Friday, January 24, 2025

KAMATI YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAIPONGEZA SEKRETARIETI YA AJIRA

 Na.Lusungu Helela — DODOMA

  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imeipongeza Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma  kwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kuhakikisha michakato ya ajira inafanyika kwa ufanisi na kwa uwazi wa hali ya juu.  

 

Mwenyekiti wa Kamati hiyo , Mhe. Dkt. Joseph Mhagama ametoa pongezi hizo leo jijini Dodoma kwa niaba ya Kamati yake wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Septemba 2024 hadi Januari  2025.

 

Mhe. Dkt. Mhagama mesema kitendo cha usaili kufanyika katika ngazi za mikoa badala ya kuwalazimu waombaji kazi wote kufika jijini Dodoma kumeleta  ahueni kubwa kwa waombaji kazi hao hususani wale waliotoka kwenye familia maskini.

 

 Hapo awali wazazi walilazimika kuuza ardhi au ngombe ili kijana wao aweze kusafiri kuja jijini Dodoma kwa ajili ya kufanya usaili ila ubunifu wa kufanya usaili kimkoa umerahisishia. Amesema  Mhe. Dkt. Mhagama amesema

 

Amesisitiza kuwa  utaratibu huo umeondoa usumbufu pamoja na kumfanya Muombaji  kazi  kutokutumia gharama ya usafiri kwa ajili ya kufika jijini Dodoma  kufanya usaili

 

 Akizungumzia matumizi ya mfumo wa Ajira Portal kwa waombaji kazi Mhe.Dkt. Mhagama  amesema mfumo juo umeondoa dhana ya upendeleo wa kupata ajira katika Utumishi wa Umma na kuchagiza ushindani miongoni mwa waombaji kwani hutoi fursa ya kuonana ana kwa ana na wahusika

 

Nimekuwa nikipokea simu nyingi kutoka kwa Watoto wa  familia masikini wa kutoka vijijini wakiwa wamepata ajira serikalini pasipo kumjua yeyote aliyepo serikalini amesisitiza Mhe.Dkt. Mhagama

 

Kwa Upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene amesema ajira katika Utumishi wa Umma zinapatikana kwa ushindani kutokana na idadi kubwa ya wasomi iliyopo lakini nafasi ni chache

 

Ametumia fursa hiyo kuwaomba Wajumbe wa Kamati hiyo kuwa Mabalozi wa Sekretariet ya Ajira Katika Utumishi wa Umma kwa kuwaeleza wananchi kuwa ajira katika Utumishi wa Umma hazihitaji kumjua yeyote na cha msingi ni kufuata taratibu zilizowekwa na Sekretarieti hiyo wakati wa  kuomba kazi.

 

Mwenyekiti wa Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria , Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akizungumza na Wajumbe mara baada ya Naibu Waziri Mhe. Deus Sangu kuwasilisha taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora kwa niaba ya Waziri Mhe. George Simbachawene

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene  akijibu hoja zilizotolewa na Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria mara baada ya Wajumbe hao kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora

 



Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria  wakimsikiliza  Naibu Waziri Mhe. Deus Sangu mara baada ya  kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora kwa niaba ya Waziri Mhe. George Simbachawene

 



Naibu Waziri , Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu  akiwasilisha  taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora kwa niaba ya Waziri Mhe. George Simbachawene mbele ya Wajumbe wa Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria

 



Baadhi ya Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao  kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya Ofisi hiyo kilichofanyika leo Jijini Dodoma

 





 Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria  wakijadili mara baada ya  kupokea  taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora kwa niaba ya Waziri Mhe. George Simbachawene

 

 

 

No comments:

Post a Comment