Thursday, November 2, 2023

MHE. DKT. MHAGAMA ASISITIZA UHIFADHI SALAMA WA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA TAIFA

 Na. Rainer Budodi- Dodoma

Tarehe 2 Novemba, 2023

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama ameitaka Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa kuongeza jitihada zaidi katika kutafuta kumbukumbu na nyaraka kutoka taasisi mbalimbali za umma na kuzihifadhi mahali salama na katika ubora unaotakiwa kwa manufaa ya vizazi vilivyopo na vijavyo.

Dkt. Mhagama amesema hayo leo Novemba 2, 2023 jijini Dodoma wakati wa ziara ya Kamati hiyo katika Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa kuona namna Idara hiyo inavyotunza kumbukumbu na nyaraka za Taifa.

Aidha, kwa niaba ya Kamati, Dkt. Mhagama ameipongeza Idara hiyo kwa kufanya kazi kubwa ya kuhifadhi Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa ikiwa ni pamoja na historia ya mambo muhimu ya kitaifa na kimataifa kwa kuzingatia misingi na maadili ya utumishi wa umma.

“Sisi kama Kamati tumeona na kushuhudia miundombinu mizuri na matumizi bora ya TEHAMA katika uhifadhi wa kumbukumbu na nyaraka hizi, hongereni sana na kwa mantiki hii tunajivunia kuwa na hazina kubwa ya taarifa” alisema Dkt. Mhagama.

Vilevile Dkt. Mhagama amemsisitiza Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kuhakikisha ofisi yake inaisimamia vyema Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa katika zoezi la kuhifadhi nyaraka ambazo zimekusanywa hivi karibuni ili ziwe kwenye utaratibu mzuri kama zilivyo nyingine kwa lengo la kuepuka upotevu wowote wa nyaraka hizo.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameishukuru Kamati hiyo ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kupanga ziara hiyo muhimu na kutoa maelekezo ambayo yatafanyiwa kazi kwa haraka na kutoa mrejesho.

“Ujio wenu hapa umeambatana na maelekezo muhimu sana kwetu ili kuimarisha shughuli zinazofanywa na Idara hii kwa ustawi wa Serikali na Taifa kwa jumla, nasi tuko tayari kutekeleza maelekezo hayo kwa haraka na ufanisi” alisema Mhe. Kikwete.

Mhe. Kikwete ameongeza kuwa ofisi yake itasimamia na kutekeleza maelekezo hayo kwa kuwa tayari Serikali imeshatoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali katika Idara hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akizungumza na sehemu ya Viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watendaji wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa wakati wa ziara ya kamati hiyo katika Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia wasilisho la taarifa ya utendaji kazi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa wakati wa ziara ya kikazi katika Ofisi hiyo jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa neno la shukrani kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa ziara ya kamati hiyo katika Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.



Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na Viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakielekea katika ghala la utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kikazi katika Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.    


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na Viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia maelezo ya Mtunza Kumbukumbu Msaidizi Bi. Rehema Mwiga (Wa kwanza kulia) kuhusu nyaraka mbalimbali zinazotunzwa katika ghala hilo wakati wa ziara ya kikazi ya kamati hiyo ilipotembelea Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.  


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa ziara ya kikazi ya kamati hiyo ilipotembelea Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi akiwaonesha wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria moja ya nyaraka zilizopo katika ofisi yake wakati wa ziara ya kikazi ya kamati hiyo jijini Dodoma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakitazama moja ya nyaraka zilizopo katika Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa wakati wa ziara ya kikazi ya kamati hiyo jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiteta jambo na Kaimu Katibu Mkuu, Bw. Xavier Daudi wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria katika Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watendaji wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa wakati ziara ya kikazi katika Idara hiyo jijini Dodoma.


 



No comments:

Post a Comment