Thursday, September 21, 2023

MHE. SIMBACHAWENE ASISITIZA MATUMIZI YA SERIKALI MTANDAO KWA TAASISI ZA UMMA ILI KUEPUSHA MALALAMIKO YA WANANCHI

Na. Rainer Budodi-Dodoma

Tarehe 21 Septemba, 2023

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amesisitiza matumizi ya Serikali Mtandao katika kudhibiti vitendo vya uvunjifu wa Maadili katika Utumishi wa Umma ambavyo vinaleta malalamiko Serikalini.

Mhe. Simbachawene amesema hayo leo tarehe 21 Septemba, 2023 wakati akifungua kikao kazi cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kilichowashirikisha wadau kutoka Taasisi Simamizi za Maadili ya Utendaji, Taasisi Simamizi za Maadili ya Kitaaluma na watumishi kutoka kwenye Wizara mbalimbali na taasisi za kitaaluma katika ukumbi wa PSSSF-Makole Dodoma.

Ni matarajio yangu kuwa mikakati itakayofikiwa katika kikao hiki itasaidia kuondoa malalamiko kuhusu vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa watumishi na Taasisi za Umma zinazosimamia upatikanaji wa haki” amesisitiza.

Aidha, Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa malalamiko yanayotolewa na wananchi yanapaswa kufanyiwa kazi kwa kutoa elimu kwa wanataaluma na watumishi wa umma wote ili wazingatie Sheria, Kanuni na Taratibu zinazosimamia maadili ya utendaji kazi na miiko ya taaluma zao.

Vilevile, ameelekeza viongozi katika Ofisi yake kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu. Pia, Mamlaka Simamizi za Maadili ya Kitaaluma zinapaswa kusimamia na kuchukua hatua stahiki kwa wakati kwa wale wanaokiuka maadili ya taaluma zao kwa lengo la kuendelea kujenga imani kwa wananchi na kuongeza uwajibikaji na usikivu.

Ofisi yangu itaendelea kushirikiana na Mamlaka Simamizi za Maadili ya Kitaaluma kutoa ushauri wa kitaalamu pale itakapohitajika; kutoa ushauri katika mapitio na maboresho ya Kanuni za Maadili za Kitaaluma; kujenga uelewa kuhusu Maadili ya Utumishi wa Umma; na kushirikiana nanyi katika kuleta mabadiliko ya fikra miongoni mwa watumishi wa umma ambao nao ni wanataaluma katika Taasisi mnazoziwakilisha” amesema.

Naye, Kaimu Katibu Mkuu – UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi amesena lengo la kikao hicho ni kubadilishana uzoefu, kutambua changamoto zilizopo, mafanikio na masuala mapya yanayojitokeza katika utumishi wa umma kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi na kuwahudumia wananchi vizuri zaidi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akifungua kikao kazi leo jijini Dodoma cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kilichowashirikisha wadau kutoka Taasisi Simamizi za Maadili ya Utendaji, Taasisi Simamizi za Maadili ya Kitaaluma na watumishi kutoka kwenye Wizara mbalimbali na taasisi za kitaaluma. 


Sehemu ya washiriki wa kikao kazi cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza alipokuwa akifungua kikao kazi hicho leo jijini Dodoma.


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kufungua kikao kazi leo jijini Dodoma cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora.


Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Leila Mavika akitoa utambulisho wa washiriki wa kikao kazi cha siku mbili cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora kabla ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kufungua kikao kazi hicho.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) alipokuwa akifungua kikao kazi cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora leo jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) alipokuwa akifungua kikao kazi cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora leo jijini Dodoma.


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi na  Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Leila Mavika wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) alipokuwa akifungua kikao kazi cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora leo jijini Dodoma.


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akisisitiza jambo kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kufungua kikao kazi leo jijini Dodoma cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akimkabidhi Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Mwl. Paulina Nkwama Mwongozo wa Kanuni za Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa Umma za mwaka 2023 na Mwongozo wa Kushughulikia Mrejesho wa Wananchi wa mwaka 2023 mara baada ya kufungua kikao kazi cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora leo jijini Dodoma. 


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akiwa na baadhi ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakisubiri kumpokea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ili akifungue kikao kazi cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora leo jijini Dodoma.


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akimpokea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene alipowasili kufungua kikao kazi cha kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya maadili na utawala bora leo katika ukumbi wa PSSSF jijini Dodoma.


 

No comments:

Post a Comment