Wednesday, January 22, 2025

WAZIRI SIMBACHAWENE AMJIBU MHE. FREEMAN MBOWE

 Na Lusungu Helela - SINGIDA 

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene amemshukia aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  Mhe. Freeman Mbowe kuhusiana na  hoja yake aliyoitoa ya kubeza juhudi ya Serikali ya kutaka kuondoa umaskini wa watu kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa kuwagawia fedha.

 

Mhe. Simbachawene ameyasema hayo  leo mara baada ya kukagua miradi mbalimbali  ya maendeleo iliyotekelezwa kupitia  TASAF Mkoani Singida ambapo amesema TASAF ni mpango mmojawapo wa uwezeshaji wananchi  kiuchumi lakini Serikali ina mipango lukuki.

 

"Jana (juzi)  nilikuwa nasikiliza  ule Mkutano wa Uchaguzi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  nilimsikia Mhe. Mbowe wakati akitoa taarifa ya Chama hicho kuwa  "Serikali ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) inataka kuondoa umaskini wa watu kupitia TASAF kwa kuwagawia fedha" 

 

"Ni kweli  Serikali ya CCM inataka kuondoa umaskini wa watu wake hasa wale wasiojiweza kabisa kwa kuwasaidia kifedha lakini pia Serikali hii inatumia mfuko wa TASAF kuondoa changamoto zinazogusa maisha ya wananchi moja kwa moja  kwa kwenda kurekebisha miundombinu pamoja na vikwazo katika maisha yao ikiwemo ujenzi  wa vivuko ili waweze kwenda mashambani kwa urahisi hususan wakati wa msimu wa mvua"  amesisitiza Mhe. Simbachawene

 

Pia, Mhe. Simbachawene amesema Serikali kupitia  TASAF imekuwa ikijenga vituo vya afya mahali ambako kuna zahanati zisizokidhi mahitaji ya wananchi ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya lengo likiwa ni kupambana na umaskini

 

"Nataka nimwambie Kaka yangu Mbowe kwamba  TASAF ni mpango mmojawapo wa kuwezesha wananchi wetu kiuchumi lakini Serikali yetu ina mipango mingi sana  na tunayo Sera ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi" amesisitiza Mhe. Simbachawene 

 

Amesema Serikali ina  Mfuko wa uwezeshaji wa wananchi kiuchumi ambapo kuna njia mbalimbali za kuwagusa kiuchumi ikiwemo  vijana na makundi mbalimbali lengo likiwa ni kupambana na umasikini na kuwapa ahueni katika hali zao za maisha

 

Ameongeza kuwa "Tuna mpango wa kuwawezesha kiuchumi kwa kutoa mikopo kwa  Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu ambapo asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri hupelekwa kwa ajili ya kukopesha makundi hayo.

 

Mbali na mipango hiyo Mhe. Simbachawene ameitaja mipango mingine ya uwezeshaji wananchi kiuchumi kuwa ni  utoaji  ruzuku kwenye  pembejeo za kilimo, utoaji wa mikopo ya elimu ya juu,  ujenzi wa Shule za Sekondari kila Kata pamoja  na Shule za Msingi kila Kijiji, utoaji wa mikopo ya Elimu ya juu pamoja na matibabu bure kwa wazee

 




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene  akizungumza na wanufaika wa TASAF katika Kijiji cha Kinyakaya kilichopo katika   Mkoa wa  Singida

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akikagua Mradi wa upandaji  miti kupitia TASAF uliotekelezwa katika Kijiji cha Kinyakaya kilichopo katika   Mkoa wa  Singida



Baadhi ya Wanufaika wa TASAF wakimsikiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene wakati akizungumza nao katika Kijiji cha Kinyakaya kilichopo katika   Mkoa wa  Singida

 



Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhe. Godwin Gondwe akizungumza na walengwa  wa TASAF katika  Kijiji cha Kinyakaya kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na walengwa hao Mkoani Singida 

 

 




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa ameongoza na Mkuu wa Wilaya ya Singida  Mhe. Godwin Gondwe mara baada ya kuwasili Mkoani Singida kwa ajili ya ziara ya kikazi 

 

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiagana na wanufaika wa mpango wa kuondoa umasikini mara baada ya kuzungumza  nao katika Kijiji cha Kinyakaya kilichopo katika Mkoa wa  Singida

 

 

 

 

 

 

 

 

No comments:

Post a Comment