Sunday, October 16, 2016

MHE. KAIRUKI AWAHIMIZA WATUMISHI WA UMMA MKOANI MWANZA KUJISAJILI KWA AJILI YA KUPATA VITAMBULISHO VYA TAIFA KABLA YA MUDA WA ZOEZI HILO KWISHA

Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Mkoa wa Mwanza Bw. Daud Hashimu Abdallah akiwasilisha taarifa ya usajili wa watumishi wa umma  kwa ajili ya kupatiwa Vitambulisho vya Taifa kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki  (hayupo pichani)  wakati wa ziara ya  kikazi  ya waziri huyo  mkoani  Mwanza kwa ajili ya kukagua na kufanya tathmini ya zoezi la usajili wa watumishi  wa umma ili kupata Vitambulisho vya Taifa.

Mkurugenzi wa Halimashauri ya Wilaya Misungwi Bw. Eliurd L. Mwaiteleke (kulia) akimuongoza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (katikati) kwenda katika moja ya kituo cha kusajili watumishi wa umma kwa ajili ya kupatiwa Vitambulisho vya Taifa wakati wa ziara ya waziri huyo ili kuona namna zoezi hilo linavyoendeshwa katika Halimashauri ya Wilaya Misungwi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki akipewa ufafanuzi  na Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa wa Halimashauri ya Wilaya Misungwi Bw. Abbasi Iwodya (kulia) juu ya taarifa zinazowasilishwa na watumishi wa umma kwa ajili ya  kupatiwa Vitambulisho vya Taifa wakati wa ziara ya  kikazi  ya waziri huyo  aliyoifanya katika Halimashauri ya Wilaya Misungwi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na mmoja wa watumishi  aliyekuwa akijisajili  kwa ajili ya kupata Kitambulisho cha Taifa wakati wa ziara ya waziri huyo ya kukagua na kufanya tathmini ya zoezi hilo katika Halimashauri ya Wilaya Misungwi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akikagua viambatisho vya malalamiko yaliyowasilishwa na mmoja wa watumishi wa Halimashauri ya Wilaya Misungwi wakati wa ziara ya  kikazi  ya waziri huyo  aliyoifanya katika Halimashauri hiyo ili kukagua na kufanya tathmini ya zoezi la usajili wa watumishi wa umma  kwa ajili ya kupatiwa Vitambulisho vya Taifa mkoani Mwanza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akipokea malalamiko ya mtumishi wa Halimashauri ya Wilaya Misungwi wakati wa ziara ya  kikazi  ya waziri huyo  aliyoifanya katika Halimashauri hiyo ili kukagua na kufanya tathmini ya zoezi la usajili wa watumishi wa umma  kwa ajili ya kupatiwa Vitambulisho vya Taifa mkoani Mwanza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na watumishi wa Halimashauri ya Wilaya Misungwi wakati wa ziara ya  kikazi  ya waziri huyo  aliyoifanya katika Halimashauri hiyo ili kukagua na kufanya tathmini ya zoezi la usajili wa watumishi wa umma  kwa ajili ya kupatiwa Vitambulisho vya Taifa mkoani Mwanza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akishuhudia mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela akisajiliwa  kwa ajili ya kupata Kitambulisho cha Taifa wakati wa ziara ya waziri huyo ya kukagua na kufanya tathmini ya zoezi hilo katika Halimashauri hiyo.

Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana waliojitokeza kwa ajili ya kujisajili ili kupata Vitambulisho vya Taifa wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya waziri huyo aliyoifanya katika Halmashauri hiyo ili kukagua na kufanya tathmini ya zoezi hilo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akishuhudia usajili wa watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana kwa ajili ya kupata Vitambulisho vya Taifa wakati wa ziara ya kikazi ya waziri huyo aliyoifanya katika Halmashauri hiyo ili kukagua na kufanya tathmini ya zoezi hilo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akisisitiza juu ya ukamilishaji wa zoezi la usajili wa watumishi wa umma mkoani Mwanza wakati wa ziara ya kikazi ya waziri huyo mkoani humo, aliyoifanya kwa lengo  la kufanya tathmini ya zoezi hilo . Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw. John Mongella akimsikiliza.

1 comment:

  1. mheshimiwa waziri nakupongeza kwa kazi nzuri unayoendelea kuifanya kwa ajiri ya kuboresha utumishi wa umma.
    Lakini kuna swala naona haliwekwi sawa pamoja na mamlaka kua ikitoa ufafanuzi, ni kuhusiana na sisi tuliositishiwa ajira na kurudishwa nyumbani kupisha zoezi hilo, serikali ipo kimya na haisemi ni lini tutarudishwa kazini takribani miezi minne imepita hatujui muafaka wetu. Tunakuomba sana mheshimiwa waziri tusaidie kuokoa maisha yetu sisi vijana tulio tayari kutumikia taifa letu katika utumishi wa umma, tunaomba kurudishwa kazini

    ReplyDelete