Thursday, January 30, 2025
Wednesday, January 29, 2025
SERIKALI YAZIDI KUWAPANDISHA VYEO MAELFU YA WATUMISHI
Na Lusungu Helela-Dodoma
Serikali imesema kwamba katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 imewapandisha vyeo watumishi 180,000 wakiwemo watumishi walioathirika na mwongozo wa upandaji madaraja wa miaka minne.
Mhe. Sangu amesema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Janejelly Ntate aliyetaka kujua Serikali imejipangaje kukwamua watumishi walioathiriwa na mwongozo wa upandaji madaraja wa miaka minne.
Aidha, katika utekelezaji wa Ikama na Bajeti ya Mwaka 2023/2024, Serikali imewapandisha vyeo watumishi zaidi ya 232,530 wakiwemo walioathirika na zoezi hilo, uhakiki wa vyeti feki na watumishi hewa
NAIBU WAZIRI MHE. SANGU:MFUMO WA UPIMAJI UTENDAJI KAZI KUJAZWA KILA WIKI NA WATUMISHI NA SIO VINGINEVYO
Lusungu Helela-Dodoma
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu amesema Mfumo wa upimaji wa utendaji kazi kwa Watumishi wa Umma ujulikanao kama PEPMIS utaendelea kujazwa kwa wiki kama ilivyopangwa.
Mhe. Deus Sangu amesema hayo Bungeni leo Jummane Januari 29, 2025 wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhe. Sophia Mwakagenda aliyetaka kujua kwa nini watumishi wa afya wasijaze ripoti za utendaji kila mwezi badala ya kila wiki ili wapate muda zaidi kuhudumia wagonjwa
Tuesday, January 28, 2025
Monday, January 27, 2025
WATUMISHI WA OFISI YA RAIS-UTUMISHI WASISITIZWA KUZINGATIA ITIFAKI NA DIPLOMASIA KATIKA UTENDAJI KAZI
Na. Mwandishi Wetu
Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wamesisitizwa
kuzingatia Itifaki na Diplomasia katika utendaji kazi Ili kujenga
heshima ya ofisi kwa manufaa ya nchi.
Wito huo umetolewa leo Januari 27, 2025 na Balozi Nelson Lyimo (mstaafu) wakati akifanya wasilisho kuhusu Itifaki na Diplomasia
kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
katika Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma.
Balozi Lyimo amesema, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ni muhimu
kwa Taifa la Tanzania kwa kuwa inasimamia rasilimaliwatu, hivyo Watumishi wake
wanatakiwa kuzingatia Itifaki na Diplomasia wakati wote wanapotekeleza majukumu
yao katika ofisi hiyo.
Amewasisitiza Watumishi kuwa wasikivu kwa wateja
wanaowahudumia na kuona namna ya kuwasaidia kupata majibu au suluhisho la suala
ambalo mteja husika ameliwasilisha.
“Niwaombe kila mtumishi wa ofisi hii ajipime namna
anavyotoa huduma kwa wateja kwani ndio kipimo cha tabia njema wakati wa
utendaji kazi, jambo ambalo litaenda kuitangaza ofisi vizuri kwa maslahi mapana
ya taifa, amesisitiza Balozi Lyimo.
Akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi
hao, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Utawala, Bw. Musa Magufuli alimshukuru Balozi Lyimo kwa kutoa
elimu hiyo kwa watumishi hao
ambayo itaboresha utendaji kazi kwa watumishi wao.
Ofisi ya Rais-UTUMISHI iliandaa utaratibu wa kutoa mafunzo kwa watumishi wake kila Jumatatu ya wiki kwa lengo la kutoa uelewa kuhusu masuala mbalimbali katika Utumishi wa Umma ili kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa ustawi wa Taifa.
Balozi Nelson Lyimo (mstaafu) akizungumza wakati akiwasilisha mada kuhusu Itifaki na Diplomasia kwenye mafunzo
ya kuwajengea uwezo watumishi wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI yaliyofanyika
katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Musa Magufuli (aliyesimama
mbele kulia) akitoa shukrani kwa Balozi Nelson Lyimo (aliyesimama mbele kushoto) mara baada ya Balozi huyo kuhitimisha mada kuhusu Itifaki na Diplomasia wakati wa mafunzo
ya kuwajengea uwezo watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika
katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya
kuwajengea uwezo watumishi hao katika masuala ya utendaji kazi yaliyofanyika
katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Friday, January 24, 2025
KAMATI YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAIPONGEZA SEKRETARIETI YA AJIRA
Na.Lusungu Helela — DODOMA
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imeipongeza Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kuhakikisha michakato ya ajira inafanyika kwa ufanisi na kwa uwazi wa hali ya juu.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo , Mhe. Dkt.
Joseph Mhagama ametoa pongezi hizo leo jijini Dodoma kwa niaba ya Kamati yake
wakati wa kikao kazi cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilicholenga kupokea
na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya mwezi Septemba 2024 hadi Januari 2025.
Mhe. Dkt. Mhagama mesema kitendo cha
usaili kufanyika katika ngazi za mikoa badala ya kuwalazimu waombaji kazi wote
kufika jijini Dodoma kumeleta ahueni
kubwa kwa waombaji kazi hao hususani wale waliotoka kwenye familia maskini.
Hapo awali wazazi walilazimika kuuza ardhi au
ngombe ili kijana wao aweze kusafiri kuja jijini Dodoma kwa ajili ya kufanya
usaili ila ubunifu wa kufanya usaili kimkoa umerahisishia. Amesema Mhe. Dkt. Mhagama amesema
Amesisitiza kuwa utaratibu huo umeondoa usumbufu pamoja na
kumfanya Muombaji kazi kutokutumia gharama ya usafiri kwa ajili ya
kufika jijini Dodoma kufanya usaili
Akizungumzia
matumizi ya mfumo wa Ajira Portal kwa waombaji kazi Mhe.Dkt. Mhagama amesema mfumo juo umeondoa dhana ya upendeleo
wa kupata ajira katika Utumishi wa Umma na kuchagiza ushindani miongoni mwa
waombaji kwani hutoi fursa ya kuonana ana kwa ana na wahusika
Nimekuwa nikipokea simu nyingi kutoka
kwa Watoto wa familia masikini wa kutoka
vijijini wakiwa wamepata ajira serikalini pasipo kumjua yeyote aliyepo
serikalini amesisitiza Mhe.Dkt. Mhagama
Kwa Upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene
amesema ajira katika Utumishi wa Umma zinapatikana kwa ushindani kutokana na
idadi kubwa ya wasomi iliyopo lakini nafasi ni chache
Ametumia fursa hiyo kuwaomba Wajumbe wa
Kamati hiyo kuwa Mabalozi wa Sekretariet ya Ajira Katika Utumishi wa Umma kwa
kuwaeleza wananchi kuwa ajira katika Utumishi wa Umma hazihitaji kumjua yeyote
na cha msingi ni kufuata taratibu zilizowekwa na Sekretarieti hiyo wakati wa kuomba kazi.
Mwenyekiti wa Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria , Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akizungumza na Wajumbe mara baada ya Naibu Waziri Mhe. Deus Sangu kuwasilisha taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora kwa niaba ya Waziri Mhe. George Simbachawene
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene
akijibu hoja zilizotolewa na Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria mara baada ya Wajumbe hao kupokea na kujadili
taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala
Bora
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya ya
Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza
Naibu Waziri Mhe. Deus Sangu mara baada ya kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi wa
Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora kwa niaba ya Waziri Mhe. George
Simbachawene
Naibu Waziri , Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi wa
Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora kwa niaba ya Waziri Mhe. George
Simbachawene mbele ya Wajumbe wa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria
Baadhi ya Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao kilicholenga kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kazi ya Ofisi hiyo kilichofanyika leo Jijini Dodoma
WAZIRI SIMBACHAWENE: USHINDANI WA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA NI JAMBO LISILOEPUKIKA KWA SASA
Na.Lusungu Helela - SINGIDA
Amesema dhamira hiyo ya kuhakikisha
waombaji kazi wote wanafanya usaili kunasaidia
kuwapata watumishi wenye sifa stahiki katika utumishi wa umma na kuondoa dhana
ya upendeleo iliyokuwa imejengeka miongoni mwa watu
Hata hivyo, Mhe.Simbachawene ametumia fursa hiyo kuwasihi waombaji kazi kuhakikisha wanaweka vyeti vyao vinavyotakiwa ili kuepuka na mchujo katika hatua za awali.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene
akizungumza na wasailiwa wakati alipotembelea kituo cha usaili wa kada za
Ualimu Mkoani
Singida ili kujionea mwenendo wa zoezi hilo.
Baadhi ya Wasailiwa wa kada ya Ualimu wakimskiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene wakati alipotembelea kituo cha usaili wa kada za Ualimu Mkoani Singida ili kujionea mwenendo wa zoezi hilo,
Mkuu wa Mkoa wa ya Singida Mhe. Halima Dendego akizungumza leo
wakati alipotembelea kituo cha usaili wa kada za Ualimu
Mkoani Singida ili kujionea mwenendo wa zoezi
hilo,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa na Mkuu wa Mkoa wa
Singida Mhe. Halima Dendego pamoja na viongozi wengine mara baada
ya kuwasili kwa ajili ya kutembelea kituo cha usaili wa kada za Ualimu
Mkoani Singida ili kujionea mwenendo wa zoezi
hilo,
Wednesday, January 22, 2025
WAZIRI SIMBACHAWENE AMJIBU MHE. FREEMAN MBOWE
Na Lusungu Helela - SINGIDA
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene amemshukia aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Freeman Mbowe kuhusiana na hoja yake aliyoitoa ya kubeza juhudi ya Serikali ya kutaka kuondoa umaskini wa watu kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa kuwagawia fedha.
Mhe.
Simbachawene ameyasema hayo leo mara baada ya
kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa kupitia TASAF
Mkoani Singida ambapo amesema TASAF ni mpango mmojawapo wa uwezeshaji
wananchi kiuchumi lakini Serikali ina mipango lukuki.
"Jana (juzi)
nilikuwa nasikiliza ule Mkutano wa Uchaguzi wa Chama Cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) nilimsikia Mhe. Mbowe wakati akitoa taarifa ya Chama
hicho kuwa "Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inataka
kuondoa umaskini wa watu kupitia TASAF kwa kuwagawia fedha"
"Ni kweli Serikali ya
CCM inataka kuondoa umaskini wa watu wake hasa wale wasiojiweza kabisa kwa
kuwasaidia kifedha lakini pia Serikali hii inatumia mfuko wa TASAF kuondoa
changamoto zinazogusa maisha ya wananchi moja kwa moja kwa kwenda kurekebisha
miundombinu pamoja na vikwazo katika maisha yao ikiwemo ujenzi wa vivuko
ili waweze kwenda mashambani kwa urahisi hususan wakati wa msimu wa
mvua" amesisitiza Mhe. Simbachawene
Pia, Mhe. Simbachawene
amesema Serikali kupitia TASAF imekuwa ikijenga vituo vya afya mahali
ambako kuna zahanati zisizokidhi mahitaji ya wananchi ili kuhakikisha wananchi
wanapata huduma bora za afya lengo likiwa ni kupambana na umaskini
"Nataka nimwambie Kaka yangu
Mbowe kwamba TASAF ni mpango mmojawapo wa kuwezesha wananchi wetu
kiuchumi lakini Serikali yetu ina mipango mingi sana na tunayo Sera ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi"
amesisitiza Mhe. Simbachawene
Amesema Serikali ina Mfuko wa
uwezeshaji wa wananchi kiuchumi ambapo kuna njia mbalimbali za kuwagusa
kiuchumi ikiwemo vijana na makundi mbalimbali lengo likiwa ni kupambana
na umasikini na kuwapa ahueni katika hali zao za maisha
Ameongeza kuwa "Tuna mpango wa
kuwawezesha kiuchumi kwa kutoa mikopo kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye
Ulemavu ambapo asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri hupelekwa kwa
ajili ya kukopesha makundi hayo.
Mbali na mipango hiyo Mhe. Simbachawene
ameitaja mipango mingine ya uwezeshaji wananchi kiuchumi kuwa ni utoaji ruzuku kwenye pembejeo za
kilimo, utoaji wa mikopo ya elimu ya juu, ujenzi wa Shule za Sekondari
kila Kata pamoja na Shule za Msingi kila Kijiji, utoaji wa mikopo ya
Elimu ya juu pamoja na matibabu bure kwa wazee
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na wanufaika wa TASAF katika Kijiji cha Kinyakaya kilichopo katika Mkoa wa Singida
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akikagua Mradi wa upandaji miti kupitia TASAF uliotekelezwa katika Kijiji cha Kinyakaya kilichopo katika Mkoa wa Singida
Baadhi ya Wanufaika wa TASAF
wakimsikiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene wakati akizungumza nao katika Kijiji cha Kinyakaya
kilichopo katika Mkoa wa Singida
Mkuu wa Wilaya ya Singida
Mhe. Godwin Gondwe akizungumza na walengwa wa TASAF katika
Kijiji cha Kinyakaya kabla ya
kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na walengwa hao Mkoani
Singida
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa
ameongoza na Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhe. Godwin Gondwe mara baada ya kuwasili
Mkoani Singida kwa ajili ya ziara ya kikazi
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George
Simbachawene akiagana na wanufaika wa mpango wa kuondoa umasikini mara baada ya
kuzungumza nao katika Kijiji cha Kinyakaya kilichopo katika Mkoa wa Singida