Thursday, July 11, 2024

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YATOA MAFUNZO KWA WATENDAJI WA JESHI LA POLISI KUHUSU MFUMO WA E-UTENDAJI KAZI



Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, SACP. Ibrahim Mahumi (Wa kwanza kulia) akizungumza na Timu ya Utekelezaji wa Mchakato wa Matumizi ya Mfumo wa Tathmini ya Utendaji Kazi wa Watendaji wa Jeshi la Polisi katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mtumba Jijini Dodoma tarehe 11 Julai, 2024.

Kamishna wa Utawala na Rasilimaliwatu wa Jeshi la Polisi DCP. Gabriel Semiono (Wa Pili Kushoto) akifafanua jambo baada ya kuwasilishwa kwa taarifa fupi ya namna ya upimaji wa utendaji kazi wa watendaji wa Jeshi la Polisi kwa sasa ili waweze kutumia Mfumo wa Tathmini ya Utendaji Kazi (e-Utendaji). Kikao kazi kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mtumba Jijini Dodoma tarehe 11 Julai, 2024.


Mkurugenzi wa Huduma za TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango akifafanua jambo kwa Timu ya Utekelezaji wa Mchakato wa Matumizi ya Mfumo wa Tathmini ya Utendaji Kazi wa Watendaji wa Jeshi la Polisi (hawapo pichani) katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mtumba Jijini Dodoma tarehe 11 Julai, 2024.


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, SACP. Ibrahim Mahumi (Wa kwanza kulia) akifuatilia wasilisho la namna Mfumo wa e-Utendaji kazi unavyofanya kazi wakati akiongoza kikao kazi cha mafunzo na majadiliano ya namna ya kutumia mfumo huo. Wa Pili Kulia ni Kamishna wa Utawala na Rasilimaliwatu wa Jeshi la Polisi DCP. Gabriel Semiono aliyeongoza Timu ya Utekelezaji wa Mchakato wa Matumizi ya Mfumo wa Tathmini ya Utendaji Kazi wa Watendaji wa Jeshi la Polisi katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mtumba Jijini Dodoma tarehe 11 Julai, 2024.




No comments:

Post a Comment