Thursday, March 13, 2025

NAIBU KATIBU MKUU XAVIER DAUDI AONGOZA KIKAO CHA UGENI KUTOKA TUME YA UTUMISHI WA UMMA MALAWI


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (wa kwanza kulia) akimsikiliza Katibu Mkuu wa Tume ya Utumishi wa Umma Malawi, Bi. Irene Chikapa (wa kwanza kushoto) wakati akielezea malengo ya kutembelea Ofisi ya Rais-UTUMISHI.


Ugeni kutoka Tume ya Utumishi wa Umma Malawi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha ofisi hiyo waliofika kwa lengo la kujifunza Mifumo ya Kielektroniki iliyopo katika Utumishi wa Umma kuhusu ajira na taarifa za kiutumishi.


Baadhi ya Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha ofisi hiyo na ugeni kutoka Tume ya Utumishi wa Umma Malawi waliofika kwa lengo la kujifunza Mifumo ya Kielektroniki iliyopo katika Utumishi wa Umma kuhusu ajira na taarifa za kiutumishi.

Baadhi ya Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Ugeni kutoka Tume ya Utumishi wa Umma Malawi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha ofisi hiyo na ugeni huo uliofika kwa lengo la kujifunza Mifumo ya Kielektroniki iliyopo katika Utumishi wa Umma kuhusu ajira na taarifa za kiutumishi.

 




Wednesday, March 12, 2025

SIMBACHAWENE NA MKENDA WAKUTANA NA VIONGOZI WA NETO

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amesema Serikali itaunda timu ya wataalam itakayojuisha Wizara tano (5) ili kuchambua Makala ya “Non-Employed Teachers Organisation-NETO)” wenye umoja wao kupitia mitandao ya kijamii ili maoni yao yatumike kwa maendeleo ya taifa.

Waziri Simbachawene amesema hayo leo wakati wa kikao kilichoshirikisha Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia na Viongozi wa NETO kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma.

“Ninamuelekeza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi kuunda timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Wizara ya Fedha ili kuchambua makala hiyo ili tuweze kutumia mapendekezo yao kupata suluhu ya upungufu wa ajira kwa walimu” alisema Mhe. Simbachawene.

Aidha, Mhe. Simbachawene amesema Serikali ina haki ya kumsikiliza kila mwananchi kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na kwa kuzingatia misingi ya 4R ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Simbachawene amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inazingatia misingi ya Falsafa ya 4R (Maridhiano, Ustahimilivu, Mabadiliko na Kujenga Upya), hivyo ujio wa viongozi na NETO na utayari wa viongozi wa Serikali kuwasikiliza viongozi hao ni jitihada madhubuti zinazosadifu uzingatiaji wa falsafa hiyo.

Naye, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda amesisitiza kuwa utaratibu wa usaili unaleta ushindani, haki na kuondoa mwanya wa upendeleo kwa wasailiwa.

“Mapendekezo yenu ni mazuri na sisi kama Serikali tunasubiri timu iliyotajwa na Mhe. Simbachawene ifanye kazi ya kupitia na kuchambua Makala hiyo na kisha kuleta ushauri wa namna bora ya kuboresha mchakato wa ajira za walimu” alisema Mhe. Mkenda.

Vilevile, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi amesema Ofisi yake iko tayari kuunda timu hiyo na itatoa taarifa ndani ya kipindi cha siku 30 hadi 45 zilizoelekezwa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza wakati wa kikao kilichoshirikisha Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Wizara ya Elimu na Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma.

Viongozi wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati akizungumza kwenye kikao kilichoshirikisha Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Wizara ya Elimu na Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma. Wa kwanza kushoto ni Naibu Kaibu Mkuu, Ofisi ya Rais-TAMISEMI anayeshughulikia Elimu Bw. Atupele Mwambene.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda (wa kwanza kushoto), Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mhe. Deus Sangu (katikati) na Naibu Kaibu Mkuu, Ofisi ya Rais-TAMISEMI anayeshughulikia Elimu Bw. Atupele Mwambene wakifuatilia kikao kilichoshirikisha ofisi hizo na Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Wajumbe wa Chama cha Walimu Wasio na Ajira (NETO) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati akizungumza kwenye kikao kilichoshirikisha Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Ofisi ya Rais-TAMISEMI na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia wakifuatilia kikao kilichoshirikisha ofisi hizo na Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wajumbe wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) baada ya kumaliza kikao kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiagana na Viongozi na Wajumbe wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) baada ya kumaliza kikao kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wajumbe wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) baada ya kumaliza kikao kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wajumbe wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira (NETO) baada ya kumaliza kikao kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.



Monday, March 10, 2025

SERIKALI IMEFANYA JITIHADA KUBWA KUWEZESHA WANAWAKE KUPIGA HATUA KIMAENDELEO

Na. Veronica Mwafisi-Dar es Salaam

Tarehe 10 Machi, 2025

Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera, Bi. Mwanaamani Mtoo amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya jitihada kubwa katika kuwawezesha wanawake kupiga hatua kimaendeleo.

Bi. Mtoo ameyasema hayo leo kwenye Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam.

Amesema uwezeshwaji wa wanawake umefanyika kwa ushirikiano wa Viongozi wa Serikali pamoja na wanawake na wanaume kwani hakuna maendeleo ya wanawake pasipokuwa na wanaume kama ambavyo Sera ya Menejimenti na Ajira ya Mwaka 2008 ilivyotanabaisha katika Sura ya 5 ambayo inazungumzia Anuai za Jamii katika Utumishi wa Umma ambao umeleta msukumo mpya wa ufanisi na tija kwenye utendaji kazi kwa kutumia ujuzi na vipaji walivyonavyo.

Aidha, Bi. Mtoo amesema kwenye Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 298 pamoja na Kanuni za Mwaka 2022 zimeelekeza uzingatiaji wa masuala ya kijinsia ambapo Ofisi hiyo imetoa Mwongozo wa Ujumuishwaji wa Jinsia unaopaswa kutumika wakati wa usimamizi wa rasilimaliwatu ikiwemo kwenye masuala ya usaili na michakato ya ajira ili kuhakikisha watumishi wanawake au kundi la jinsi yenye uwakilishi mdogo linapewa fursa katika nafasi za ajira kwa kuzingatia sifa na vigezo.

Mwongozo huu ni kielelezo tosha cha dhamira ya Serikali ya kuimarisha ujumuishwaji wa jinsia katika Utumishi wa Umma jambo ambalo ni muhimu katika kuboresha utendaji kazi serikalini unaoiwezesha Serikali kuimarisha uchumi wa nchi na utoaji wa huduma kwa wananchi wote.” Amesisitiza Bi. Mtoo.

Ameipongeza Wizara ya Elimu kwa kuleta mapinduzi kwenye Sekta ya Elimu ambayo kwa kiasi kikubwa imewezesha kuibua viongozi mbalimbali wakiwemo wanawake kujumuishwa na kuleta uwiano sawa wa jinsia.

Ameongeza kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa kutambua thamani ya mwanamke, inampongeza Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa masuala mbalimbali ya maendeleo katika taifa hili.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu, Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid Maulid amesema kongamano hilo limelenga kujadili mustakabali wa Mwanamke na Uongozi katika Elimu ambapo itawawezesha kupata maoni, ushauri na mapendekezo  yatakayoleta matokeo na mikakati itakayowezesha  kupiga hatua kubwa kwa maendeleo ya ustawi wa taifa.

Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo akichangia mada wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam. 


Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo akiwa katika kazi ya vikundi wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam. 


Mtendaji Mkuu, Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dr. Maulid Maulid akielezea malengo ya Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam. 


Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo (kulia) akizungumza jambo na Kiongozi wa Timu (Shule Bora) Bi. Virginie Briand (kushoto) na Bi. Zainab Dhanani (katikati) kwenye Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam.

Mtendaji Mkuu, Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dr. Maulid Maulid akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililolenga kujadili kuhusu Wanawake na Uongozi katika Elimu lililofanyika Ukumbi wa Mikutano Hoteli ya WhiteSands jijini Dar es Salaam.  Kushoto kwake ni Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera,Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo.

 

 

 



 

Saturday, March 8, 2025

WANAWAKE OFISI YA RAIS-UTUMISHI WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 2025

Na. Veronica Mwafisi-Arusha

Tarehe 08 Machi, 2025

Watumishi Wanawake kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wameshiriki kwa wingi kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani leo Machi 8, 2025 jijini Arusha ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wanawake ni jeshi kubwa ambalo likiwezeshwa katika masuala mbalimbali nchini huongeza chachu ya utendaji kazi kwa kuzingatia usawa wa kijinsia kwa kushirikiana na wanaume na kuleta maendeleo kwa ustawi wa taifa.

Katika kuadhimisha Siku hiyo, Wanawake wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI walipata fursa ya kishiriki kikamilifu maonesho kuanzia tarehe 01 Machi hadi 08 kwenye Kilele cha Maadhimisho hayo kwa kutoa huduma mbalimbali za Kiutumishi kwa Watumishi wa Umma na Wananchi.

Maadhimisho hayo kwa Mwaka huu yamefanyika Kitaifa Jijini Arusha katika Viwanja vya Amri Abeid Karume yaliyobeba kauli mbiu isemayo “Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji”.

Watumishi Wanawake wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa katika picha ya pamoja nje ya Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yaliyofanyika jijini Arusha leo tarehe 08 Machi, 2025 ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 


Watumishi Wanawake wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa katika maandamano ya kuingia Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yaliyofanyika jijini Arusha leo tarehe 08 Machi, 2025 ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 


Watumishi Wanawake wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa katika furaha nje ya Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yaliyofanyika jijini Arusha leo tarehe 08 Machi, 2024 ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 


Watumishi Wanawake wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa katika picha ya pamoja nje ya Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yaliyofanyika jijini Arusha leo tarehe 08 Machi, 2025 ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 


Watumishi Wanawake wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa katika furaha nje ya Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yaliyofanyika jijini Arusha leo tarehe 08 Machi, 2024 ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 


Watumishi Wanawake wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa katika picha ya pamoja kwenye Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yaliyofanyika jijini Arusha leo tarehe 08 Machi, 2025 ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 



WANAWAKE WATUMISHI WA UTUMISHI WAUNGANA NA WANAWAKE WENGINE MKOANI DODOMA KUADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Na. Lusungu Helela– Dodoma

 Watumishi Wanawake  wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  wameungana  na wanawake wengine  jijini Dodoma na Duniani kote  kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani  ambayo huadhimishwa Machi  08 kila mwaka.

Watumishi hao wameongozwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Ofisi hiyo,   sehemu ya Utawala, Bi Mwalibora Mwamtuya katika kuadhimisha Siku hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Chinangali kwa ngazi ya Mkoa,  jijini Dodoma.

Maadhimisho hayo Kitaifa yamefanyika  Jijini Arusha  ambapo Mgeni Rasmi alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni  ‘’ Wanawake  na Wasichana 2025: Tuimarishe  Haki, Usawa na Uwezeshaji" Lengo likiwa ni kuhamasisha jamii kukuza  Usawa, Haki na Uwezeshaji wa Wanawake  na Wasichana  kwa kuzingatia kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ili wajiamini, wajiandae na wajitokeze kugombea nafasi za uongozi.

Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma  na Utawala Bora  wakiwa wameshika bango la ofisi hiyo wakati wa maandamano ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali 
Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma  na Utawala Bora  wakiwa wameshika bango la ofisi hiyo wakati wa maandamano ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali 

Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi na Utawala Bora  wakiwa na wanawake wa  Wizara zingine wakiwa kwenye  maandamano wakitokea Viwanja vya "Nyerere Square"  ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali 

Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi na Utawala Bora  wakiwa wamejawa na furaha   wakati wa maandamano  ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali 


Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi na Utawala Bora  wakiwa wamejawa na furaha   wakati wa maandamano  ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali 

Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi na Utawala Bora  wakiwa na wanawake wa  Wizara zingine wakiwa kwenye  maandamano wakitokea Viwanja vya "Nyerere Square"  ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali 

 

Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi na Utawala Bora  wakiwa na wanawake wa  Wizara zingine wakiwa kwenye  maandamano wakitokea Viwanja vya "Nyerere Square"  ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali 

 

Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi na Utawala Bora  wakiwa wamejawa na furaha   wakati wa maandamano  ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali 
Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi na Utawala Bora  wakiwa wamejawa na furaha   wakati wa maandamano  ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Chinangali 

Baadhi ya Wanawake wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi na Utawala Bora  wakijipanga kuingia viwanja vya Chinangali ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika jijini Dodoma katika viwanja hivyo vya Chinangali




Friday, March 7, 2025

HABARI KATIKA PICHA-MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 2025


Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Anuai za Jamii, Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo (kulia) akimhudumia Mwananchi aliyefika katika banda la ofisi hiyo kwa ajili ya kupata huduma wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yanayoendelea katika Viwanja vya Shekh Amri Abeid Karume jijini Arusha.

Afisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Annajackline Muhuga (wa pili kutoka kushoto) akifafanua jambo kwa Mwananchi aliyetembelea banda la Ofisi hiyo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yanayoendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume jijini Arusha.


Maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakionesha bango la Mwongozo wa Mavazi kwa Utumishi wa Umma wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yanayoendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume jijini Arusha.


Mtumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Justina Diyabene akionesha huduma zinazotolewa katika banda la ofisi hiyo lililopo katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume wakati wa Maadhimisho ya Siku ya wanawake Duniani 2025 yanayoendelea jijini Arusha.


Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakiwa mbele ya banda la ofisi hiyo tayari kwa kuwahudumia Watumishi wa Umma na Wananchi katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume wakati wa Maadhimisho ya Siku ya wanawake Duniani 2025 yanayoendelea jijini Arusha.


Afisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Enasy Lwidiko (kulia) akimhudumia Mtumishi wa Umma aliyefika katika banda la ofisi hiyo kwa ajili ya kupata huduma za Kiutumishi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025 yanayoendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume jijini Arusha. 




Thursday, March 6, 2025

WAZIRI SIMBACHAWENE ASIFU USHIRIKIANO WA SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA NA IAA KUKUZA MAADILI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameipongeza Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma pamoja na Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA)  kwa kuanzisha ushirikiano katika mafunzo ambayo yatalenga kuwa sehemu ya mkakati wa kuhakikisha kuwa maadili na uwajibikaji wa viongozi wa umma yanakuwa dhahiri na yanaimarishwa kupitia elimu na utafiti. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Simbachawene amesema kuwa Mpango wa Taifa dhidi ya Rushwa na Kukuza Uadilifu ni dhamira ya dhati  ya Serikali ya kuhakikisha kuwa jamii inayojengwa inakuwa  na  maadili, uwajibikaji, na uwazi katika kuwahudumia wananchi.

Aidha, Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesisitiza mara kwa mara kuwa "Mapambano dhidi ya rushwa hayawezi kuwa kazi ya mtu mmoja au taasisi moja; ni jukumu letu sote kama Taifa. Hivyo,  nazipongeza kwa dhati taasisi hizi mbili". 
Awali,  Mkuu wa Chuo cha IAA  Prof. Eliamani Sedoyeka  alisema , elimu bila maadili ni hatari, na maadili bila elimu ni bure. 
Amefafanua kuwa elimu ya kitaaluma na maadili thabiti katika uongozi ni jambo lisiloepukika . ‘‘Taasisi za elimu ya juu zina wajibu wa kuhakikisha kuwa wanaowazalisha wanakuwa si tu wataalamu wa fani zao, bali pia viongozi wenye maadili mema na wenye kuzingatia misingi ya utawala bora’’


Amesema makubaliano hayo na Sekretarieti ya Maadili kwa viongozi wa Umma yamejikita katika kutoa mafunzo kwa makundi mbalimbali katika jamii. 
Pia, Prof. Sedoyeka, ameipongeza serikali kwa kuendelea kuweka msisitizo katika kukuza maadili ya viongozi wa umma huku akisema kuwa anaamini kwa pamoja, wataweza kujenga Tanzania yenye utawala bora na maendeleo endelevu.

Naye Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Sikalalilwa Mwangesii amesema maadili na uongozi bora ni jukumu la pamoja linalohitaji ushirikiano wa wadau wote, wakiwemo taasisi za umma, sekta binafsi, asasi za kiraia na mashirika ya kimataifa.

Mhe. Jaji (Mst) Mwangesi amesisitiza kuwa, kupitia ushirikiano huo wataweza kujenga mfumo imara wa maadili unaozingatia misingi ya haki, usawa, na utawala bora na sio tu kwa viongozi wa umma bali kwa watumishi wa umma wote kwani hata hao viongozi ni wale wanaotokea kwenye Utumishi wa Umma


Waziri   wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene,akikata utepe kuashiria uzinduzi wa  makubaliano ya ushirikiano kati ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma,akiwa na Kamishna   wa maadili, Jaji Mstaafu Sivangilwa Mwangesi,(Kulia) na Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka,(kushoto).

Waziri   wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene akimsikiliza Mkuu wa  Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Prof. Eliamani Sedoyeka,(kushoto) akiwa na  Kamishna   wa maadili, Jaji Mstaafu Sivangilwa Mwangesi,(Kulia) wakati wa hafla ya uzinduzi wa  makubaliano ya ushirikiano kati ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mhe. Simbachawene akizungumza  wakati wa hafla ya makubaliano ya ushirikiano katika ya  Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) pamoja na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa lengo la kuanzisha ushirikiano katika mafunzo ambayo yatalenga kuwa sehemu ya mkakati wa kuhakikisha kuwa maadili na uwajibikaji wa viongozi wa umma yanakuwa dhahiri na yanaimarishwa kupitia elimu na utafiti. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mhe. Simbachawene akisalimiana na Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka mara baada ya kuwasili kwenye  hafla ya makubaliano ya ushirikiano katika ya  Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) pamoja na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa lengo la kuanzisha ushirikiano katika mafunzo ambayo yatalenga kuwa sehemu ya mkakati wa kuhakikisha kuwa maadili na uwajibikaji wa viongozi wa umma yanakuwa dhahiri na yanaimarishwa kupitia elimu na utafiti. 

Sehemu ya washiriki wakisikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene,(hayupo pichani)   wakati wa uzinduzi wa  makubaliano ya ushirikiano kati ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma,hafla iliyofanyika leo Machi 6,2025 jijini Dodoma.
Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka,akizungumza  wakati wa uzinduzi wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma,hafla iliyofanyika leo Machi 6,2025 jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wakisikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene,(hayupo pichani)   wakati wa uzinduzi wa  makubaliano ya ushirikiano kati ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma,hafla iliyofanyika leo Machi 6,2025 jijini Dodoma.