Wednesday, April 18, 2018

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAPATA MFANYAKAZI BORA WA MWAKA 2018


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bi. Dorothy Mwaluko akifungua mkutano wa kumchagua mfanyakazi bora wa mwaka 2018 wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora uliofanyika mapema leo katika ofisi hiyo mkoani Dodoma.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bi. Dorothy Mwaluko akitoa maelekezo kuhusu uchaguzi wa kumpata mfanyakazi bora wa ofisi wa mwaka 2018.

Wawakilishi wa wafanyakazi bora wa Idara/Vitengo vya Ofisi ya Rais-Utumishi wakishuhudia zoezi la kuhesabu kura ili kumpata mfanyakazi bora wa ofisi wa mwaka 2018.

No comments:

Post a Comment