Saturday, May 11, 2019

DKT. MWANJELWA AWATAKA WAHITIMU WA TPSC KUWA WAADILIFU, WACHAPAKAZI NA WAZALENDO WANAPOTEKELEZA MAJUKUMU YAO



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na wahitimu na wananchi waliohudhuria mahafali ya 30 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Kampasi ya Mtwara.
Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza mgeni rasmi, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (hayupo pichani) wakati wa mahafali ya 30 ya chuo hicho yaliyofanyika katika Kampasi ya Mtwara.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na menejimenti ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) na baadhi ya wahitimu wa mahafali ya 30 ya chuo hicho yaliyofanyika katika Kampasi ya Mtwara.
Baadhi ya wanafunzi bora waliohitimu Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakiwa mbele ya meza kuu mara baada ya kukabidhiwa vyeti na zawadi wakati wa mahafali ya 30 ya chuo hicho yaliyofanyika katika Kampasi ya Mtwara.
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Dkt. Charles Msonde akitoa neno la utangulizi wakati wa mahafali ya 30 ya chuo hicho yaliyofanyika katika Kampasi ya Mtwara.

Kaimu Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Emmanuel Shindika akitambulisha makundi ya wahitimu wakati wa mahafali ya 30 ya chuo hicho yaliyofanyika katika Kampasi ya Mtwara.

No comments:

Post a Comment