Saturday, November 9, 2019

TAASISI YA UONGOZI YATAKIWA KUTOA MAFUNZO KWA VIONGOZI KATIKA MAENEO YAO YA KAZI ILI KUIMARISHA UTAWALA BORA



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akihimiza uwajibikaji kwa watumishi wa Taasisi ya Uongozi (UONGOZI Institute) ( hawapo pichani) wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo jijini Dar es Salaam jana.

Baadhi ya watumishi wa Taasisi ya Uongozi (UONGOZI Institute) wakisikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakati wa kikao kazi cha watumishi hao na Naibu waziri huyo chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kilichofanyika katika ukumbi wa Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Taasisi ya Uongozi (UONGOZI Institute) mara baada ya kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo jijini Dar es Salaam jana.



Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Prof. Joseph Semboja akimkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) mara baada ya Naibu Waziri huyo kuwasili katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kikao kazi cha kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa taasisi hiyo.

No comments:

Post a Comment