Thursday, August 31, 2023

JIANDIKISHE SASA


 

MSITUME NYARAKA ‘WHATSAPP’ Ni MARUFUKU


 

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema sheria inayosimamia nyaraka za Serikali inaelekeza kuwa mawasiliano ya Serikali yafanyike kwa njia ya barua na si vinginevyo.

Kufuatia kuwepo kwa sheria hiyo, Naibu Waziri  Kikwete  amewaonya watendaji wa Serikali ambao  wanatumia njia ambazo sio rasmi kutuma nyaraka. 

“Haitokuwa sawa na ni marufuku ya Serikali kuwasilisha au kutumiiana ‘Documents’ za Serikali kupitia njia ya WhatsApps na njia nyingine zisizo rasmi, isipokuwa kwa maelekezo ambayo yatakuwa yametolewa vinginevyo katika mamlaka,” amesema Naibu Waziri Ridhiwani Kikwete.

Ameyasema hayo Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Janejelly Ntate James ambaye amehoji uhalali wa  matumizi ya makundi ya WhatsApp kutumiana nyaraka. 

Aidha, Naibu Waziri Kikwete amelihakikishia Bunge kuwa  Serikali bado inaendelea kutengeneza mifumo mbalimbali ambayo itaileta ufanisi katika utendaji kazi Serikalini.

Tuesday, August 29, 2023

MHE. RIDHIWANI KIKWETE; MAADILI NI MSINGI WA MAGEUZI YA MAENDELEO ENDELEVU

 

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewasisitiza watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi na ubunifu ili tija ya kazi zao iweze kuonekana kupitia huduma bora wanazozitoa kwa wananchi.

“Ninatamani kuona utendaji kazi wenu unazingitia misingi ya maadili ya utendaji katika utumishi wa Umma kwani ndiyo msingi wa mageuzi kuelekea maendeleo endelevu vinginevyo watumishi wazembe na wenye mienendo isiyofaa kimaadili mwisho wao umefika.” alisisitiza Mhe. Ridhiwani.

Aidha, amewakumbusha watumishi hao kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anasisitiza uadilifu kazini na ametoa haki na stahiki mbalimbali kwa watumishi, hivyo, Serikali kupitia Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imekamilisha mapitio, kusanifu na kuanza kujenga mifumo ya utendaji kazi Serikalini ili dhana ya wajibu pia iweze kutekelezeka kwa ufanisi.

Pia, Naibu Waziri huyo amezitaka Mamlaka za Ajira na Nidhamu kuendelea kusimamia haki na stahiki zote za watumishi na kuachana na kasumba ya utendaji wa mazoea. Pia, amesema Mamlaka za Ajira na Nidhamu zirejee Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298 ambayo inaonesha kuwa madaraka kuhusu ajira, kuthibitishwa kazini, mafunzo, kupandishwa cheo, nidhamu hadi hitimisho la kazi kwa mtumishi wa umma yalishagatuliwa na hivyo kushindwa kutekeleza wajibu huo ni kielelezo cha kushindwa kutekeleza majukumu waliyopewa.

Katika hatua nyingine Mhe. Ridhiwani amezitaka Halmashauri nchini kuhakikisha zinaendeleza miradi ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF kwa kuwa ni chaguo na imeridhiwa na wananchi wenyewe katika maeneo yao. Iwapo Halmashauri na TASAF zitaunganisha nguvu ni rahisi kuwakomboa wananchi katika umaskini.

“Ninaelekeza walengwa wote wenye sifa za kunufaika na TASAF wasilipwe fedha nusu nusu kwa kuwa lengo ni kuwatoa katika wimbi la umaskini” alisema Mhe. Ridhiwani.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Kemilembe Lwotta ameomba pongezi zifike kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta watumishi wapya wa kada mbalimbali 228 na wote wameripoti kazini na watumishi 289 walimu na wasio walimu wamepandishwa vyeo na 15 wamebadilishiwa vyeo.

Vilevile, ameongeza kuwa wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi katika vijiji vyote 39 wananufaika vyema na uwepo wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF kwa kiwango kikubwa kwa kuwa kaya masikini zimefikiwa na zinawezeshwa kujikwamua kiuchumi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi Bw. John Mgalula pamoja na shukurani alizotoa kwa Serikali, ameomba Serikali kuendelea kutoa vibali vya ajira ili watumishi waongezeke na utoaji huduma kwa umma uimarike.

Mhe. Ridhiwani amehitimisha ziara yake ya siku moja tarehe 25 Agosti, 2023 katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi na kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Halmashauri  hiyo.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida kwenye kikao kazi ambapo amewataka kufanya kazi kwa weledi na ubunifu  katika kuwahudumia wananchi.

Sehemu ya   Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida wakimsiliza Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati alipofanya ziara mkoani humo kwa lengo la  kuwataka Watumishi hao  kufanya kazi kwa weledi na ubunifu  katika kuwahudumia wananchi.

Mkuu wa wilaya ya Manyoni  Mhe.Kemilembe Lwotta  akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida kwenye kikao kazi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete na Watumishi hao  ambapo amewataka kufanya kazi kwa weledi na ubunifu  katika kuwahudumia wananchi.


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimia na Katibu Tawala wa wilaya ya Manyoni ,Bw. James Mchembe  mara baada ya kuwasili katika Halmashauri  hiyo kwa lengo la kuzungumza na watumishi ambapo amewataka kufanya kazi kwa weledi na ubunifu  katika kuwahudumia wananchi.

 




Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Itigi,Bw. John Mgalula akizungumza kabla ya kumkaribisha  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete kuzungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida kwenye kikao kazi ambapo amewataka Watumishi  kufanya kazi kwa weledi na ubunifu  katika kuwahudumia wananchi.



Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiandika changamoto zinazowakabili   Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida kwenye kikao kazi alichokifanya leo mkoani humo  ambapo amewataka kufanya kazi kwa weledi na ubunifu  katika kuwahudumia wananchi.

 

 

MHE. KIKWETE; MASLAHI KWA WATUMISHI NI KIPAUMBELE KWA AWAMU YA SITA


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesisitiza kuwa maslahi ya watumishi ni kipaumbele katika awamu hii ya Sita ili kuongeza motisha na kuchochea zaidi utendaji kazi na utoaji wa huduma bora kwa umma.

“Kila mara tunaona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitangaza kutoa haki na stahiki mbalimbali kwa watumishi wa umma, hivyo, kila mmoja wetu kwa nafasi yake anatakiwa pia kuwajibika ipasavyo ili kuleta ufanisi zaidi” ameongeza Mhe. Ridhiwani.

Mhe. Ridhiwani amesema na kusisitiza hayo tarehe 26 Agosti, 2023 alipokuwa akizungumza na viongozi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Singida katika ofisi hizo.  Aidha, amewakumbusha watumishi hao kutoka ofisini na kwenda kuwahudumia wananchi na kutatua changamoto zilizo ndani ya uwezo wao.

Katika hatua nyingine Mhe. Ridhiwani ametembelea na kukagua ujenzi wa majengo ya Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Singida awamu ya pili inayohusu majengo ya madarasa na vyoo vya nje na kuelekeza viongozi kuhakikisha miundombinu ya watu wenye ulemavu inazingatiwa katika ujenzi huo.

“Chuo cha Utumishi wa Umma ni muhimu sana kwa kuwa kinaandaa watumishi wa umma bora na ambao ni msingi wa maendeleo ya nchi katika nyanja zote” ameongeza Mhe. Ridhiwani.

Vilevile, akiwa katika ziara ya kutembelea wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF katika Kijiji cha Ughaugha Kata ya Unyamikumbi, Manispaa ya Singida amesema Serikali imetoa zaidi ya bilioni 51 kwa ajili ya kunusuru kaya maskini nchini ili ziweze kuboresha maisha yao mathalani kwa kupata chakula milo 3 kwa siku, kusomesha watoto na kupata huduma za matibabu kwenye vituo vya afya na zahanati.

Naye, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Bw. Stanislaus Choaji amesema wamepokea maelekezo na watahakikisha wanatazama kwa jicho pevu maeneo ya pembezoni katika Mkoa wa Singida kwa kutoa na kupanga watumishi ili kuboresha utoaji wa huduma kwa umma.

Aidha, Bw. Choaji ameongeza kuwa wananchi wa Mkoa wa Singida wananufaika na uwepo wa TASAF kwa kuwa kaya maskini ambazo ni wanufaika wamepata fedha na wanafanya shughuli za kiuchumi ikiwemo kufuga Mbuzi, Kuku na Kondoo kwa ajili ya kujikwamua katika wimbi la umaskini, hivyo salamu za shukurani zimfikie Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ukombozi huo.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha Utumishi wa Umma Dkt. Ernest Mabonesho amesema ujenzi umefikia asilimia 21 na kazi inayoendelea ni ujenzi wa kuta ambapo hadi sasa mradi huo umetoa ajira za vibarua kwa wananchi 96 wanaozunguka eneo la mradi ikiwa wanaume ni 62 na wanawake ni 34.

Mhe. Ridhiwani amehitimisha ziara yake ya siku mbili katika Mkoa wa Singida kwa tarehe 25-26 Agosti, 2023 ambapo alianzia Halmashauri ya Wilaya ya Itigi na kumalizia katika Manispaa ya Singida. Ziara hiyo ililenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi na kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Mkoa huo.

 


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na viongozi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Singida ambapo amesema  kuwa maslahi ya watumishi ni kipaumbele katika awamu hii ya Sita ili kuongeza motisha na kuchochea zaidi utendaji kazi na utoaji wa huduma bora kwa umma.


Sehemu ya  wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF katika Kijiji cha Ughaugha Kata ya Unyamikumbi, Manispaa ya Singida  wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete ambapo amewaeleza kuwa  Serikali imetoa zaidi ya bilioni 51 kwa ajili ya kunusuru kaya hizo

.


 Baadhi ya Wakurugenzi wa Taasisi mbalimbali za mkoa wa Singida pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo wakimsiliza  Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete  wakati alipotembelea na kukagua ujenzi wa majengo ya Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Singida awamu ya pili

 


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akioneshwa ramani ya majengo ya Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Singida awamu ya pili mara baada ya kufika katika eneo hilo  kwa ajili kukagua ujenzi wa chuo hicho unavyoendelea 



Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa  majengo ya Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Singida awamu ya pili mara baada ya kufika katika eneo hilo  

 Muonekano wa baadhi ya majengo ya Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Singida ambayo tayari yameshakamilika



Mnufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF katika Kijiji cha Ughaugha Kata ya Unyamikumbi, Manispaa ya Singida, Mariamu Luguti ambaye amewezeshwa kufuga mbuzi akizungumza mbele ya   Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete ambapo ameishukuru   Serikali kwa kumsaidia kuondokana kwenye lindi la umasikini



 Kaimu Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha Utumishi wa Umma Dkt. Ernest Mabonesho akizungumza mbele ya   Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete ambapo  amesema ujenzi umefikia asilimia 21wa Chuo cha Utumisi wa Umma Kampasi ya Singida

 

 

 

 

 

 

 

Friday, August 25, 2023

MHE. SIMBACHAWENE AWATAKA WANANCHI KUPUUZA TAARIFA ZA UZUSHI KUHUSIANA NA NDEGE YA RAIS Gulf Stream (G550)

 Na. Veronica Mwafisi-Dar es Salaam

Tarehe 25 Agosti, 2023

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amewataka wananchi kupuuza taarifa za uzushi zinazosambazwa na watu wasio wema kuhusiana na ndege ya Rais Gulf Stream (G550) kushikiliwa nchini Dubai.

Mhe. Simbachawene ameyasema hayo leo wakati akizindua Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali katika Kituo cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

“Mtu anaweza kuzusha jambo na likawapotezea muda mwingi wananchi badala ya kufanya mambo ya maendeleo, kwa mfano uzushi kuhusiana na ndege ya Rais Gulf Stream (G550) kuzuiliwa Dubai, nataka niwahakikishie Watanzania kuwa ndege hiyo ipo sehemu husika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal 1 VIP, jijini Dar es Salaam kwenye eneo ambalo Wakala wa Ndege za Serikali wanalitumia na yeyote anayepita barabarani ataiona,” Mhe. Simbachawene amesisitiza.

Mhe. Simbachawene amesema yeye akiwa ndiye Waziri mwenye dhamana ya Utawala Bora ameona aliweke wazi jambo hilo, lililoleta taharuki ili kuwaondoa hofu Watanzania na uvumi huo ulioenea, hivyo lisiwapotezee muda wao na kuwahakikishia wanaovumisha hayo kwa nia ovu wanaweza kwenda kupata uhakika wa uwepo wa ndege hiyo ambapo ameongeza kuwa Viongozi wanasafiri kama kawaida kwa kutumia ndege hiyo.

Aidha, Mhe. Simbachawene ametoa wito kwa Wajumbe wa Bodi hiyo kushirikiana na Menejimenti ya Wakala wa Ndege za Serikali ili kuiwezesha Wakala hiyo kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

 “Ni matarajio yangu kuwa Bodi hii itasimamia vema utendaji wa Wakala hii ili kuleta tija kwa maendeleo ya taifa kama inavyosisitizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan,” Mhe. Simbachawene amesisitiza.

Akitoa neno la shukrani, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi, Idrissa Mshoro amemuahidi Mhe. Simbachawene kuwa, yeye pamoja na Wajumbe wa Bodi hiyo kwa kushirikiana na Menejimenti ya TGFA watatekeleza yote ambayo ameyaelekeza kwani wanafahamu kwa kina maono makubwa ya Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika katika kuharakisha maendeleo ya nchi katika kuhakikisha uwepo wa usafiri madhubuti. 

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) Capt. Budodi Budodi amesema Menejimenti ya Wakala inamhakikishia Mhe. Simbachawene kuwa wataendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu pamoja na maelekezo ya Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali ili kufikia malengo ya uanzishwaji wa Wakala hiyo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali kabla ya kuzindua bodi hiyo jijini Dar es Salaam. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisisitiza jambo kwa Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa bodi hiyo jijini Dar es Salaam. 


Sehemu ya Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa bodi hiyo jijini Dar es Salaam. 


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu, Bw. Mululi Mahendeka akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzindua Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali jijini Dar es Salaam. 


Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi, Idrissa Mshoro akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene mara baada ya Waziri Simbachawene kuzindua Bodi hiyo jijini Dar es Salaam. 


Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) Capt. Budodi Budodi akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya taasisi yake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kabla ya Waziri huyo kuzindua Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali jijini Dar es Salaam. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akikabidhi vitendea kazi kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi, Idrissa Mshoro, mara baada ya Waziri huyo kuzindua Bodi ya Ushauri ya Wakala hiyo jijini Dar es Salaam. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali mara baada ya kuzindua Bodi hiyo jijini Dar es Salaam. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiagana na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) Capt. Budodi Budodi mara baada ya Waziri huyo kuwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam kuzindua Bodi ya Ushauri ya Wakala hiyo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu, Bw. Mululi Mahendeka na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi, Idrissa Mshoro. 



 

 

Thursday, August 24, 2023

MHE. SIMBACHAWENE AIPONGEZA WHI KWA KUENDELEA KUJENGA MAKAZI BORA YA WATUMISHI , ASISITIZA KUJENGA ZAIDI KARIBU NA MAENEO YA KAZI

 Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 24 Agosti, 2023

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameipongeza Taasisi ya Watumishi Housing Investments (WHI) kwa kuendelea kujenga makazi bora ya watumishi wa umma nchini na kuwasisitiza kuelekeza nguvu zaidi ya ujenzi jirani na maeneo ambayo watumishi wanafanya kazi ili kuwaondolea changamoto ya makazi kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.

Me. Simbachawene amezungumza hayo jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba zilizojengwa na taasisi hiyo eneo la Njedengwa  na Kisasa Relini kwa lengo la kuwauzia na kuwapangisha watumishi wa umma na wanachama wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Mhe. Simbachawene amesema kitendo cha watumishi wa umma kutokuwa na makazi bora na kuwa mbali na maeneo yao wanayofanyia kazi ni changamoto kubwa inayoathiri utendaji kazi, hivyo ameisisitiza taasisi hiyo kuona umuhimu wa kufanya hivyo kwani licha ya kuwasaidia watumishi kupata makazi bora watakuwa wametekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hasssan ya kuhimiza uwepo wa makazi bora kwa watumishi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa, umuhimu wa kuwa na makazi bora karibu na maeneo ya kazi, kutawasaidia watumishi hasa wanaoajiriwa kwa mara ya kwanza maeneo ambayo yana changamoto ya nyumba, kutohangaika.

“Mkijenga nyumba maeneo ya jirani na vituo vya kazi, kutawasaidia sana watumishi hasa wa ajira mpya kutopata changamoto na kuchukia kazi kwa sababu ya kuhangaika kutafuta sehemu nzuri ya kuishi,” Mhe. Simbachawene amesisitiza.

Kwa upande wake Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameungana na Mhe. Simbachawene kuipongeza taasisi hiyo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kujenga nyumba bora kwa ajili ya kuwauzia na kuwapangisha watumishi wa umma na wanachama wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Naye, Mtendaji Mkuu wa Watumishi Housing Investments (WHI) Dkt. Fredy Msemwa, amewashukuru viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kutembelea mradi wa ujenzi wa nyumba zinazojegwa na taasisi hiyo katika eneo la Kisasa Relini na Njedengwa na kuhimiza uwajibikaji na ubunifu.

Dkt. Msemwa amewaahidi viongozi hao kuwa, watayafanyia kazi maelekezo yote ambayo wameyatoa kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kukagua mradi wa nyumba zilizojengwa na Watumishi Housing Investments (WHI) eneo la Njedengwa na Kisasa Relini jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa WHI.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kukagua mradi wa nyumba zilizojengwa na Watumishi Housing Investments (WHI) eneo la Njedengwa na Kisasa Relini jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa WHI.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Investments (WHI), Dkt. Fred Msemwa alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi wa nyumba zilizojengwa na WHI eneo la Njedengwa na Kisasa Relini jijini Dodoma. Kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi yake, Bw. Xavier Daudi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiambatana na Naibu Waziri wake, Mhe. Ridhiwani Kikwete na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi yake, Bw. Xavier Daudi wakielekea kukagua mradi wa nyumba zilizojengwa na Watumishi Housing Investments (WHI) eneo la Njedengwa jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa WHI.


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akimuonyesha Mtendaji wa Watumishi Housing Investments (WHI), Dkt. Fred Msemwa namna alivyovutiwa na mojawapo ya nyumba zilizojengwa na Watumishi Housing Investments (WHI) walipokuwa wakimsubiri Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kukagua mradi wa nyumba hizo eneo la Kisasa Relini jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na Menejimenti ya Watumishi Housing Investments (WHI) wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua nyumba zilizojengwa na Watumishi Housing Investments (WHI) eneo la Njedengwa na Kisasa Relini jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na Menejimenti ya Watumishi Housing Investments (WHI) wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua nyumba zilizojengwa na Watumishi Housing Investments (WHI) eneo la Njedengwa na Kisasa Relini jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza jambo na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene iliyolenga kukagua mradi wa nyumba zilizojengwa na Watumishi Housing Investments (WHI) eneo la Njedengwa na Kisasa Relini jijini Dodoma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza jambo na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene iliyolenga kukagua mradi wa nyumba zilizojengwa na Watumishi Housing Investments (WHI) eneo la Njedengwa na Kisasa Relini jijini Dodoma.


Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Investments (WHI), Dkt. Fred Msemwa akitoa ufafanuzi kwa Waandishi wa Habari kuhusu mradi wa nyumba zilizojengwa na WHI eneo la Njedengwa na Kisasa Relini jijini Dodoma. 














Wednesday, August 23, 2023

Tuesday, August 15, 2023

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAPONGEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA KWA KUIPA USHIRIKIANO KAMATI HIYO WAKATI WA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAKE

 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akiongoza kikao kazi cha kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa mwaka 2022/23.

Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kuwasilisha Utekelezaji wa Mpango na Bajeti wa taasisi zilizo chini ya Ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa mwaka 2022/23.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwasilisha taarifa ya Utelezaji wa Mpango na Bajeti wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa mwaka 2022/23 kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha kamati hiyo kilichofanyika jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa neno la shukrani kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi cha kamati hiyo kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti wa taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa mwaka 2022/23 kilichofanyika jijini Dodoma.


Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA), Cpt. Budodi Budodi akijibu moja ya hoja ya taasisi yake kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa Mwaka 2022/23.

 


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba akitoa ufafanuzi wa hoja za masuala ya serikali mtandao zilizowasilishwa na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) Kwa Mwaka 2022/23.


Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Deogratias Usangira akijibu moja ya hoja ya Taasisi ya UONGOZI kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa Mwaka 2022/23.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Mashimba Ndaki akichangia hoja kuhusu serikali mtandao wakati wa kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na viongozi pamoja na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa Mwaka 2022/23.

 


Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Majula Mahendeka akitoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja iliyowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa Mwaka 2022/23.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akitoa ufafanuzi wa moja ya hoja iliyowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Katiba na Sheria wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa Mwaka 2022/23.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao kazi cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na Watendaji wa ofisi hiyo kuhusu Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo (TGFA, eGA na Taasisi ya UONGOZI) kwa Mwaka 2022/23.