Thursday, June 19, 2014

KONGAMANO LA MIAKA 50 YA MUUNGANO KATIKA UTUMISHI WA UMMA LAFUNGULIWA RASMI LEO

Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI akifungua Kongamano la Miaka 50 ya Muungano katika Utumishi wa Umma 2014 katika Kituo cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere mapema leo.

Sehemu ya Washiriki wa Kongamano la Miaka 50 ya Muungano katika Utumishi wa Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Mstaafu Bi.Ruth H. Mollel mapema leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam

Kaimu Katibu Mkuu Utumishi Bw.HAB Mkwizu akiongea kabla ya ufunguzi rasmi wa Kongamano la Miaka 50 ya Muungano katika Utumishi wa Umma katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere mapema leo. Kongamano hilo ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2014
Sekretarieti ikichukua michango wakati wa Kongamano la Miaka 50 ya Muungano katika Utumishi wa Umma katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerer (JNICC) uliopo jijini Dar es Salaam mapema leo.

Katibu Mkuu mstaafu Bi. Ruth H. Mollel akiwasilisha mada wakati wa Kongamano la Miaka 50 ya Muungano katika Utumishi katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere (JNICC). Anayeonekana kulia ni Kaimu Katibu Mkuu Utumishi Bw.HAB Mkwizu, ambaye ni Mwenyekiti wa Kongamano hilo

Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI (wa tatu kutoka kulia) akiwa na wageni waalikwa wa Kongamano la Miaka 50 ya Muungano katika Utumishi wa Umma.Kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Bw.Phillemon Luhanjo akifuatiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Prof.Sifuni Mchome.Kulia kwa mgeni Rasmi  ni Kaimu Katibu Mkuu Utumishi Bw.HAB Mkwizu.



Mgeni rasmi katika Kongamano la Miaka 50 ya Muungano ,Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bi.Hawa A. Ghasia (Mb) akiongea na vyombo vya habari baada ya ufunguzi katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa washiriki wa Kongamano la Miaka 50 ya Muungan o katika Utumishi wa Umma akihojiwa na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa Kongamano la Miaka 50 ya Muungano katika Utumishi wa Umma kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Tuesday, June 17, 2014

SERIKALI YAAGA WATAALAMU 9 WA KUJITOLEA KUTOKA NCHINI JAPAN

Mwakilishi Mwandamizi kutoka JAICA Bw. Yoichiro Kimataakiwatambulisha Wataalamu tisa wa kujitolea kutoka Japan waliomaliza muda wao wa kutoa huduma nchini baada ya kufanya kazi kwa miaka miwili.Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw.HAB Mkwizu. 

Mmoja kati ya Wataalamu wa kujtolea kutoka Japan Bi. Maiko Shimizu akieleza mafanikio ya kazi alizokua akifanya mkoani Dar es Salaam.

Mmoja kati ya Wataalamu wa kujtolea kutoka Japan Bw.Yoshiharu Kamata akieleza mafanikio ya kazi alizokua akifanya mkoani Mbeya.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw.HAB Mkwizu (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa kujitolea kutoka nchini Japan waliomaliza muda wao wa kufanya kazi nchini.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu akimkabidhi zawadi mmoja wa Wataalamu wa Kujitolea kutoka nchini Japan waliomaliza muda wao hapa nchini Bi.Maiko Shimizu.

Monday, June 16, 2014

MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2014 YAFUNGULIWA RASMI LEO

Mgeni rasmi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais  Utawala Bora  Mhe.George  H. Mkuchika (Mb) akifungua Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam mapema leo.Kushoto kwake ni Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw.HAB Mkwizu.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw.HAB Mkwizu akimkaribisha mgeni rasmi kufungua Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam mapema leo.Kulia kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utawala Bora Mhe.George H. Mkuchika (Mb), Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw.Xavier Daudi na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao Bw. Kuwe Bakari (wa kwanza kulia).

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. HAB Mkwizu (katikati) akifafanua jambo wakati mgeni rasmi Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Utawala Bora Mhe.George Mkuchika(Mb) (kushoto) alipotembelea mabanda ya Taasisi mbalimbali zinazoshiriki maonesho hayo. Kulia ni Mchambuzi wa Mifumo ya Kompyuta Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bi.Ilham Mwinyi.



Wakazi wa jiji la Dar es salaam wakiwa katika banda la  Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma wakipewa maelezo kuhusu majukumu ya Ofisi ya Rais-Utumishi.