Friday, October 4, 2019

WATUMISHI WA UMMA NCHINI WATAKIWA KUTUMIA VIZURI RASILIMALI KATIKA UTENDAJI KAZI WAO


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu (hawapo pichani) wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika Shule ya Sekondari Magu Mkoani  Mwanza. Kulia ni Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma, Balozi Mstaafu Mhe. John Haule, Mhe. Khadija Mbarak na Mhe. Alhaj Yahya Mbila.

Baadhi ya Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika Shule ya Sekondari Magu Mkoani  Mwanza.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Magu kabla ya kikao kazi kati yake na Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Magu.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Magu, Mhe. Dkt. Philemon Sengati wakati wa kikao kazi kati yake na Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Mkoani Mwanza kilichofanyika katika Shule ya Sekondari Magu.

Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma, Balozi Mstaafu Mhe.John Haule, akiwasilisha mada kuhusu majukumu ya Tume ya Utumishi wa Umma, wakati wa kikao kazi kati ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa na Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Mkoani Mwanza  kilichofanyika katika Shule ya Sekondari Magu.

MHE. MKUCHIKA NA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU WARIDHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA KLABU YA KUPINGA RUSHWA YA SHULE YA SEKONDARI MTANGALANGA WILAYANI NEWALA



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Mji Newala waliojitokeza kuulaki Mwenge wa Uhuru mara baada ya ujumbe wa Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2019 kuwasili katika halmashauri hiyo ya mji na kufanikiwa kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa kwa fedha za Serikali.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akishiriki kuupokea Mwenge wa Uhuru ulipowasili katika Halmashauri ya Mji Newala. 

Baadhi ya wananchi wa Halmashauri ya Mji Newala waliojitokeza kuulaki Mwenge wa Uhuru mara baada ya ujumbe wa Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2019 kuwasili katika halmashauri hiyo ya mji na kufanikiwa kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa kwa fedha za Serikali.

Kiongozi wa Kitaifa wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 Bw. Mzee Mkongea Ali akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Mji Newala waliojitokeza kuulaki Mwenge wa Uhuru mara baada ya Mwenge huo kuwasili katika halmashauri hiyo ya mji huo na kufanikiwa kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa kwa fedha za Serikali.

Mwenge wa Uhuru ukiwa mbele ya Zahanati ya Tupendane iliyojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) mara baada ya ujumbe wa Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2019 kuitembelea Halmashauri ya Mji Newala na kukagua ujenzi wa jengo hilo ili kujiridhisha na ubora wa jengo ikiwa ni pamoja na matumizi ya fedha za Serikali zilizotolewa na Serikali kujenga zahanati hiyo.

Thursday, October 3, 2019

WATENDAJI SERIKALINI WATAKIWA KUTENDA HAKI WANAPOWAHUDUMIA WATUMISHI ILI KUPUNGUZA IDADI YA RUFAA NA MALALAMIKO YANAYOWASILISHWA TUME YA UTUMISHI WA UMMA



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na Watendaji wa Mkoa wa Mwanza (hawapo pichani) wakati wa kikao kazi kilichofanyika jijini Mwanza.

Baadhi ya Watendaji kutoka Mkoa wa Mwanza wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza wakati wa kikao kazi kilichofanyika jijini Mwanza.


Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nyakimura Muhoji akijibu hoja wakati wa kikao kazi kati ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb), Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma na Watendaji wa Mkoa wa Mwanza kilichofanyika jijini Mwanza.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (kulia) akiteta jambo na Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma Mhe.John Haule wakati wa kikao kazi kati yake na Watendaji wa Mkoa wa Mwanza kilichofanyika jijini Mwanza. Kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela Bw. Said Raphael Kitinga.