwa kuwa wananchi wanakosa imani na Serikali yao, hivyo  ametoa wito  kwa watumishi hao kufanya kazi kwa juhudu na maarifa ili Serikali iendelee kuiaminika kwa umma” alisisitiza Bw. Mahendeka.

Alibainisha kuwa, usiri na utengano sambamba ni jambo la msingi katika uendeshaji wa shughuli za Serikali na mambo hayo yasipozingatiwa na kutiliwa mkazo yanaweza kubomoa msingi wa umoja wa Taifa ambao uliwekwa na unaendelea kusimamiwa vyema na Viongozi wetu wakuu.

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Crispin Chalamila alimuahidi Mhe. Sangu kupata ushirikiano wa dhati kutoka kwa Viongozi na Watumishi wa TAKUKURU ili kutekeleza majukumu aliyopewa kwa ufanisi.

Pia, alimuomba Mhe. Sangu kufikisha salaamu za shukurani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akizungumza na Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakati wa ziara yake ya kikazi iliyofanyika jijini Dodoma.

Baadhi ya Watendaji na Watumishi na wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi.

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila akielezea utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyofanyika jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila (hayupo pichani) wakati akielezea utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo alipofanya ziara ya kikazi. Kulia ni Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Majula Mahendeka.

 

Baadhi ya Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akipokea baadhi ya vitendea kazi vya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakati alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi hiyo jijini Dodoma kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa majukumu na kuhimiza uwajibikaji.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akisalimiana na baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakati alipowasili katika ofisi hiyo kwa ziara ya kikazi jijini Dodoma.

Kwaya ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ikitoa elimu kupitia nyimbo wakati Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu alipofanya ziara katika ofisi hiyo kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa majukumu na kuhimiza uwajibikaji.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watendaji wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dodoma.






MHE. SANGUA AWATAKA WATUMISHI eGA KUFANYA KAZI KWA UZALENDO NA UADILIFU

 Na. Mwandishi Wetu

Septemba 5, 2024

“Nimekuja kujifunza na kuhimiza masuala ya uadilifu, uzalendo na namna bora ya kutoa huduma kwa umma, kwa kuwa watumishi wa mamlaka hii wanawajibu wa kusanifu, kujenga na kusimamia mifumo ya TEHAMA Serikalini ili  Serikali iweze kutoa huduma kwa umma kwa urahisi, haraka na gharama nafuu”.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu Septemba 5, 2024 jijini Dodoma wakati alipotembelea ofisi za Mamlaka ya  Serikali Mtandao (eGA) lengo la kujifunza namna taasisi hiyo inavyofanya kazi na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao.

Mhe. Sangu alieleza kuwa Mamlaka ya Serikali ni muhimu sana kwa ustawi wa taifa, hivyo watumishi wake hawanabudi kuzingatia misingi ya uadilifu na uzalendo kwa kuwa taarifa nyingi za Serikali zinapita katika mifumo waliyoijenga na wanayoisimamia.

Aidha, aliongeza kwa kutoa pongezi kwa watumishi wa eGA kwa kuifanya Serikali kuwa ya kidijitali na kurahisisha utoaji wa huduma kwa umma, mathalani mifumo iliyosanifiwa na kujengwa na eGA imeondoa upendeleo katika ajira za Serikali, wananchi wanaweza kulipia na kupata huduma mbalimbali wakiwa mahali popote na kwa wakati wowote.

Pia, alisisitiza  watumishi wa Mamlaka hiyo kuendelea kuhimiza taasisi za umma  kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya Serikali Mtandao katika utekelezaji wa jitihada za Serikali Mtandao kwa lengo la kuimarisha usalama wa mifumo ya Serikali na ya sekta binafsi iliyounganishwa na Serikali.

Awali, Katibu Mkuu-IKULU Bw. Mululi Majula Mahendeka alisema kuwa watumishi wa eGA wanatakiwa kufanyakazi kwa weledi na uadilifu ili kuifanya mifumo ya Serikali kuwa imara na inayoaminika kwa wananchi.

Vilevile, Mkurugenzi Mkuu wa eGA Eng. Benedict Ndomba alisema kuwa pamoja na mambo mengine mamlaka imeshirikiana na taasisi husika kujenga Mfumo wa kielektroni wa Usimamizi wa Vyama vya Ushiriki (MUVU) ambao unarahisisha ukaguzi, usimamizi na uendeshaji wa Vyama vya Ushirika ili kuboresha utendajikazi, kuchochea mabadiliko ya kiuchumi na kuongeza uwazi na uwajibikaji.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akizungumza na Watumishi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wakati wa ziara yake ya kikazi iliyofanyika jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi jijini Dodoma.



Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Majula Mahendeka akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu kuzungumza na Watumishi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyofanyika jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba akielezea mafanikio na utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyofanyika jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akisalimiana na baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wakati alipowasili katika ofisi hiyo kwa ziara ya kikazi jijini Dodoma.







Tuesday, September 3, 2024

WIZARA KUPIMWA KWA UTEKELEZAJI WA MWONGOZO WA UJUMUISHAJI WA JINSIA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

 Na Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 03 Septemba, 2024

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi amezitaka Wizara zote kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mwongozo wa Ujumuishaji wa Jinsia katika Utumishi wa Umma kila mwisho wa mwaka katika Ofisi hiyo ili kuhakikisha Mwongozo huo unatekelezwa kwa ufanisi kama ilivyokusudiwa na Serikali.

Bw. Daudi amezungumza hayo leo wakati akifunga semina elekezi ya siku mbili ya Mwongozo wa Ujumuishaji wa Jinsia katika Utumishi wa Umma kwa Wakurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Wizara pamoja na Waratibu wa Jinsia Ngazi ya Wizara iliyofanyika jijini Dodoma.

Amesema kuwasilisha taarifa ya utekelezaji na kupimwa kila mwisho wa mwaka ni suala la lazima kwani kuongea ni suala lingine na utekelezaji ni suala lingine, hivyo ni lazima wapimwe ili kuona namna mwongozo huo unavyotekelezwa kwa maslahi mapana ya taifa.

Aidha, Naibu Katibu Mkuu huyo amewataka Wakurugenzi hao na Waratibu wa Madawati ya Jinsia kutekeleza Mwongozo huo kwa kushirikiana na Idara na Vitengo vilivyo ndani ya Wizara zao kwani ukiwa shirikishi utekelezaji wake unakuwa ni rahisi na wa haraka. 

Vile vile amezielekeza taasisi zilizo chini ya Wizara zote kutekeleza Mwongozo huo kupitia Wakurugenzi hao ambao ni wawakilishi kwa sababu Serikali haitoweza kumwita kila mmoja na kutoa semina hiyo.

“Sasa haya ni maelekezo, kwasababau sisi hatuna uwezo wa kumwita kila mmoja mahali hapa, ninyi ni wawakilishi wenye nguvu kubwa, hivyo haya tunayoyasema mahali hapa mkiyafikisha kwa wenzetu wa taasisi, itakuwa jambo jema kwani kwa kufanya hivyo Serikali itatekeleza mambo yake kwa ufanisi mkubwa”

Semina elekezi ya Mwongozo wa Ujumuishaji wa Jinsia katika Utumishi wa Umma kwa Wakurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara zote na Waratibu wa Ujumuishwaji Jinsia ngazi ya Wizara imefanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 2 hadi 3 Septemba, 2024 katika Ukumbi wa Kambarage uliopo Wizara ya Fedha jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akizungumza na Wakurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara zote na Waratibu wa Ujumuishwaji Jinsia ngazi ya Wizara wakati akifunga semina elekezi ya Mwongozo wa Jinsia katika Utumishi wa Umma.

Wakurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara zote na Waratibu wa Ujumuishwaji Jinsia ngazi ya Wizara wakisikiliza mada kuhusu Mpango Kazi wa Utekelezaji wa Masuala ya Jinsia mahali pa Kazi wakati wa semina elekezi ya Mwongozo wa Jinsia katika Utumishi wa Umma 

Afisa Mipango Mwandamizi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Staricko Nyikwa akiwasilisha mada kuhusu Mwongozo wa Ujumuishwaji wa Jinsia katika Utumishi wa Umma (2023) kwenye semina elekezi ya Mwongozo wa Jinsia katika Utumishi wa Umma kwa Wakurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara zote na Waratibu wa Ujumuishwaji Jinsia ngazi ya Wizara.

Wawezeshaji katika semina elekezi ya Mwongozo wa Jinsia katika Utumishi wa Umma wakijadili jambo na kupitia nyaraka zao kabla ya kuwasilisha mada kwa Wakurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara zote na Waratibu wa Ujumuishwaji Jinsia ngazi ya Wizara.

Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Nyasinde Mukono (katikati) akijadili namna ya kuandaa Mpango Kazi wa Masuala ya Jinsia Mahali pa Kazi na Mratibu wa Ujumuishwaji Jinsia ngazi ya Wizara kutoka katika ofisi hiyo Bw. Kokolo Lusanda (wa kwanza kushoto) wakati wa semina elekezi ya Mwongozo wa Jinsia katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Mary Mwakapenda (kulia) na Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Ufuatiliaji wa Uzingatiaji wa Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Janet Mishinga (kushoto) wakifurahia jambo wakati wa semina elekezi ya Mwongozo wa Jinsia katika Utumishi wa Umma iliyoshirikisha Wakurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara zote na Waratibu wa Ujumuishwaji Jinsia ngazi ya Wizara.

Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu masuala ya Bajeti iliyokuwa ikitolewa na Prof. John Jeckoniah kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) wakati wa semina elekezi ya Mwongozo wa Jinsia katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma. 

Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Usimamizi wa Rasilimawatu Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Jeanfrida Mushumbusi akielezea ujumuishwaji wa jinsi unavyotumika katika Idara hiyo wakati wa semina elekezi ya Mwongozo wa Jinsia katika Utumishi wa Umma. 

Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Huduma za Tehama Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Tiba Manoni akielezea namna ujumuishwaji wa jinsia katika Utumishi wa Umma unavyotumika katika utendaji kazi wa Idara hiyo.


Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Maafisa Waandamizi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Jafari Maganga akielezea majukumu ya Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo wakati wa semina elekezi ya Mwongozo wa Jinsia katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.