Sunday, March 15, 2020

RUZUKU YA TASAF YAMUWEZESHA ALBINA KUENDESHA MRADI WA KOKOTO NA KUBORESHA MAISHA YAKE MJINI BABATI

Mnufaika wa Ruzuku inayotolewa na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF), Bibi Albina Matayo, mkazi wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Mtaa wa Mrara, akitoa ushuhuda jana kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wa namna TASAF ilivyomuwezesha kuboresha maisha yake.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. Dkt. Jasson Rweikiza (Mb), akieleza kuridhishwa na maendeleo ya Mnufaika wa (TASAF), Bibi Albina Matayo, mkazi wa Halmashauri ya Mji wa Babati.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George Mkuchika (Mb) akishuhudia kokoto zilizopondwa kwa ajili ya kuuzwa na Bibi Albina Matayo ambaye ni Mnufaika wa Ruzuku inayotolewa na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF), Halmashauri ya Mji wa Babati.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George Mkuchika (Mb) akiwa katika picha na mnufaika wa TASAF, Halmashauri ya Mji wa Babati, Bibi Albina Matayo mbele ya nyumba iliyojengwa na mnufaika huyo kupitia Ruzuku inayotolewa na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF).

Mbuzi wanaofugwa na Bibi Albina Matayo, mkazi wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Mtaa wa Mrara ambaye ni mnufaika wa Ruzuku inayotolewa na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF), ambayo imemuwezesha kuwanunua mbuzi hao.


No comments:

Post a Comment