Tuesday, July 23, 2024

TAASISI ZA UMMA KUFANYA UHAKIKI WA TAKWIMU ZA WATUMISHI WA UMMA WENYE VVU, UKIMWI NA MAGONJWA SUGU YASIYOAMBUKIZA

 Na. Veronica Mwafisi-Manyara

Tarehe 23 Julai, 2024

Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Cyprus Kapinga amezitaka Wizara na Taasisi za Umma kufanya uhakiki wa takwimu za watumishi wa umma wenye VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY) ili kulinda afya za watumishi hao.

Bw. Kapinga ametoa wito huo leo wakati akifungua kikao kazi cha Robo ya Nne ya Mwaka 2023/2024 kilichoshirikisha Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa Mkoa wa Manyara wanaosimamia magonjwa hayo.

“Tunatakiwa kuwa na takwimu sahihi ya watumishi hao ili kurahisisha zoezi la kupanga bajeti ya kuwahudumia na kuimarisha afya ya akili na kudhibiti msongo wa mawazo. Watumishi hao ni sehemu ya nguvu kazi ya Taifa inayohudumia wananchi” alisisitiza Bw. Kapinga.

Aidha, Bw. Kapinga ametoa rai kwa Maafisa Masuuli wote katika taasisi za umma kuunda na kuimarisha Kamati za VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY) zilizopo kwa kutoa nafasi kwa wanakamati hao kupata mafunzo na elimu itakayowafanya wawe na uwezo wa kushawishi watumishi kupima afya na hivyo kuwa na takwimu sahihi kwa  mipango bora na endelevu.

Awali akitoa neno la utangulizi, Katibu Tawala Mkoa wa Manyara, Bi. Maryam Muhaji aliwataka washiriki wa kikao kazi hicho kusikiliza na kufuatilila kwa makini mada zote zitakazowasilishwa ili wapate uwezo na ujuzi Madhubuti wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kupitia Idara ya Uendelezaji Sera ipo mkoani Manyara kwa lengo la kujadili utekelezaji wa mapambano dhidi ya VVU, Ukimwi na Magonjwa yasiyoambukiza (MSY) ili kuwalinda watumishi wa umma na kuhakikisha taifa linaondokana na vifo vitokanavyo na magonjwa hayo ifikapo mwaka 2030.

Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyprus Kapinga akizungumza na Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara wanaosimamia magonjwa hayo wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024.


Baadhi ya Wakurugenzi wa Rasilimaliwatu wa Kamati ya Kitaifa ya Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY) na Waratibu wa magonjwa hayo wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyprus Kapinga (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kinachofanyika mkoani Manyara.


Katibu Tawala Mkoa wa Manyara, Bi. Maryam Muhaji akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyprus Kapinga kufungua kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 cha Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) kinachofanyika mkoani Manyara.

Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo akitoa utambulisho wa Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara wanaosimamia magonjwa hayo kwenye kikao kazi kilichofanyika mkoani Manyara.


Afisa Maendeleo ya Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Neema Range akiwasilisha mada kuhusu Ujumuishwaji wa Sehemu za Anuai za Jamii wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kilichoshirikisha Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara.


Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi na Mratibu wa Kitaifa wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Juliana Ntukey akiwasilisha mada kuhusu Mwongozo wa Waraka wa kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza mahali pa kazi katika Utumishi wa Umma (2014) wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024.


Mratibu wa VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY), Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara, Bi. Marietha Kyomo akiwasilisha taarifa ya Mkoa wa Manyara kuhusu hali ya utekelezaji wa Afua za VVU, Ukimwi na MSY wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kilichofanyika katika mkoa huo.


Mratibu wa Kinga na Mwitikio wa Kitaifa dhidi ya VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza, Dkt. Haffidh Ameir akitoa taarifa kuhusu hali halisi ya VVU na Ukimwi Nchini wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kilichoshirikisha Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara.


Daktari Bingwa wa Afya na Magonjwa ya Akili, Dkt. Sadiki Mandari akiwasilisha mada kuhusu kuimarisha afya ya akili kwa Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara wanaosimamia magonjwa hayo wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kinachofanyika mkoani Manyara.


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyprus Kapinga akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY) wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kinachofanyika mkoani Manyara.



 

No comments:

Post a Comment