Wednesday, May 19, 2021
MHE. MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA WA TAKUKURU KUTUNZA SIRI ZA WANAOTOA TAARIFA ZA VITENDO VYA RUSHWA
Na. James K.
Mwanamyoto-Dar es Salaam
Tarehe 19 Mei, 2021
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) kutotoa siri za wananchi wanaowasilisha taarifa za uwepo wa vitendo vya rushwa kwenye taasisi hiyo ili ziweze kufanyiwa kazi.
Akizungumza wakati wa kikao
kazi chake na Viongozi wa TAKUKURU leo jijini Dar es Salaam, Mhe. Mchengerwa
amemuelekeza Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Kamishna wa Polisi (CP) Salum Hamduni
kuhakikisha vyanzo vya taarifa za rushwa vinalindwa ili kuhamashisha wananchi
kuendelea kutoa taarifa zitakazoiwezesha Serikali kulinda rasilimali za taifa.
Mhe. Mchengerwa amehimiza
uadilifu kwa Watumishi wa TAKUKURU hususan kwenye eneo la utunzaji siri za
watoa taarifa ili kuwajengea wananchi imani ya kuendelea kushirikiana na
TAKUKURU katika mapambano dhidi ya rushwa.
“Utoaji wa siri za
wanaowasilisha taarifa za vitendo vya rushwa, unahatarisha usalama wao, hivyo
Mkurugenzi Mkuu uanze na suala hili ili tubaini watumishi wote wanaotoa siri za
watoa taarifa na kuwachukulia hatua za kinidhamu.” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.
Mhe. Mchengerwa amewaasa
watumishi hao kutenda haki wanaposhughulikia vitendo vya rushwa ili kutoitia
dosari Ofisi hiyo inayoaminiwa na wananchi.
Kuhusu utekelezaji wa
maelekezo ya Mhe. Rais juu ya taasisi hiyo kujikita moja kwa moja katika
majukumu yake, Mhe. Mchengerwa amewakumbusha Viongozi hao kutekeleza maelekezo hayo
ipasavyo kwa kushughulikia masuala yanayohusiana na rushwa, ubadhirifu wa mali
za umma na uhujumu uchumi na si vinginevyo.
Aidha, Mhe. Mchengerwa amesema,
Serikali ina imani na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU CP Salum Hamduni na Naibu
wake Bi. Neema Mwakalyelye walioapishwa leo na Mhe. Rais, na ndio maana
wamepewa dhamana ya kuiongoza taasisi hiyo nyeti.
Akizungumza na viongozi wa TAKUKURU kabla ya kumkaribisha Mhe. Mchengerwa, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi amewahimiza watendaji wa TAKUKURU kutofanya kazi zisizoihusu TAKUKURU kama ambavyo Mhe. Rais na Waziri Mchengerwa wamekuwa wasisitiza.
Mhe. Ndejembi ameitaka
TAKUKURU kuhakikisha inayakamilisha kwa wakati mashauri ya msingi yanayoihusu taasisi
hiyo na kwa yale yasiyokuwa na msingi yafutwe ili kutoa fursa kwa taasisi hiyo kuendelea
kutekeleza majukumu yenye tija kwa taifa.
Kwa upande wake. Mkurugenzi wa
TAKUKURU, CP Salum Hamduni amekiri kupokea maelekezo ya Mhe. Waziri na kuahidi
kuyafanyia kazi ndani ya muda aliolekeza.
Ili kutekeleza maelekezo ya
Mhe. Mchengerwa kwa wakati, CP Hamduni amewataka watumishi wake kujitoa
kikamilifu katika utekelezaji wa majukumu ya TAKUKURU ili kufikia malengo ya
taasisi hiyo.
Mhe. Mchengerwa amefanya kikao
kazi na Viongozi wa TAKUKURU mara baada ya Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo na
Naibu wake kuapishwa na Mhe. Rais-Ikulu Jijini Dar es Salaam lengo likiwa ni kuhimiza
uwajibikaji na utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais aliyedhamiria taasisi hiyo
kutekeleza majukumu yake kwa weledi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akikaribishwa na
Watumishi wa TAKUKURU leo Jijini Dar es Salaam alipowasili kwa ajili ya kikao
kazi chake na Viongozi wa TAKUKURU kilicholenga kuhimiza uwajibikaji.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akisalimiana na
Watumishi wa TAKUKURU leo Jijini Dar es Salaam alipowasili kwa ajili ya kikao
kazi chake na Viongozi wa TAKUKURU kilicholenga kuhimiza uwajibikaji. Kulia
kwake Naibu Waziri wake, Mhe. Deogratius Ndejembi na Viongozi Wakuu wa TAKUKURU
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Mohamed Mchengerwa akizungumza na Viongozi wa TAKUKURU leo Jijini Dar es Salaam
wakati wa kikao kazi chake na Viongozi hao chenye lengo la kuhimiza
uwajibikaji. Kulia kwake ni Naibu Waziri wake, Mhe. Deogratius Ndejembi na
kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, CP Salum Hamduni.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiwa katika kikao
kazi na Viongozi wa TAKUKURU leo Jijini Dar es Salaam chenye lengo la kuhimiza
uwajibikaji.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza kabla
ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa kuzungumza na Viongozi wa TAKUKURU leo
Jijini Dar es Salaam wakati wa kikao kazi chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, CP Salum
Hamduni akiahidi kutekeleza maelekezo aliyopewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa
wakati wa kikao kazi cha Waziri huyo na Viongozi wa TAKUKURU leo Jijini Dar es
Salaam chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akionyesha nembo
ya TAKUKURU aliyokabidhiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, CP Salum Hamduni baada
ya kikao kazi cha Waziri huyo na Viongozi wa TAKUKURU leo Jijini Dar es Salaam
chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiwa katika picha
ya pamoja na Viongozi wa TAKUKURU mara baada ya kikao kazi cha Waziri huyo na
Viongozi hao wa TAKUKURU leo Jijini Dar es Salaam chenye lengo la kuhimiza
uwajibikaji. Kulia kwake ni Naibu Waziri wake, Mhe. Deogratius Ndejembi na
kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, CP Salum Hamduni.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiagana na
Viongozi Wakuu wa TAKUKURU mara baada ya kikao kazi cha Waziri huyo na Viongozi
hao wa TAKUKURU leo Jijini Dar es Salaam chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Wednesday, May 12, 2021
MHE. MCHENGERWA AZITAKA TAASISI ZA KIFEDHA KUTOA MIKOPO KUPITIA HATIMILIKI ZINAZOTOLEWA NA MKURABITA
Na. James K.
Mwanamyoto-Zanzibar
Tarehe 12 Mei, 2021
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amezitaka taasisi za kifedha nchini kutoa mikopo kwa wananchi wenye hatimiliki za kimila zinazotolewa na Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) ili kuwawezesha wananchi hao kuendesha shughuli zao na kuinua kipato.
Akikabidhi
hatimiliki hizo kwa baadhi ya wananchi wa Shehia ya Welezo, Zanzibar, Mhe.
Mchengerwa amesema, hatimiliki hizo zinalenga kutoa fursa kwa wananchi kupata
mikopo itayowawezesha kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo na biashara
ili kuboresha maisha yao.
“Taasisi
za kifedha zitambue hatimiliki hizi na kupunguza masharti ili kuwawezesha wafanyabiashara
wadogo kukopa na kuongeza mtaji.” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.
Akiwa katika kituo Jumuishi
cha Urasimishaji na Uendelezaji Biashara kilichoko katika Baraza la Biashara,
eneo la Darajani Wilaya ya Mjini, Mhe. Mchengerwa amezitaka pia taasisi za
kifedha kutoa mikopo kwa wajasiriamali waliorasimisha biashara zao na kuongeza
kuwa, mikopo hiyo itawaongezea mitaji ya kuendesha shughuli zao za ujasiriamali.
Kutokana na uwepo wa kituo
hicho, Mhe. Mchengerwa amehimiza zoezi la urasimishaji biashara lisichukue muda
mrefu ili kutoa hamasa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kurasimisha biashara
zao.
Akieleza mchango wa ofisi yake
katika zoezi la urasimishaji biashara, Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na
Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum amesema kituo hicho
kimejengwa ili kuondoa changamoto za urasimishaji walizokuwa wakikutana nazo wafanyabiashara
wadogo.
Dkt. Salum ameongeza kuwa
kutokana na faida za uwepo wa kituo hiki, Serikali imedhamiria kujenga kituo
kama hiki Pemba ili wananchi wa eneo hilo nao waweze kunufaika.
Naye Mratibu wa Mkurabita,
Dkt. Seraphia Mgembe amesema utekelezaji wa MKURABITA Zanzibar umewanufaisha
wananchi wa Zanzibar kwa kuwapatia mafunzo ya utunzaji wa kumbukumbu za
biashara ambapo hivi sasa wanazo takwimu sahihi za maendeleo ya biashara zao.
Mhe. Mchengerwa amehitimisha
ziara yake ya kikazi Zanzibar ya kukagua miradi inayotekelezwa na taasisi
zilizo chini ya ofisi yake ikiwa ni pamoja na kuhimiza uwajibikaji kwa
watumishi wa Sekretarieti ya Ajira ofisi ya Zanzibar.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Mohamed Mchengerwa akizungumza na wananchi wa Shehia ya Welezo wakati wa ziara
yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya MKURABITA, Zanzibar.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Mohamed Mchengerwa akitoa hatimiliki kwa mmoja wa wananchi wa Shehia ya Welezo
wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya MKURABITA,
Zanzibar.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Mohamed Mchengerwa akizungumza na wajasiriamali (hawapo pichani) wanaopata
huduma katika kituo Jumuishi cha
Urasimishaji na Uendelezaji Biashara kilichoko katika Baraza la Biashara, eneo
la Darajani Wilaya ya Mjini wakati wa ziara yake ya
kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya MKURABITA, Zanzibar. Kulia kwake ni Katibu
Mkuu, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar, Dkt. Islam Seif
Salum.
Baadhi
ya Wajasiriamali wa Zanzibar waliorasimisha biashara zao kupitia kituo Jumuishi cha Urasimishaji na Uendelezaji Biashara
kilichoko katika Baraza la Biashara, eneo la Darajani Wilaya ya Mjini
wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara
ya kikazi ya Waziri huyo Zanzibar.
Mratibu
wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania
(MKURABITA), Dkt. Seraphia Mgembe akitoa taarifa ya utekelezaji ya kituo Jumuishi cha Urasimishaji na Uendelezaji Biashara
kilichoko katika Baraza la Biashara eneo la Darajani Wilaya ya Mjini, wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ya kukagua
utekelezaji wa miradi ya MKURABITA, Zanzibar.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Mohamed Mchengerwa akihimiza zoezi la urasimishaji wa biashara kufanyika kwa
wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi katika kituo Jumuishi cha Urasimishaji na Uendelezaji Biashara
kilichoko katika Baraza la Biashara, eneo la Darajani Wilaya ya Mjini.
Wanaomsikiliza ni Watendaji wa Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda
Zanzibar na Mratibu wa MKURABITA, Dkt. Seraphia Mgembe.
















