Friday, June 23, 2023

WAZIRI MHE. SIMBACHAWENE AZITAKA TAASISI ZA UMMA KUZINGATIA MIKATABA YA HUDUMA KWA MTEJA KATIKA KUTOA HUDUMA BORA

 Na. Lusungu Helela-Dodoma

Tarehe 23 Juni, 2023

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amewataka Watumishi wa Umma kutoa huduma bora kwa wananchi huku akizitaka Taasisi zote za Umma kuhuisha Mikataba ya Huduma kwa Mteja kwani ni nyenzo na kiungo muhimu katika kuboresha utendaji kazi kati ya Serikali na Wananchi inaowahudumia.

Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Juni 23, 2023 wakati akizungumza na watumishi mbalimbali wa Serikali pamoja na wananchi walioshiriki  kwenye Uzinduzi  wa Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika  Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.

Mhe. Simbachawene amewataka Watumishi hao kutambua kuwa wanapotoa huduma bora kwa wananchi wanamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa akisisitiza suala hilo mara kwa mara.

Kufuatia hatua hiyo, amezitaka Taasisi za Umma kuzingatia Mikataba ya Huduma kwa Mteja katika utoaji wa huduma kwa wananchi ili haki na wajibu wa pande zote mbili utendeke kwa watoa huduma na wapokea huduma ambao ndio wateja.

Ameongeza kuwa Ofisi yake ina wajibu wa kusimamia mifumo na viwango vya utendaji kazi Serikalini kwa lengo la kuongeza uwajibikaji na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na moja ya mifumo na viwango  vya Utendaji Kazi huo ni Mkataba wa Huduma kwa Mteja.

Awali, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amesema uzinduzi wa Mikataba ya Huduma kwa Mteja ni moja ya hatua muhimu ya kuboresha huduma bora kwa wananchi ambapo amesema jumla ya Mikataba ya Huduma kwa Mteja 34 ya Taasisi za Umma imeweza kuzinduliwa.

"Uzinduzi wa mikataba hii ya Huduma kwa mteja inakwenda kuwezesha watumishi wa umma kuwa na utamaduni wa utendaji kazi unaojali matokeo na tija kwa wakati" amesema Mkomi

Aidha, Katibu Mkuu Mkomi ametumia fursa hiyo kuzipongeza Taasisi za Umma ambazo zimeadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma kwenye maeneo yao kama ilivyoelekezwa na Ofisi yake.

Naye, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Daudi Kandoro akitoa neno la shukrani mara baada ya uzinduzi wa mikataba hiyo  kwa niaba ya Wakuu wa Taasisi, amesema  watatekeleza maagizo yote yaliyotolewa huku akiahidi kutoa elimu kwa wananchi kuhusu kilichoandikwa katika mikataba hiyo ili wananchi waweze kujua wajibu na haki zao.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akizungumza na watumishi mbalimbali wa Serikali pamoja na wananchi walioshiriki  kwenye Uzinduzi  wa Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika  Kilele cha Maadhimisho Wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw.Juma Mkomi akizungumza wakati wa Uzinduzi  wa Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika  Kilele cha Maadhimisho Wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw.Xavier Daudi  akizungumza wakati wa Uzinduzi  wa Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika  Kilele cha Maadhimisho Wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akimkabidhi  Naibu Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Xavier Daudi  cheti cha  kuwa Mkataba wa Huduma  kwa Mteja uliokidhi viwango wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma wakati wa Uzinduzi  wa Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika  Kilele cha Maadhimisho wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora mara baada ya Uzinduzi  wa Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika  Kilele cha Maadhimisho Wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe.Rosemary Senyamule pamoja na viongozi wengine  akiiaga kwaya ya Chuo cha Utumishi wa Umma mara baada ya Uzinduzi  wa Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika  Kilele cha Maadhimisho wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.

 


 


Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene wakati wa Uzinduzi wa Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika  Kilele cha Maadhimisho Wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akifurahia jambo na Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw.Juma Mkomi wakati wa Uzinduzi  wa Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa na baadhi ya Watumishi wakifurahi mara baada ya kuzindua Mikataba ya Huduma  kwa Mteja ya Taasisi za Umma katika Kilele cha Maadhimisho Wiki ya  Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma. 

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda akizungumza wakati wa utoaji vyeti na Tuzo mbalimbali kwa Taasisi za Umma wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo Kitaifa yamnefanyika katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.






No comments:

Post a Comment