Thursday, December 4, 2025
Tuesday, December 2, 2025
Monday, December 1, 2025
MAFUNZO
Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na mwezeshaji ikiwa ni sehemu ya Mafunzo ya kuwajengea watumishi hao uwezo wa kiutendaji ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalum la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma.
Sunday, November 30, 2025
TUJIKITE KUFUNDISHA KOZI ZITAKAZOENDA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAHITIMU NA WANANCHI-Mhe. Kikwete
Na. Eric Amani-Dar es Salaam
Tarehe
28 Novemba, 2025
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameielekeza Bodi ya Ushauri na Menejimenti ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kujikita zaidi katika kufundisha kozi zitakazoenda kutatua changamoto za wahitimu na wananchi kwa ujumla.
Waziri Kikwete ametoa maelekezo hayo leo tarehe 28 Novemba, 2025 kabla ya kuwatunuku wahitimu wa kozi mbalimbali katika mahafali ya 42 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Mhe. Kikwete amesema, Watanzania wanahitaji kupata elimu ya kuwasaidia katika maisha yao na sio ya kukaa na vyeti ndani. “Naielekeza Bodi na Menejimenti kuhakikisha Kozi tunazoanzisha zinaleta majawabu ya changamoto za Watanzania,” Mhe. Kikwete amesisitiza.
Mhe. Kikwete amesema anayo maswali ya msingi ya kujiuliza, akitolea mfano wa Kozi ya Makatibu Mahususi, je Kozi zilizotolewa kwa watumishi hawa zamani zinafanana na zinazotolewa sasa? Tumeshuhudia uvunjifu wa maadili kwa watumishi. Ni wajibu wetu kuhakikisha watumishi wanakuwa na uadilifu, tutengeneze Utumishi wa Umma wenye weledi. Je watumishi wa umma bado ni wazalendo? Ni majibu yanayopatikana kwa Menejimenti na Bodi ya Chuo hiki. Tuangalie Mitaala ili ijibu maswali yangu,” amesisitiza.
Aidha, ametoa wito kwa Wahitimu kuendelea kujifunza hata baada ya kuhitimu, kwani dunia ya leo inahitaji kujifunza maisha yote ili kuendelea kuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji yanayobadilika kila uchwao.
“Nawasihi mjiepushe na vitendo vyovyote vinavyoweza kuharibu taswira yenu na ya Utumishi wa Umma, kama vile rushwa, uzembe, ubaguzi, matumizi mabaya ya madaraka na kutowajibika. Badala yake, muwe mfano wa kuigwa katika weledi, uwajibikaji, uadilifu na kujituma kazini,” ameongeza
“Leo mmehitimu, na baadhi yenu kesho mnatarajiwa kuwa viongozi na watendaji katika sekta mbalimbali. Taifa linawategemea hivyo mtakapopata fursa ya kuajiriwa mkawe mabalozi wa Chuo cha Utumishi wa Umma kwa kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Maadili ya Utumishi wa Umma” amesema.
Mhe. Kikwete amesema ni matarajio ya Serikali kwamba Chuo hiki kitaendelea kuwa chachu ya mabadiliko katika utumishi wa umma kupitia mafunzo ya muda mfupi, tafiti zinazolenga kutatua changamoto mbalimbali katika utumishi wa umma pamoja na ushauri wa kitaalamu zinazotolewa kwa taasisi za umma na sekta binafsi. Serikali itaendelea kushirikiana na uongozi wa chuo kuhakikisha kuwa bajeti ya maendeleo inaendelea kutengwa mwaka hadi mwaka.
Akiwasilisha hotuba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kabla ya kumkaribisha Waziri Kikwete kuzungumza na wahitimu hao, Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Nolasco Kipanda amewapongeza wadau wote waliofanikisha Chuo hiki kuendelea na kuwapongeza pia wahitimu kwa kutunukiwa vyeti na kuwasisitiza kuitumia vyema elimu waliyoipata.
Amesema Serikali imeendelea
kukijengea uwezo Chuo cha Utumishi wa Umma kupitia miradi ya kimkakati yenye
tija.
Kufuatia hotuba hiyo ya
Katibu Mkuu, Dkt. Turuka, amepongezwa kwa kuteuliwa kwa mara nyingine kuwa
Mwenyekiti wa Bodi hiyo kwani inaonyesha uongozi wake mahiri, uadilifu na
usimamizi madhubuti aliouonyesha.
Naye Mwenyekiti wa Bodi
ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Frolens Turuka
akizungumza kwa niaba ya Bodi hiyo na Menejimenti ya TPSC, amewapongeza wahitimu
wote waliomaliza salama na kutunukiwa vyeti na kutoa wito wa kutumia vema
maarifa waliyoyapata wakati wote wa masomo yao kwa manufaa yao na taifa kwa
ujumla.
Amesema wao kama Bodi
ya Ushauri ya Chuo hicho wataendelea kushauri ipasavyo ili kujenga uwezo wa Sekta
ya Umma kulingana na mabadiliko ya teknolojia na kutekeleza yale yanayopaswa
kufanywa katika Utumishi wa Umma.
Akiwasilisha taarifa ya utendaji wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Mtendaji Mkuu na Mkuu wa TPSC, Dkt. Ernest Mabonesho amesema jumla ya wahitimu 6956 kutoka katika kampasi zote sita za TPSC ambazo ni Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Tabora, Singida na Mbeya wametunukiwa vyeti katika ngazi ya shahada, stashahada na astashahada katika kozi mbalimbali.
Dkt. Mabonesho amesema Mahafali hayo ni miongoni mwa matukio muhimu yanayoashiria maendeleo ya chuo hicho ambacho tangu kilipoanza mpaka leo kinatimiza miaka 25. “Mhe. Mgeni Rasmi, kufanyika kwa mahafali ya leo sio tukio la kawaida tu bali ni maendeleo na uvumilivu tangu kuanzishwa kwake kama Wakala ya Serikali. Tulianza na Kampasi mbili lakini sasa ziko sita, jambo lililoongeza fursa za mafunzo kwa wahitaji kwani kozi pia zimeongezeka katika taaluma mbalimbali ikiwemo mafunzo kwa njia ya mtandao,” Dkt. Mabonesho ameongeza.
1. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiongea na wahitimu na wageni waalikwa wakati wa mahafali ya
42 ya Chuo cha Utumishi wa umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Kituo
cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) leo tarehe 28.11.2025 jijini
Dar es Salaam.
![]() |
1. Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw.
Nolasco Kipanda akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri Kikwete
kuzungumza na wahitimu na wageni waalikwa wakati wa
mahafali ya 42 ya Chuo cha Utumishi wa umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika
katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius
Nyerere (JNICC) leo tarehe 28.11.2025 jijini Dar es Salaam. |

1. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiongoza maandamano ya wahitimu wa mahafali ya 42 ya
Chuo cha Utumishi wa umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Kituo
cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) leo tarehe 28.11.2025 jijini
Dar es Salaam.
1. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa zawadi kwa mmoja wa wahitimu waliofanya vizuri katika
masomo yao wakati wa mahafali ya 42 ya Chuo cha Utumishi wa umma Tanzania
(TPSC) yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano
cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) tarehe 28.11.2025 jijini Dar es Salaam.
1. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Serikali kabla ya
tamko la kufungua mahafali ya 42 ya Chuo cha Utumishi wa umma Tanzania (TPSC)
yaliyofanyika katika Kituo cha
Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) leo tarehe 28.11.2025 jijini
Dar es Salaam.
1. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiteta na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo
(kulia) na Mwenyekiti
wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Frolens Turuka (kushoto) kabla ya kuanza maandamano ya
wahitimu kwenye mahafali ya 42 ya Chuo cha Utumishi wa umma Tanzania
(TPSC) yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) leo tarehe
28.11.2025 jijini Dar es Salaam.
Saturday, November 29, 2025
Friday, November 28, 2025
Thursday, November 27, 2025
WAZIRI KIKWETE AWATAKA TPSC KUFANYA TAFITI ZITAKAZOSAIDIA KUBORESHA UTUMISHI WA UMMA NCHINI
1. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Menejimenti ya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakati wa kikao kazi chake na Menejimenti hiyo
leo tarehe 27.11.2025 jijini Dar es Salaam.
![]() |
1. Mwakilishi
wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Nolasco Kipanda akitoa neno la utangulizi kabla ya
kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
kuzungumza na Menejimenti ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC)
wakati wa ziara ya kikazi ya Mhe. Kikwete katika taasisi hiyo leo jijini Dar es
Salaam. |
![]() |
. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) mara baada ya kikao kazi chake na Menejimenti hiyo leo tarehe 27.11.2025 jijini Dar es Salaam.
1
Na Eric Amani-Dar es Salaam
Tarehe 27 Novemba, 2025
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameitaka Menejimenti
ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kufanya tafiti zitakazosaidia
kuboresha Utumishi wa Umma nchini kwa ustawi wa taifa.
Mhe. Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 27 Novemba, 2025 alipokuwa akizungumza na Menejimenti ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Chuo hicho jijini Dar es Salaam.
Amesema ni jukumu la TPSC kueleza ukweli kwa kufanya tafiti, kwani wanao wajibu wa kuhakikisha Utumishi wa Umma unakaa vizuri, “tuambieni yale mnayofikiri ni vema yakafanyika ili kuwa na Utumishi wa Umma bora, hatuwezi kufanikiwa kama Chuo hiki kitashindwa kutuambia wapi kuna tatizo,” amesisitiza.
“Tufanye tafiti tujiulize, kuna vitu gani tunatakiwa kuviboresha, lazima tujadili Utumishi wa Umma kwa upana wake. Huwezi kuwa Mtumishi wa Umma na matendo yako hayafanani na Utumishi wa Umma Mhe. Kikwete amesema.
Aidha, Mhe. Kikwete ameipongeza taasisi hiyo kwa kufanya kazi nzuri na kuisisitiza kuendelea kutoa mafunzo elekezi na kujitangaza zaidi ili Chuo hicho kifahamike kwa wananchi na kutoa fursa ya kujiunga huku akiwataka kujielekeze zaidi kwenye Dira waka ya Maendeleo ya Taifa 2050 katika utekelezaji wa majukumu yao.
Ameitaka taasisi hiyo kumshirikisha pale wanapokwama kutekeleza majukumu yao ili aone namna ya kuwezesha. “Nishirikisheni pale mnapokwana ili tusaidiane namna bora ya kufanya, kwangu hakuna jibu la hapana, kuna haiwezekani lakini tukifanya hivi itawezekana. Tupeane ushirikiano mkubwa kwani ndio utakaotusaidia kusonga mbele.” Mhe. Kikwete ameongeza.
Naye Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Nolasco Kipanda amesema Katibu Mkuu-UTUMISHI anafurahia kuona Waziri Kikwete akifanya ziara katika taasisi zilizo chini ya Ofisi yake, kwani anaamini anaweka msingi katika maeneo mbalimbali ya kuboresha utendaji.
Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Mkuu wa Chuo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Ernest Mabonesho ametoa shukrani kwa Waziri Kikwete kwa kutenga muda wake na kuwatembelea katika chuo chao na kuahidi ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake.
“TUWAELEZE WANANCHI MAFANIKIO YALIYOPATIKANA, YALIYOFANYWA NA SERIKALI NI MENGI SANA”-Mhe. Kikwete
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma
|
na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani
Kikwete akisisitiza jambo wakati wa kikao kazi chake na Menejimenti ya
Watumishi Housing Investments (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi katika
taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam. |
![]() |
Kaimu Mkurugenzi wa Watumishi Housing
Investments (WHI) Bw. Sephania Solomon akiwasilisha taarifa
ya utekelezaji wa majukumu ya Taasisi hiyo wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete katika taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam. |
![]() |
| Sehemu ya Menejimenti ya Watumishi Housing Investments wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza nao katika kikao kazi cha Waziri huyo na Menejimenti hiyo jijini Dar es Salaam. |
Na Eric Amani-Dar es Salaam
Tarehe 27 Novemba, 2025
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
ameitaka Menejimenti ya Watumishi Housing Investments (WHI) kuwaeleza wananchi
mafanikio yaliyopatikana kwani Serikali imekuwa ikifanya mambo mengi na makubwa lakini wananchi hawajui.
“Mnafanya kazi nzuri sana ya ujenzi
wa makazi ya Watumishi wa Umma na Wananchi na uwekezaji kupitia Faida Fund,
lakini wananchi hawajui, wa kuwaambia wananchi ni sisi, tuwaambie, tuangalie
namna ya kutangaza ili wajue” Mhe. Kikwete amesisitiza.
Mhe. Kikwete ametoa maelekezo hayo
leo tarehe 27.11. 2025 akiwa kwenye mwendelezo wa ziara ya kikazi katika
taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora ambapo leo ametembelea Watumishi Housing Investments (WHI) jijini
Dar es Salaam.
Amesema suala la ujenzi wa makazi ya
Watumishi wa Umma ni muhimu ili waweze kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia
wananchi kwa utulivu na kuweza kuwabakisha watumishi hao katika maeneo yao ya
kazi kwani kila mtu anatamani kuishi kwenye mazingira rafiki.
Amesema pamoja na ujenzi wa makazi ya
Watumishi, WHI inapaswa kutumia teknolojia ya ujenzi wa nyumba za gharama nafuu
na zenye ubora ili Watumishi waweze kununua na kuongeza kuwa kipaumbele kiwe kwenye
mikoa ya pembezoni.
“Simamieni msingi ya uanzishwaji wa
Taasisi hii wa kujenga nyumba za watumishi kwa gharama nafuu, tufikirie nje ya
boksi ili kupata fedha za kujenga nyumba za kutosha na kufikia malengo ya
Serikali ya utoaji wa huduma bora kwa wananchi badala ya kutegemea zaidi
Serikali, bajeti ya
Serikali iwe kichocheo tu,” Mhe.
Kikwete amesisitiza. “Mmeyafanya mengi yenye ubunifu, tunaona, mnastahili
pongezi kwa mliyoyafanya, kwa mfano kuanzisha Mfuko wa Uwekezaji (Faida Fund)
ni ubunifu mzuri, tuendelee kusimamia msingi wa uanzishwaji wa mfuko huu, tujitahidi
kutoa elimu ili Watumishi wa Umma wengi zaidi na wananchi wawekeze katika Mfuko
huu kwa maisha yao ya sasa na ya baadae pindi wanapohitimisha utumishi wao,”
ameongeza.
Amesema ni matamanio ya Rais Mhe.
Dkt. Samia Suluhu Hassan kuona Watumishi wa Umma wanaishi kwenye mazingira
mazuri kama ambavyo amekuwa akisisitiza anataka watumishi waishi vizuri ili
kuweza kuwahudumia wananchi kwa ubora, “tutafsiri maono yake kwa kuyafanyia kazi,”
ameongeza.
Ametoa mfano kuwa WHI inaweza kuingia
mkataba wa ujenzi kwa kutumia Halmashauri zenye makusanyo makubwa ya mapato na
kujenga nyumba za watumishi, “angalieni Halmashauri inaweza kuchangia kiasi
gani na ninyi kiasi gani maana Halmashauri hawawezi kujenga nyumba, muingie katika
makubaliano kuona namna gani mnaweza kutekeleza mpango wenu.” Amesisitiza.
Mhe. Kikwete amesema ni wakati sasa
wa kuambiana ukweli na sio kuoneeana aibu, “nimeletwa kuja kusaidiana nanyi ili
pale mnapokwama tusonge mbele, ndio jukumu lililonileta hapa, tunatamani kuona
mabadiliko yanaonekana, tuongeze kasi ya wawekezaji katika Mfuko huu wa Faida Fund
kwa kujitangaza zaidi,” amesisitiza.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu
Mkuu-UTUMISHI, Bw. Nolasco Kipanda, akitoa neno la utangulizi kabla ya
kumkaribisha Waziri kuzungumza na Menejimenti ya WHI amesema kitendo cha Waziri
kufanya ziara katika taasisi zilizo chini ya Ofisi yake ni fursa kubwa kwa Watendaji
wa taasisi hizo kuboresha utendaji.
“Mhe. Waziri amerudi kwa kofia
nyingine ya juu zaidi hivyo, kutembelea taasisi zilizo chini ya Ofisi yake ni
fundisho kwa Viongozi wa Taasisi na hata kwetu sote kwani tunapata fursa ya
kusikiliza matamanio yake ili kuona namna bora ya kufanya vizuri zaidi katika
utekelezaji wa majukumu yetu kwa ustawi wa taifa.” Bw. Kipanda ameongeza.
Amesema kila anachozungumza Mhe.
Waziri kinagusa Watumishi wa Umma na wananchi akitolea mfano wa ujenzi wa
makazi ya watumishi na uwekezaji kupitia Mfuko wa Faida Fund kuwa ni kazi yake
ya kisera.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji,
Kaimu Mkurugenzi wa Watumishi Housing Investments (WHI) Bw. Sephania Solomon
amemshukuru Mhe. Kikwete kwa ushauri na maelekezo aliyoyatoa ambapo ameahidi kuyafanyia
kazi.
KIKAO KAZI CHA MAAFISA SHERIA NA MAAFISA UTUMISHI KILICHOLENGA KUBADILISHANA UZOEFU JUU YA CHANGAMOTO ZA UTEKELEZAJI WA SHERIA YA UTUMISHI WA UMMA SURA 298 NA KANUNI ZAKE
Mwenyekiti
wa kikao kazi cha kutambua
changamoto za utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma ambaye ni Mkuu wa Idara
ya Utumishi na Utawala kutoka halmashauri ya wilaya ya Ludewa Bw. Oscar Semtengu
akitoa neno la shukrani baada ya kumalizika kwa kikao hicho kilichofanyika katika
ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
Sehemu ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga Kutambua
changamoto za utekelezaji wa Sheria ya Utumishi ya Umma na kanuni zake wakifuatilia mada mbalimbali
zilizikuwa zikitolewa wakati wa majadiliano ya kikao hicho katika Ofisi ya Mkuu
wa Mkoa wa Iringa kilichofanyika tarehe 27&28 Novemba,2025 katika Ofisi ya
Mkuu wa Mkoa Iringa.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utawala wa Usimamizi wa Utumishi wa Umma Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi Verediana Ngahega akitoa maelekezo mafupi juu ya ushughulikiaji wa Uhamisho (E transfer), Upandishwaji Vyeo na Ubadilishwaji Kada katika Utumishi wa Umma wakati wa Kikao kazi cha kutambua changamoto za utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma kilichofanyika Mkoani Iringa tarehe 27&28 Novemba,2025.
Mkurugenzi
Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini Ofisi ya Rais Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Senzota akitoa maelezo mafupi kuhusu
ushughulikiaji wa Malimbikizo ya Mishahara kwa watumishi wa Umma waliopandishwa
Vyeo, waliofukuzwa kazi na kurejeshwa katika Utumishi wa Umma na Mamlaka zao za
Rufaa katika Kikao kazi cha kutambua changamoto za
utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma kilichofanyika Mkoani Iringa tarehe
27&28 Novemba,2025.
Sehemu
ya Wakurugenzi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na
viongozi mbalimbali wakifuatilia mada mbabalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshajiwakati wa Kikao kazi cha kutambua changamoto za utekelezaji
wa Sheria ya Utumishi wa Umma kilichofanyika tarehe 27&28 Novemba,2025 katika
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.
Mshiriki
wa kikao kazi cha Maafisa Sheria na Maafisa Utumishi ambaye ni Meneja anayesimamia
mafao Mfuko wa Mafao wa PSSF Bw. James Oigo akiwasilisha mada ihusuyo ushughulikiaji
na ulipaji wa mafao kwa Watumishi wa Umma baada ya kustaafu wakati wa Kikao kazi
cha kutambua changamoto za utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma kilichofanyika
tarehe 27&28 Novemba,2025 katika Ofisi ya Mkuu
wa Mkoa Iringa.
Mgeni Rasmi ambaye ni Mkurugenzi Idara ya Usimamizi wa Maadili Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Felista Shuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa Sheria na Maafisa Utumishi wakati wa Kikao kazi cha kutambua changamoto za utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma kilichofanyika tarehe 27&28 Novemba,2025 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.
Mkurugenzi
Idara ya Usimamizi wa Maadili Ofisi ya
Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Felista
Shuli akitoa neno la kufunga
kikao kazi cha Kutambua changamoto
za utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na kanuni zake kwa niaba ya Katibu Mkuu wa
Ofisi hiyo Bw Juma Mkomi kilichofanyika Mkoani Iringa tarehe 27&28 Novemba ,2025.
Mgeni
Rasmi ambaye ni Mkurugenzi Idara ya Usimamizi wa Maadili Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Felista Shuli akiwa katika
picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa Sheria na Maafisa Utumishi wakati wa Kikao kazi cha kutambua changamoto za utekelezaji
wa Sheria ya Utumishi wa Umma kilichofanyika tarehe 27&28 Novemba,2025 katika
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi Hilda Kabissa akifafanua jambo kwa Maafisa Sheria na Maafisa Utumishi wakati wakijadili mada mbalimbali katika Kikao kazi cha kutambua changamoto za utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma kilichofanyika tarehe 27&28 Novemba,2025 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.
Mgeni
Rasmi ambaye ni Mkurugenzi Idara ya Usimamizi wa Maadili Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Felista Shuli akiwa katika
picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa Sheria na Maafisa Utumishi wakati wa Kikao kazi cha kutambua changamoto za utekelezaji
wa Sheria ya Utumishi wa Umma kilichofanyika tarehe 27&28 Novemba,2025 katika
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.
Mshiriki wa kikao kazi cha Maafisa Sheria na Maafisa Utumishi ambaye ni Afisa Mafao Mwandamizi Bw. Emmanuel Kalumuna kutoka Mfuko wa Mafao wa NSSF akiwasilisha mada ihusuyo ushughulikiaji na ulipaji wa mafao kwa Watumishi wa Umma baada ya kustaafu wakati wa Kikao kazi cha kutambua changamoto za utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma kilichofanyika tarehe 27&28 Novemba,2025 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa






















