Friday, June 28, 2024

OFISI YA RAIS, UTUMISHI NA UTAWALA BORA YAWAASA WATUMISHI WA UMMA KUACHA KUCHEZA KAMALI


Na. Lusungu Helela - Dodoma

Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imesema sio maadili kwa Watumishi wa Umma kucheza kamali ikwemo michezo wa kubashiri (betting) kwani inatweza utumishi wao katika jamii.

Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa Juni 28, 2024 katika Ofisi ya Mtumba jijini Dodoma na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamzi wa Maadili, Bw. Ally Ngowo wakati wa utoaji wa Semina ya kuwajengea uwezo Watumishi wa Ofisi hiyo mahali pa kazi

Amesema Mtumishi wa Umma ni kioo katika jamii hivyo kujihusisha kucheza kamali kunapelekea Mtumishi kushindwa kuwahudumia wananchi na wakati mwingine kupata msongo wa mawazo endapo atapoteza fedha kwenye kamari

Katika hatua nyingine, Bw. Ngowo amesema sio maadili kwa Watumishi wa Umma kukopa fedha bila mpangilio.

Amefafanua kuwa baadhi ya watumishi wamekuwa wakikopa pasipokuwa na malengo, hivyo wakijikuta na madeni mengi yasiyokuwa na ulazima, hali inayowafanya kushindwa kufanya kazi zao ipasavyo.

Kwa upande wake Mtaalamu wa Saikolojia, Dkt. Chris Mauki amesema katika maisha ya kila siku mabadiliko hayaepukiki na kama hawatayakubali mabadiliko hayo ni lazima watumishi wapate changamoto ya afya ya akili.

"Miili yetu haijaumbwa kupokea mabadiliko yanayotokea katika maeneo yetu ya kazi na maisha kwa ujumla na hivyo tumejikuta tukipata changamoto ya afya ya akili " amesema Dkt. Chris Mauki

Amesema kiasili binadamu wote ni woga wa mabadiliko na hiyo imepelekea binadamu kupambana na mabadiliko yasitokee hali inayopelekea kujikuta kwenye msongo wa mawazo na muda mwingine kupata matatizo makubwa.

Awali Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi amesema mafunzo hayo yameletwa kwa vile Watumishi wa Ofisi hiyo wana kazi nyingi ambazo zimekuwa zikiwaletea msongo wa Mawazo hivyo mafunzo ni muhimu ili waweze kuwa wastahimilivu.

‘’Hapa kuna msongo wa mawazo sana hivyo mafunzo haya ya afya ya akili ni muhimu ili kuweza kuepukana nayo’’ amesisitiza Kaimu Katibu  Mkuu, SACP. Ibrahim Mahumi

Naye Daktari Bingwa wa Macho, Joshua Yeuze kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa akiwasilisha mada kuhusu Magonjwa Sugu yasiyoambukiza (Sukari na Presha ya Macho) akitoa semina ya magonjwa hayo amewaasa Watumishi wa Umma kujenga utamaduni wa kupima angalau kwa mwaka mara moja ili kujua hali za afya zao

‘’Hakikisheni mnafanya mazoezi mara kwa mara pamoja na kula chakula bora ili kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza’’ amesema Dkt. Yeuze

Katika hatua nyingine Mchunguzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Stephew Agwanda wakati akiwasilisha mada kuhusu Mkakati wa Taifa dhidi ya Rushwa amewaasa Watumishi hao kujiepusha vitendo vya rushwa mahali pa kazi


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi akizungumza na watumishi wa ofisi hiyo (hawapo pichani) wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo watumishi mahali pa kazi iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo watumishi mahali pa kazi iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.

Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Dkt. Chris Mauki wakati akiwasilisha mada ya Mabadiliko ikiwemo kipengele cha afya ya akili kwenye semina ya kuwajengea uwezo watumishi mahali pa kazi iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Dkt. Joshua Yeuze wakati akiwasilisha mada kuhusu Magonjwa Sugu yasiyoambukiza (Sukari na Presha ya Macho) kwenye semina ya kuwajengea uwezo watumishi mahali pa kazi iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Mtaalam wa Saikolojia, Dkt. Chris Mauki akiwasilisha mada ya mabadiliko kwenye kipengele cha afya ya akili kwenye semina ya kuwajengea uwezo mahali pa kazi watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Daktari Bingwa wa Macho, Joshua Yeuze kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa akiwasilisha mada kuhusu Magonjwa Sugu yasiyoambukiza (Sukari na Presha ya Macho) wakati wa semina ya kuwajengea uwezo mahali pa kazi watumishi wa ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Dkt. Joshua Yeuze wakati akiwasilisha mada kuhusu Magonjwa Sugu yasiyoambukiza (Sukari na Presha ya Macho) kwenye semina ya kuwajengea uwezo watumishi mahali pa kazi iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais - UTUMISHI, Bw. Ally Ngowo alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Maadili katika Utumishi wa Umma wakati wa semina ya kuwajengea uwezo watumishi mahali pa kazi iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Usimamizi wa Maadili Ofisi ya Rais - UTUMISHI, Bw. Ally Ngowo akiwasilisha mada kuhusu Maadili katika Utumishi wa Umma wakati wa semina ya kuwajengea uwezo mahali pa kazi watumishi wa ofisi hiyo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Mchunguzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Stephew Agwanda (hayupo pichani) alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Mkakati wa Taifa dhidi ya Rushwa wakati wa semina ya kuwajengea uwezo watumishi mahali pa kazi iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Mchunguzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Stephew Agwanda akiwasilisha mada kuhusu Mkakati wa Taifa dhidi ya Rushwa kwenye semina ya kuwajengea uwezo mahali pa kazi watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Mchunguzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Stephew Agwanda (hayupo pichani) alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Mkakati wa Taifa dhidi ya Rushwa wakati wa semina ya kuwajengea uwezo watumishi mahali pa kazi iliyofanyika katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.

 



 

 


Wednesday, June 26, 2024

TANZANIA YANG’ARA TUZO ZA KIMATAIFA ZA UBUNIFU WA MFUMO WA KIDIJITALI WA eMREJESHO

 Na. Mwandishi wetu- Korea Kusini

Tanzania imeng'ara katika tuzo za Kimataifa za ubunifu wa mfumo ya kidijitali wa Mrejeshoi (e-Mrejesho) uliosaidia kuleta mageuzi makubwa katika  uboreshaji wa utoaji wa  huduma kwa wananchi.

Tuzo hizo zimetolewa jana nchini Korea Kusini na Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) wakati wa Mkutano wa Umoja wa Jukwaa la Umoja wa Mataifa la Tuzo za Utumishi wa Umma (2024 UN Public Service Awards (UNPSF).

Tuzo hiyo iliyopokelewa na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora, Bw.  Xavier Daudi ambapo nchi 15 kati ya 72 zimetunukiwa tuzo hizo huku kwa upande wa Afrika, Tanzania na Afrika ya Kusini ndizo zilizotambuliwa katika tuzo hizo.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Naibu Katibu Mkuu, Bw. Daudi amesema Tanzania imepokea tuzo kwenye kipengele cha ubunifu kwenye Taasisi za Umma (Honorable Mention Innovation in Public Institution).

‘‘Tuzo tuliyoipokea ni heshima kubwa na pia ni fahari kwa vijana wetu wazawa waliobuni mfumo huo ambao wananchi wana uwezo wa kuiambia Serikali yao kwamba utumishi wa umma una uimara na ulegevu katika utoaji huduma’’ amesema.

Katika mkutano huo ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi pamoja na Wakurugenzi kutoka Ofisi hiyo akiwemo Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maadili Bi. Leila Mavika, Mkurugenzi wa Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Serikalini, Bw. Priscus Kiwango pamoja na Mkurugenzi, Mhandisi Rico Bomani na Meneja wa Mafunzo na Ubunifu, Mhandisi Jaha Mvula kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA).

Aidha Mhe. Balozi Togolani Edris Mavura, Balozi wa Tanzania nchini Korea ya Kusini aliambatana na ujumbe huo katika kupokea tuzo.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora, Bw.  Xavier Daudi ( wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi alioongozana nao nchini Korea Kusini wakifurahia mara baada ya kupokea  tuzo za Kimataifa za ubunifu wa mfumo ya kidijitali wa Mrejeshoi (e-Mrejesho) ambayo Tanzania imekabidhiwa na  Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) wakati wa Mkutano wa Umoja wa Jukwaa la Umoja wa Mataifa la Tuzo za Utumishi wa Umma (2024 UN Public Service Awards (UNPSF) Wa pili kushoto ni Balozi wa  Tanzania nchini Korea ya Kusini, Mhe. Balozi Togolani Mavura.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora, Bw.  Xavier Daudi (wa tatu kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi alioongozana nao nchini Korea Kusini wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kupokea tuzo za Kimataifa za ubunifu wa mfumo ya kidijitali wa Mrejesho (e-Mrejesho) ambapo  Mkurugenzi wa Idara ya Maadili, Bi. Leila Mavika (wa tatu kushoto) akiwa ameshika tuzo hiyo ambayo Tanzania imekabidhiwa na  Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) wakati wa Mkutano wa Umoja wa Jukwaa la Umoja wa Mataifa la Tuzo za Utumishi wa Umma ( 2024 UN Public Service Awards (UNPSF) Wa nne kulia ni Balozi wa  Tanzania nchini Korea ya Kusini, Mhe. Balozi Togolani Mavura.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora,  Bw.  Xavier Daudi (wa tatu kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi alioongozana nao nchini Korea Kusini wakiwa kwenye picha ya pamoja  mara baada ya kupokea  tuzo za Kimataifa za ubunifu wa mfumo ya kidijitali wa Mrejesho (e-Mrejesho) ambapo  Mkurugenzi wa Idara ya Maadili, Bi. Leila Mavika (katikati) akiwa ameshika tuzo hiyo ambayo Tanzania imekabidhiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) wakati wa Mkutano wa Umoja wa Jukwaa la Umoja wa Mataifa la Tuzo za Utumishi wa Umma (2024 UN Public Service Awards (UNPSF) Wa tatu kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Korea ya Kusini, Mhe. Balozi Togolani Mavura.

 



 

Saturday, June 22, 2024

WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA ATAKA MPANGO MKAKATI WA MATUMIZI WA MIFUMO YA KIDIGITALI KATIKA UTUMISHI WA UMMA

 Na. Lusungu Helela- Dodoma  

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amezitaka Taasisi za Umma kuweka mipango madhubuti ya kutumia mifumo ya kidijitali ambayo italeta mageuzi ya kiutendaji na kuifanya Tanzania kuendana na mapinduzi ya nne ya viwanda yanayotumia TEHAMA.

Ametoa kauli hiyo leo Jumapili, Juni 23 , 2024 jijni Dodoma katika viwanja vya Chinangali Park wakati akimwakilisha Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali iliyosanifiwa na kujengwa na Ofisi ya Rais-UTUMISHI. 

Amezitaka Taasisi hizo kufuatilia na kuhimiza matumizi ya mifumo hiyo kwa Watumishi wanaowaongoza.

Amesema uzinduzi wa mifumo hiyo ya kidijitali ni utelelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambapo Serikali itaweza kuwahudumia wananchi kwa uwazi na kwa haraka zaidi.

Ameitaja mifumo iliyozinduliwa kuwa ni HR Assesment, PEPMIS na PIPMIS, e-Watumishi (HCMIS) pamoja na e-Mrejesho.

Amesema mifumo hiyo ikitumika ipasavyo itasaidia kuwabaini Watumishi mahiri na watumishi wazembe pamoja na kuongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika utumishi wa umma.

"Mifumo hii ikitumiwa kama ilivyokusudiwa itasaidia kuwabana Watumishi wazembe na hivyo kuongeza uwazi uwajibikaji na ufanisi katika kuwahudumia wananchi " amesisitiza Mhe.Majaliwa

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amewapongeza vijana wazawa kwa ubunifu wa kusanifu mifumo hiyo huku akiutaja mfumo wa e-Mrejesho uliotambulika kimataifa kutokana na ubora wake.

Akizungumzia Wiki ya Utumishi wa Umma amesema moja ya lengo lake ni kuhimiza uwajibikaji, uwazi, uadilifu pamoja na utoaji huduma bora kwa wananchi

"Hongereni sana Taasisi za Umma kwa utayari wenu wa kutoa huduma kwa wananchi kuanzia Juni 16 hadi leo hii siku ya Kilele" amesisiiza Waziri Mkuu.

Amesema kitendo cha kufanyika kwa maonesho hayo ni dalili tosha kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imejizatiti kutoa huduma bora za papo kwa hapo kwa wananchi pasipo wananchi  kulazimika kuzifuata huduma hizo maofisini.

Kwa upade wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ys Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amesema matumizi ya  TEHAMA  katika Utumishi wa Umma yameondoa usumbufu, rushwa pamoja  na kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi.

Amesema mifumo hiyo imesanifiwa na kujengwa na wazawa ukiwemo mfumo wa e-Watumishi (HCMIS) ambao una uwezo wa kuhifadhi taarifa za watumishi wa umma kuanzia siku aliyoajiriwa hadi siku ya kustaafu.

Amesema mfumo wa upimaji wa utendaji kazi kwa watumishi na taasisi PEPMIS na PIPMS umesaidia kuondoa upendeleo na uonevu na unahamasisha utendaji kazi miongoni mwa watumishi.

Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, UTUMISHI, Bw.J uma Mkomi amesema matumizi wa Mifumo ya Utendaji Kazi ikiwemo PEPMIS na PIPMIS imeonekana kuwa   ni kikwazo kwa baadhi ya Watumishi kwa sababu Watumishi wengi hawapendi kubanwa

Bw. Mkomi amesema mtumishi yeyote ambaye hatojaza majukumu yake kwenye mfumo huo   hatopata ruhusa ya kuhama wala kwenda masomoni pamoja na kutopanda cheo

Katika hatua nyingine Bw. Mkomi amesema Mfumo wa e-mkopo umewarahisishia Watumishi wa Umma kupata mkopo kwa haraka na pia mfumo huo hautoi  fursa kwa Watumishi  kukopa benki nyingine  endapo Mtumishi atakuwa na mkopo katika benki nyingine.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Katiba, Sheria na Utawala Bora, Mhe. Frolent Kyombo ameipongeza Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa usanifu na kujenga mifumo hiyo ya Kidijitali kwani imesaidia kupunguza usumbufu na gharama kwa watumishi wa Umma wa kufuatilia huduma Dodoma.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu Mifumo ya Utendaji Kazi katika  Utumishi wa Umma kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Sera za Tehama na Viwango, Bw. Ibrahim Toure wakati  alipotembelea banda la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na  Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.  


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi mbalimbali wa Serikali pamoja na wananchi walioshiriki kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali yaliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma. 

Sehemu ya watumishi mbalimbali wa Serikali pamoja na wananchi walioshiriki kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali wakimsikiliza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa yaliyofanyika kitaifa  katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa kuzungumza na Wananchi na Watumishi mbalimbali walioshiriki kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali yaliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.  


Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akitoa utambulisho wa Viongozi waliohudhuria kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.  


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akitazama Nyaraka za Kiutumishi wakati alipotembelea banda Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na  Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.  


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mhifadhi Mkuu wa Malikale Bw. William Mwita wakati alipotembelea banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na  Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali  iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.  


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akipiga makofi mara baada ya kuzindua Mifumo ya Utendaji Kazi Serikalini wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na  Uzinduzi wa mifumo ya  kidijitali  iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.  Wengine ni Viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watendaji wengine wa Serikali.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akimkabidhi Tuzo ya Usanifu na Ujenzi wa Mifumo ya Kielektroni katika Utumishi wa Umma Bw. Ibrahim Mrisha wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na  Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.  


Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma wakimsikiliza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali  iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.  


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Mussa Magufuli akizungumza jambo na Wakurugenzi wasaidizi wa Ofisi hiyo wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.   Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mikataba ya Utendaji Kazi Serikalini, Bi. Zainabu Kutengeza.


Kwaya ya TAKUKURU ikitumbuiza wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Uzinduzi wa mifumo ya kidijitali iliyofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.  




KATIBU MKUU MKOMI AFURAHISHWA NA TAASISI KUJITOKEZA KWA WINGI KUTOA HUDUMA KWENYE WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

 Na. Veronica Mwafisi- Dodoma  

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amefurahishwa na Taasisi za Umma kujitokeza kwa wingi kushiriki na kutoa huduma za Kiserikali papo kwa hapo kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma huku akitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kutembelea Maonesho hayo.

Bw. Mkomi ameyasema hayo wakati alipotembelea mabanda na kujionea huduma zikitolewa na Wizara na Taasisi mbalimbali zilizoshiriki kwenye maonesho hayo yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Maonesho hayo yaliyoanza Juni 16 yanatarajiwa kuhitimishwa siku ya kesho Juni 23, ambapo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi.

Maadhimisho na Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kitaifa yameratibiwa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambapo Kaulimbiu ya Mwaka huu ni “Kuwezesha kwa Utumishi wa Umma uliojikita kwa Umma wa Afrika ya Karne ya 21 iliyojumuishi na inayostawi; Ni Safari ya Mafunzo na Mabadiliko ya Kiteknolojia”.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akipata maelezo kuhusu kitabu kilichokuwa kinatumika na Serikali ya Kikoloni (Mwingereza) wakati alipotembelea katika banda la Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yanafanyika jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akifurahia jambo na watumishi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) alipotembelea Viwanja vya Chinangali kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yanafanyika jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akizungumza na mtumishi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) alipotembelea Viwanja vya Chinangali kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yanafanyika jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza na watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii alipotembelea Viwanja vya Chinangali kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yanafanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akisisitiza jambo kwa watumishi wa Tume ya Utumishi wa Umma alipotembelea Viwanja vya Chinangali kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yanafanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Mary Mwakapenda mara baada ya Katibu Mkuu huyo kuwasili katika Viwanja vya Chinangali Park kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika Jijini Dodoma.