Monday, April 15, 2024

MFUMO WA AJIRA WADUMISHA MUUNGANO WA TANZANIA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kipindi cha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kuweka utaratibu wa mgao wa ajira unaotekelezwa kwa mujibu wa Waraka wa Serikali wa tarehe 10 Mei, 2013 ambapo Tanzania Bara ni asilimia 79 na Tanzania Zanzibar ni asilimia 21.

 

Ameyasema hayo leo Aprili 15, 2024 jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya miaka 60 ya Muungano kwa upande wa Ofisi yake.

 Amesema katika kipindi hicho cha miaka 60 ya Muungano, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imekuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na Tume ya Utumishi wa Umma Zanzibar inayoratibu masuala ya ajira katika watumishi wa umma ili kurahisisha zoezi la utangazaji wa nafasi za kazi na upatikanaji wa watumishi.

 Kutokana na ukuaji wa teknolojia, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imesanifu na kujenga mfumo wa kidijitali wa ajira Serikalini ambao ni rafiki kwa watafuta fursa wote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Aidha, Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa utengenezaji wa programu ya rununu (Ajira Portal Mobile App) inayopatikana kwenye PlayStore na ApStore za simu janja inalenga kuimarisha Muungano kwa kuwarahisishia waombaji wa fursa za ajira kupata taarifa za uwepo wa fursa hizo kiganjani mwao mahali popote.

 Katika hatua nyingine Mhe. Simbachawene amesema Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imedhamiria kuondoa changamoto zinazowakabili waombaji wa fursa za ajira Tanzania Bara na Zanzibar.

 

Aidha, matumizi ya mifumo ya TEHAMA katika kipindi hiki cha miaka 60 ya Muungano imesaidia waombaji kuepuka gharama za usafiri, malazi na changamoto za ajali, wakati Serikali imepunguza muda wa usaili na gharama za uendeshaji wa zoezi hilo.

 

Mhe. Simbachawene amewataka watafuta fursa za ajira wote kutoka pande mbili za Muungano kufahamu akaunti zao, nywila na kuwa mahiri katika matumizi ya kompyuta ili kuepukana na usumbufu.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza kwenye  Mkutano na  Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala bora leo Jijini Dodoma.  

Sehemu ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati  akizungumza kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Maelezo, Bi. Zamaradi Kawawa akitoa neon la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na Waandishi wa Habari  kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala bora leo Jijini Dodoma.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (katikati) akiwa na baadhi ya Wakurugenzi baada ya kuzungumza na   Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala bora, wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Mary Mwakapenda

Baadhi ya Watumishi kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakimsiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati akizungumza na  Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

 

No comments:

Post a Comment