Monday, December 15, 2025

MKOMI ATOA WITO KWA WATUMISHI KUJICHUNGUZA KAMA WANAFAA KUWA VIONGOZI

 Na.Mwandishi Wetu

Tarehe 15 Disemba, 2025

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi amesema kuwa mtumishi wa umma anaweza kujifanyia uchunguzi (vetting) mwenyewe juu ya tabia na mwenendo katika utendaji kazi bila kusubiri taarifa ya vyombo vya usalama.

Bw. Mkomi alisema hayo Desemba 15, 2025 kwa Watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa kuhitimisha mafunzo ya uelewa wa namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi yaliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

“Mtumishi anaweza kujichunguza na kuona kama anafaa kuwa kiongozi au la, kwa sababu tabia njema au mbaya anaweza kuitambua kwa ufasaha mtumishi mwenyewe” alisema Bw. Mkomi.

Bw. Mkomi aliongeza kuwa tabia na mienendo ya watumishi inatakiwa kuwa na taswira chanya kwao wenyewe na mbele ya macho ya wale wanaopokea huduma kutoka kwao.

Aidha, Bw. Mkomi alisisitiza kuwa tabia na mienendo ya watumishi wa ofisi hiyo inatakiwa kwenda sambamba na misingi mikuu ya utendaji kazi wa ofisi, pia tabia hizo zitoe mitazamo chanya juu ya utendaji kazi wao na namna anavyowahudumia watumishi wa umma na umma kwa jumla.

Awali, Mkufunzi Bw. Moses Raymond alisema kuwa Watumishi  wa Ofisi ya Rais UTUMISHI ni kioo kwa watumishi wengine wote katika utumishi wa umma na ndio wenye dhamana ya kusimamia utumishi wa umma nchini. Hivyo, hawana budi kuwaongoza watumishi wengine vyema katika ujenzi wa taswira chanya ya Serikali.

Alifafanua kuwa, mtumishi wa Ofisi ya Rais UTUMISHI akifanya vibaya katika utoaji wa huduma, wananchi wanatafsiri kuwa watumishi wote wa ofisi hiyo wana tabia hiyo.

“Binafsi natoa rai katika mafunzo haya kuhakikisha  kila mmoja anashiriki ipasavyo katika jitihada za ujenzi wa taswira nzuri ya ofisi kwa kufanya vyema hususani katika utekelezaji wa majukumu yake ili kulinda taswira chanya ya ofisi” aliongeza Bw. Raymond.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya uelewa yanayofanyika kila Jumatatu ya Wiki katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi (Kulia) na Naibu Katibu Mkuu Bw. Xavier Daudi wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi wakati wa mafunzo ya uelewa yanaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi (Katika Mbele) na Naibu Katibu Mkuu Bw. Xavier Daudi (Wa kwanza kushoto), Viongozi na Watumishi wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond (Hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.


Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.

Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.


Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi kutoka kwa Mkufunzi Moses Raymond wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.


Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bi. Nyasinde Mkono  akitoa neno la shukurani baada ya mafunzo ya namna bora ya kulinda taswira nzuri ya taasisi yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma tarehe 15 Desemba, 2025.

Saturday, December 13, 2025

MATUKIO YA PICHA LEO DISEMBA 13, 2025 IKIWA KATIKA IBADA MAALUM YA KUAGA MWILI WA ALIYEWAHI KUWA WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS - UTUMISHI MAREHEMU JENISTA MHAGAMA JIJINI DODOMA

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasili katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kiwanja cha Ndege Jijini Dodoma leo tarehe 13/12/2025 kwa ajili ya kushiriki misa maalum ya kuuaga mwili wa Marehemu Mhe Jenista Mhagama ambaye aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiteta na mmoja wa wananchi aliyefika katika misa maalum ya kuuga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI Mhe. Jenista Mhagama jijini Dodoma Disemba 13, 2025.

 Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi akishiriki ibada maalum ya kuuaga  mwili wa Marehemu Mhe Jenista Mhagama ambaye aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI leo 13/12/2025 Jijini Dodoma.

 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi akiteta na Waziri wa Nchi Mambo ya Ndani Mhe. George Simbachawene leo Disemba 13, 2025 maara baada ya kumaliza ibada ibada maalum ya kuuaga  mwili wa Marehemu Mhe Jenista Mhagama ambaye aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI jijini Dodoma.


  Mkurugenzi wa Mishahara Malupulupu na Maslahi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Mariam Mwanilwa (Kulia) akiwa na Mkurugenzi Msaidizi Mipango na Bajeti ofisi hiyo Bi. Julieth Magambo (Kushoto) wakishiriki Misa ya Kuuga mwili wa aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI Mhe Jenista Mhagama Leo tarehe 13/12/2025 katika Parokia ya Kiwanja Cha Ndege Jijini Dodoma.

 Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Mussa Magufuli akiwasili katika Kanisa Katoliki parokia ya kiwanja cha ndege Jijini Dodoma leo tarehe 13/12/2025 kwa ajili ya kushiriki misa ya kuuaga mwili wa Marehemu Mhe Jenista Mwagama ambaye aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI.

Mkurugenzi Msaidizi Utawala Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bi.Nyasinde Mukono akiwasili kwa ajili ya kushiriki Ibada Maalum ya kuuaga mwili wa aliyewahi kuwa Waziri wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI Marehemu Jenista Mhagama katika Parokia ya Kiwanja cha Ndege Jijini Dodoma Disemba 13, 2025.




WAZIRI KIKWETE AAHIDI USHIRIKIANO KWA WATUMISHI WA WAKALA YA NDEGE ZA SERIKALI

Na. Mwandishi Wetu-Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete ameipongeza Bodi, Menejimenti na Watumishi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) kwa kuongoza na kusimamia Ndege za Serikali kwa weledi na  ufanisi mkubwa.

Waziri Kikwete amesema hayo Desemba 12, 2025 jijini Dar es salaam wakati alipotembelea ofisi ya Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) kwa lengo la kujitambulisha.


“Ninaipongeza Bodi kwa kuendelea kuwa washauri wazuri na kufanya uendelevu wa Wakala, binafsi ninaridhika na utendaji kazi wake. Pia Nitumie fursa hii kuwapongeza watumishi wote kwa ustadi wenu mkubwa wa kusimamia Ndege za Serikali, mimi na Naibu Waziri wa ofisi yangu Mhe. Regina Qwaray tunawahakikishia ushirikiano wa dhati wakati wote wa uongozi wetu” alisema Mhe. Kikwete.

Aidha, Mhe. Kikwete amewapongeza kwa kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi ambao unaonekana kuridhisha viongozi wanawahudumia. Hivyo, ametoa rai pia kwa watumishi hao kumpa ushirikiano Naibu Waziri Mhe. Regina Qwaray kwa kuwa anamfahamu uwezo wake katika kazi na atasaidia kuongeza ufanisi mara dufu.

Vile vile Mhe. Kikwete amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumuamini na kumpa nafasi ya kuongoza Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambapo TGFA ni moja ya taasisi zilizo chini ya Ofisi hiyo.

Naye, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray ameahidi kutoa ushirikiano katika kutekeleza majukumu ya taasisi hiyo muhimu katika Taifa.

“Leo tumekuja kujitambulisha ili tupate kufahamiana kwa kuwa sisi ndio tutafanya kazi pamoja, naomba tuendelee kuwa na ari ile ile ya kufanya kazi kwa ushirikiano ili tuweze kufanikiwa” alisema Mhe. Qwaray.

Awali, Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Ndege za Serikali Capt. Budodi Nicholaus Budodi alisema kuwa Wakala inaendelea vizuri kusimamia miradi mbalimbali inayoendelea katika ofisi hiyo.

Vile vile, kwa niaba ya taasisi ameahidi kuendelea kuwa wasikivu katika maelekezo wanapata  kutoka kwa viongozi na kutekeleza kwa wakati na kwa ufanisi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Menejimenti na Watumishi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) wakati alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam.

 


Mkurugenzi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA)Capt. Budodi Budodi (aliyesimama) akisoma taarifa ya taasisi hiyo pamoja na maendeleo ya ujenzi wa Karakana ya Wakala ya Ndege za Serikali wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipotembelea taasisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam.


Sehemu ya Watumishi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam.


Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi Idrissa Mshoro (kushoto) akifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wapili kutoka kushoto) akielekea kukagua maendeleo ya ujenzi wa Karakana ya Wakala wa Ndege za Serikali jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Naibu Waziri wa Ofisi yake Mhe. Regina Qwaray. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA)Capt. Budodi Budodi


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wakwanza kushoto) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA)Capt. Budodi Budodi (wakwanza kulia). Wa pili kutoka kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray na wa pili kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi Idrissa Mshoro.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo kabla ya kuzungumza na Menejimenti na Watumishi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) wakati alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Regina Qwaray.

 


Mkurugenzi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA)Capt. Budodi Budodi (wakwanza kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wapili kutoka kushoto). Wa pili kutoka kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiwasili katika ofisi ya Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) wakati alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiwa katika Ukumbi wa Mkutano wa Ofisi ya Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) kabla ya kuzungumza na Menejimenti na Watumishi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) wakati alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Regina Qwaray.

Sehemu ya Menejimenti ya Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam.


Sehemu ya Watumishi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wa kwanza kulia) akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi Idrissa Mshoro. Katikati ni Mkurugenzi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA)Capt. Budodi Budodi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Viongozi, Watendaji na Watumishi wa Wakala ya Ndege za Serikali baada ya kuwasili katika ofisi hiyo kwa lengo la kujitambulisha jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi na Menejimenti ya Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) baada ya kuzungumza nao alipokwenda kujitambulisha katika ofisi hiyo jijini Dar es Salaam 


 

 

Friday, December 12, 2025

SERIKALI KUJENGA UTUMISHI WA UMMA WENYE UFANISI, UWAJIBIKAJI NA KUONGEZA FURSA ZA AJIRA NA USTAWI WA VIJANA

Na Veonica Mwafisi-Dar es Salaam

Tarehe 12 Disemba, 2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Serikali kupitia Ofisi yake inaonesha dhamira thabiti ya kujenga Utumishi wa Umma wenye ufanisi, uwajibikaji na unaozingatia misingi ya utawala bora ili kwenda sambamba na matarajio ya Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.

Waziri Kikwete amesema hayo wakati wa Mkutano wake na Waandishi wa Habari uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam Desemba 12, 2025. Mkutano huo ulilenga kutoa taarifa ya namna Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora inavyotekeleza wajibu wake kwa Taasisi za umma, Watumishi wa Umma na Wananchi kwa jumla.

Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, dhamira hiyo imeweka vipaumbele ambavyo ni kuongeza fursa za ajira na ustawi wa vijana wa kitanzania, maboresho ya mifumo ya ajira, utoaji wa huduma, mafunzo ya kujenga uwezo, usimamizi wa rasilimaliwatu pamoja na kuimarisha mifumo ya mawasiliano kati ya Serikali na wananchi.

Mhe. Kikwete alibainisha kuwa Serikali inaendelea kuhakikisha nafasi za ajira katika Utumishi wa Umma zinakuwa za wazi na ushindani kupitia Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS) ili kuwajengea Watanzania imani na uaminifu kwa Serikali yao kwa ustawi wa Taifa.

Vile vile, Mhe. Kikwete amesema, kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 imeelekeza Sekta ya kipaumbele iwe na uwezo wa kuzalisha ajira na kuongeza fursa ya ajira kwa vijana, kuongeza kipato kwa wananchi na kupunguza umaskini kwa kuzingatia viwango vya juu vya weledi unaopatikana na kufuata misingi ya haki, umahiri na utendaji bora.

Aidha, Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, katika kufanikisha maelekezo ya Dira 2050, kupitia Serikali kwa mwaka wa Fedha 2025/26 kibali cha nafasi 41,500 za ajira zikiwemo nafasi 12,000 za ajira ambazo ni ahadi ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoahidi kutoa nafasi 5,000 za kada za Afya na nafasi 7,000 za Walimu wa Masomo ya Sayansi na Hisabati ambazo ni uzalishaji wa ajira zilizo rasmi ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani.

Mhe. Kikwete amesema kuwa, ili kuhakikisha usaili unafanyika kwa wakati na kwa lengo la kuongeza ufanisi, usaili wa mchujo wa nafasi hizo utafanyika kwa kutumia mfumo wa kieletroniki uitwao “Online Aptitude Test (OATS)” na utafanyika katika vituo mbalimbali kama vile Taasisi za Elimu ya Juu, Vyuo vya Mafunzo ya Ufundi na Ufundi Stadi (VETA) na Shule za Sekondari zenye maabara za Komputa zinazopatikana katika mikoa yote na Vituo mahsusi kwa Unguja na Pemba.

“Mhe. Rais Dkt. Samia aliahidi baada ya kuingia madarakani atatoa nafasi 5,000 za kada za Afya na nafasi 7,000 za Walimu ndani ya siku 100 na tayari nafasi za ajira 12,000 zimeshatangazwa na waombaji wenye sifa wameitwa kwenye usaili utakaofanyika kuanzia tarehe 13 Desemba, 2025 katika mikoa yote Tanzania Bara na Vituo mahsusi kwa Unguja na Pemba,” Amefafanua Mhe. Kikwete.

Pia, Waziri huyo aliwaomba wandishi wa habari kuendelea kuwahabarisha na kuwaelimisha Watanzania hususan vijana, kutambua fursa zilizopo na kuzitumia kwa manufaa ya taifa. Utambuzi huo unaifanya Serikali kuendelea na jitihada zake za kukuza ujuzi, kuhimiza maadili, kupanua fursa za makazi bora na kuandaa vijana wa Kitanzania ili kukabiliana na uchumi wa kidijiti.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa Mkutano wake na Waandishi hao uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam uliolenga kutoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake.  


Sehemu ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo kwenye Mkutano wake na Waandishi hao uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam. Wa kwanza kulia waliokaa ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi hiyo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wanne kutoka kushoto) akimsikiliza, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Maelezo, Bi. Zamaradi Kawawa (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri huyo kuzungumza na Waandishi wa Habari kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI. Watatu kutoka kushoto ni Naibu Waziri, wa Ofisi yake Mhe. Regina Qwaray na wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi hiyo. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiteta jambo na Naibu Waziri wa Ofisi yake Mhe. Regina Qwaray (kushoto) kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Waziri huyo na Waandishi wa Habari uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam kwa lengo la kutoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake.  


Mwandishi wa Habari kutoka Kituo cha Habari Azam Tv, Bi. Sheila Mkumba (aliyeshika kipaza sauti) akiuliza swali kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa Mkutano wa Waziri huyo na Waandishi wa Habari uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam kwa lengo la kutoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake.  


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiwa na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Bw. Mick Kiliba (kulia) kabla ya Waziri huyo kuzungumza na Waandishi wa Habari wakati wa Mkutano wake na Waandishi hao uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam uliolenga kutoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake.  


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyesimama kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa Mkutano wake na Waandishi hao uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam uliolenga kutoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake.  Wa pili kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Ofisi yake Mhe. Regina Qwaray. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi hiyo.


Mwandishi wa Habari kutoka Kituo cha Habari Radio Maria, Bw. Martin Joseph (aliyeshika kipaza sauti) akiuliza swali kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa Mkutano wa Waziri huyo na Waandishi wa Habari uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam kwa lengo la kutoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake.  


Sehemu ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo kwenye Mkutano wake na Waandishi hao uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi yake.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (watatu kutoka kushoto) akifuatilia Mkutano wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) na Waandishi wa Habari uliofanyika katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es salaam uliolenga kutoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake. 

 



 

 

Thursday, December 11, 2025

MHE. RIDHIWANI KIKWETE AWAKUMBUSHA SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA KUZINGATIA WAJIBU WAO WA KUSIMAMIA MAADILI BILA UPENDELEO

 Na Antonia Mbwambo na Eric Amani-Dodoma

Tarehe 11 Disemba, 2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ametoa wito kwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa weledi, uadilifu na bila upendeleo kwa kiongozi yeyote.

Akizungumza wakati akimkaribisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mwigulu Nchemba kwa ajili ya kuzungumza na watendaji wa Sekretarieti hiyo, Mhe. Kikwete amesisitiza umuhimu wa chombo hicho katika kusimamia maadili kwa kuzingatia misingi ya sheria, uwazi, ukweli na usawa, ili kuendelea kujenga taswira njema ya utumishi wa umma nchini.

Ameeleza kuwa viongozi wa umma wana wajibu mkubwa kwa jamii, hivyo ni muhimu Sekretarieti hiyo kutekeleza dhima yake ya kisheria ya kuhakikisha viongozi wote wanazingatia miiko na maadili katika kutekeleza majukumu yao.

“Hatuwezi kuwa na Serikali ambayo viongozi wanalalamikiwa kwamba ni wapotofu wa Maadili na sisi kama chombo cha kusimamia Maadili ya Viongozi wa Umma tumekaa kimya” Waziri Kikwete alisema.

Aidha, ametoa rai kwa watumishi wa Sekretarieti ya Maadili kuimarisha ushirikiano, kuendesha uchunguzi kwa haki bila upendeleo na kutoa elimu ya kutosha kuhusu maadili kwa viongozi wa umma na wananchi kwa ujumla.

Kwa upande wao, watendaji wa Sekretarieti hiyo wamemhakikishia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI Mhe. Ridhiwani Kikwete kuwa wataendelea kufanya kazi kwa kuzingatia uwajibikaji, uadilifu na weledi ili kuimarisha imani ya wananchi katika mifumo ya utawala bora


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mwigulu Nchemba (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali pamoja na menejimenti na watumishi wa Sekretariati ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa ziara yake ya  kikazi aliyoifanya katika Ofisi hiyo leo tarehe Disemba 11, 2025 Jijini Dodoma. Kulia kwake ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete na Kushoto ni Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Sekretarieti ya Maadili Jaji Sivangilwa Mwangesi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiteta jambo na Katibu Mkuu Ikulu Bw. Mululi Mahendeka wakati wakimsubiria Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Mwigulu Nchemba awasili katika Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambapo alikuwa na ziara ya kikazi leo Disemba 11, 2025 jijini Dodoma.

Waziri Mkuu  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Mwigulu Nchemba (kulia) akiteta jambo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) baada ya kuwasili katika Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambapo alikuwa na ziara ya kikazi leo Disemba 11, 2025.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Kamishna wa Maadili,Jaji Mstaafu Bw. Sivangilwa Mwangesi (katikati) pamoja na Katibu Mkuu Ikulu Bw. Mululi Mahendeka (kulia) wakati wakimsubiria Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba kuwasili katika Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa ziara ya kikazi iliyofanyika leo Disemba 11, 2025 jijini Dodoma.

1.  Waziri Mkuu  wa Jamhurin ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Mwigulu Nchemba akiwasili katika Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambapo alikuwa na ziara ya kikazi leo Disemba 11, 2025

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mwigulu Nchemba akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambapo alikuwa na ziara ya kikazi leo Disemba 11, 2025 jijini Dodoma.Kulia kwake ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete,wengine ni Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Sekretarieti ya Maadili Jaji Sivangilwa Mwangesi (wa tatu kulia) na Katibu Mkuu Ikulu Bw. Mululi Mahendeka (wa kwanza kushoto).


Menejimenti na Watumishi wa Sekretarieti ya Maadili wakimsikiliza Waziri Mkuu  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Mwigulu Nchemba (hayupo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi hiyo leo Disemba 11, 2025 jijini Dodoma.


Menejimenti na Watumishi wa Sekretarieti ya Maadili wakimsikiliza Waziri Mkuu  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Mwigulu Nchemba (hayupo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi hiyo leo Disemba 11, 2025 jijini Dodoma.

9(