Monday, February 10, 2025

MFUMO WA USHUGHULIKIAJI WA RUFAA NA MALALAMIKO UTAONGEZA UFANISI KATIKA UTOAJI HAKI KWENYE UTUMISHI WA UMMA-Mhe. Sangu

Na. Veronica Mwafisi

Tarehe 10 Februari, 2025-Morogoro

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu amesema mafunzo yanayotolewa kwa Washiriki kutoka Serikali Kuu zikiwemo (Wizara, Sekretarieti za Mikoa, Idara zinazojitegemea na Wakala za Serikali), Taasisi za Umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhusu Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko yataongeza ufanisi katika utoaji haki kwenye Utumishi wa Umma.

Mhe. Sangu amesema hayo leo wakati akifungua mafunzo ya Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma yanayofanyika Mkoani Morogoro.

Mhe. Sangu amesema kuwa, kutokana na Serikali kusisitiza matumizi ya mifumo kwenye utendaji wa shughuli zake, Tume ya Utumishi wa Umma, imejenga Mfumo wa kushughulikia Rufaa na Malalamiko kwa Watumishi wa Umma, Mamlaka za Rufaa, Mamlaka za Nidhamu na Waajiri kwa lengo la kutoa huduma bora ili kuendana na Serikali ya kidijitali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Sangu ameongeza kuwa mfumo huo utasaidia kupatikana kwa taarifa za hali ya Utumishi wa Umma kwa wakati na katika ubora unaotakiwa kulingana na uzito wa taarifa hizo.

Naibu Waziri Sangu amewasihi washiriki wa mafunzo hayo kutumia vyema Mfumo huo na kuhakikisha wanatuma taarifa sahihi Tume ya Utumishi wa Umma kwa lengo la kuchakatwa na kuwasilisha taarifa hizo kwa Mamlaka husika ili kuirahisishia Serikali kupanga masuala mbalimbali yanayohusu Utumishi wa Umma.

Aidha, Naibu Waziri Sangu amewataka Waajiri, Mamlaka za Ajira na Mamlaka za Nidhamu kuwasilisha vielelezo vya rufaa na malalamiko Tume ya Utumishi wa Umma kwa wakati kama Sheria inavyoelekeza pale zinapotakiwa kufanya hivyo.

Kwa Upande wake, Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma Mhe. Hamisa Kalombola (Jaji Mst), amesema kuwa Tume iliamua kujenga mifumo ya kielektroniki na kuendelea kutoa elimu ya kutumia mifumo hiyo kwa wadau wao ili kuondokana na baadhi ya changamoto ambazo zilikuwa zinakwamisha utendaji kazi wa namna ya kuitumia wakati wa uendeshaji wa mashauri na nidhamu hasa kwenye ushughulikiaji wa rufaa na malalamiko.

Awali, Kaimu Katibu, Tume ya Utumishi wa Umma Bw. John Mbisso alisema, mafunzo hayo yanafanyika ili kutekeleza Sheria ya Utumishi wa Umma ya kutoa miongozo na elimu ya masuala mbalimbali ya kiutumishi kwa lengo la kuboresha usimamizi wa Watumishi wa Umma.

Tume ya Utumishi wa Umma ni chombo rekebu chini ya Ofisi ya Rais  kilichoundwa kwa mujibu wa Kifungu cha 9(1) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298 [Marejeo ya Mwaka 2019].

Aidha, majukumu ya Tume yameainishwa katika Kifungu cha 10(1) cha Sheria hiyo ambapo baadhi ya majukumu yake ni pamoja na kutoa Miongozo, Uwezeshaji, Utafiti, kufuatilia Uzingatiaji katika Usimamizi wa Utumishi wa Umma na ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu akizungumza wakati akifungua mafunzo kuhusu Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma yanayofanyika mkoani Morogoro.


Sehemu ya washiriki wa mafunzo kuhusu Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo hayo yanayofanyika mkoani Morogoro.

Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma Mhe. Hamisa Kalombola (Jaji Mst) akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) kufungua rasmi mafunzo kuhusu Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma yanayofanyika mkoani Morogoro.

Sehemu ya Watendaji wa Tume ya Utumishi wa Umma wakifuatilia mafunzo waliyoyaratibu kuhusu Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma yanayofanyika mkoani Morogoro.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo kuhusu Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma wakifuatilia mafunzo hayo yanayofanyika mkoani Morogoro.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (wapili kutoka kulia) akiagana na Kaimu Katibu, Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. John Mbisso (kulia) wakati akiondoka baada ya kufungua mafunzo kuhusu Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma yanayofanyika mkoani Morogoro. Aliyejitanda kilemba ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma Mhe. Hamisa Kalombola (Jaji Mst). Nyuma yake ni Naibu Katibu Msaidizi wa Tume hiyo Bi. Celina Maongezi.

Mkurugenzi wa Idara ya Miongozo, Uwezeshaji na Utafiti, Bw. Peleleja Masesa akitoa utambulisho wa washiriki waliohudhuria mafunzo kuhusu Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma yanayofanyika mkoani Morogoro.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (katikati) akifuatilia jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma yanayofanyika mkoani Morogoro. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma Mhe. Hamisa Kalombola (Jaji Mst).

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watendaji wa Tume ya Utumishi wa Umma na Washiriki kutoka Serikali Kuu zikiwemo (Wizara, Sekretarieti za Mikoa, Idara zinazojitegemea na Wakala za Serikali), Taasisi za Umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa baada ya kufungua mafunzo kuhusu Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma yanayofanyika mkoani Morogoro.

Afisa Utumishi, Bodi ya Pamba Tanzania ambaye ni mshiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa ushughulikiaji wa Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma Bi. Changwa Mkwazu akitoa neno la shukrani kwa niaba ya washiriki wote kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) baada ya Waziri huyo kufungua mafunzo hayo yanayofanyika mkoani Morogoro.


Sunday, February 9, 2025

WAZIRI SIMBACHAWENE ASHIRIKI IBADA YA SHUKRANI YA ALIYEKUWA WAZIRI MKUU, HAYATI EDWARD LOWASSA, ASISITIZA SUALA LA AMANI


Na Lusungu Helela-MONDULI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amewataka Watanzania kumuenzi aliyekuwa Waziri Mkuu, Hayati Edward Lowassa kwa  kuendelea kudumisha umoja, amani na mshikamano ili kuepuka mapigano yanayoendelea katika nchi zingine.

Mhe. Simbachawene ametoa kauli hiyo leo Jumapili Februari 9, 2025 wakati wa Ibada maalumu ya Kumbukizi ya mwaka mmoja wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania,  Hayati  Edward Lowassa huku akiwataka Watanzania kuendeleza  yale yote mazuri aliyokuwa akiyafanya. 

Aidha, Mhe. Simbachawene amesema Hayati Edward Lowassa atakumbukwa daima kwa kuwagusa watu wengi kwa namna  chanya.

Amefafanua kuwa Hayati Edward Lowassa  ni Kiongozi aliyekuwa na upendo, aliyewasaidia watu wengi  na aliyependa kuzungumza na  kila mtu bila kujali anamfahamu au hamfahamu.

Ameongeza kuwa "Hayati Edward Lowassa ni kiongozi aliyekuwa  hapendi kumuona mtu yeyote akipata shida, alitamani kumuona kila mmoja akiwa na furaha wakati wote" amesema.

Katika hatua nyingine Mhe. Simbachawene amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumuenzi Hayati Lowassa kwa mchango wake chanya aliokuwa akiutoa kwa maendeleo ya taifa.

“Hivi sasa tuna shule nyingi zimejengwa na zimeendelea kujengwa, barabara, miradi ya maji imeendelea kutekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan” ameongeza.

Akizungumza kwa niaba ya Familia ya Hayati Edward Lowassa,   mtoto wa kwanza  ambaye pia ni Mbunge wa  Monduli, Mhe. Fredrick Lowassa ametumia fursa hiyo kuwashukuru wote waliokuwa pamoja tangu baba yao alipofariki hadi hivi sasa huku akimtaja  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa mchango wake mkubwa  kwa familia hiyo tangu baba yao alipoanza kuugua hadi umauti ulipomkuta.

"Ikiwa leo ni mwaka mmoja tangu baba yetu atutoke, alikuwa ni kiongozi na nembo ya Wananchi wa Monduli,   tuendelee kumuenzi kwa  mchango wake  mkubwa  katika kudumisha mshikamano kwa jamii za wafugaji wa asili" amesisitiza Mhe. Fredrick Lowassa

Aidha, Ametumia fursa hiyo  kuiomba Serikali iharakishe mchakato wa kuandaa Makumbusho ya Hayati Edward Lowassa kutokana na ujio wa wageni wengi wanaofika nyumbani hapo kwa ajili ya kujifunza mambo aliyokuwa akiyafanya baba yao.

Naye, Baba Askofu Mstaafu  wa Kanisa la Kiinjili la kilutheri Tanzania KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati, Dkt. Solomon  Masangwa ameisisitiza familia ya Hayati Edward Lowassa kuzidi kumshirikisha Mungu katika kila jambo wanalolifanya ili kuendelea kushikamana.

Hayati Edward Ngoyai Lowassa alifariki dunia  Februari 10, 2024 na kuzikwa nyumbani kwake Monduli tarehe 17 Februari 2024.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza  katika Ibada ya Shukrani ya aliyekuwa Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Ngoyai Lowassa  iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)  Monduli Mjini Mkoani Arusha.

Sehemu ya wanafamilia wa Hayati Edward Lowassa wakiwa kwenye Ibada ya Shukrani ya aliyekuwa Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Edward Ngoyai Lowassa iliyofanyika leo  katika Kanisa la Kiinjili Kilutheri Tanzania (KKKT) Monduli Mjini Mkoani Arusha.

Sehemu ya wanafamilia wa Hayati Edward Lowassa wakiwa kwenye Ibada ya Shukrani ya aliyekuwa Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Edward Ngoyai Lowassa iliyofanyika leo  katika Kanisa la Kiinjili Kilutheri Tanzania (KKKT) Monduli Mjini Mkoani Arusha.

Mbunge wa  Monduli, Mhe. Fredrick Lowassa akisalimiana na baadhi ya Washarika  wakati wa Ibada ya Shukrani ya aliyekuwa Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Ngoyai Lowassa  iliyofanyika leo  katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Monduli Mjini Mkoani Arusha.

 


 


 


RAIS KAGAME AWASILI TANZANIA MKUTANO WA KUJADILI SUALA LA AMANI YA DRC

 Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame amewasili nchini Tanzania kwa ajili ya mkutano wa kujadili amani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),

Mhe. Kagame  amewasili asubuhi ya leo Jumamosi Februari 8, 2025 na kupokewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere

Mkutano huo unafanyika huku vikundi vya waasi chini ya Alliance Fleuve Congo (AFC/M23) vimekamata miji ya Goma, Kivu Kaskazini na Nyabibwe, Kivu Kusini vikielekea Bukavu.


Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame akisalimiana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene mara baada ya kuwasili   katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere  kwa ajili ya mkutano wa kujadili amani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),

Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame akizungumza na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene mara baada ya kuwasili   katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere  kwa ajili ya mkutano wa kujadili amani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),

Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame akiwa na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene mara baada ya kuwasili   katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere  kwa ajili ya mkutano wa kujadili amani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),

Friday, February 7, 2025

WAZIRI WA UTUMISHI ZANZIBAR MHE. HAROUN ASISITIZA MASHIRIKIANO BAINA YA SJMT NA SMZ KATIKA MASUALA YA UTUMISHI

 Na. Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman amewataka Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (SJMT) na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kuendeleza mashirikiano katika masuala ya utumishi kwa ustawi wa maendeleo ya taifa.

Mhe. Suleiman amesema hayo leo wakati akihitimisha kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi baina ya ofisi hizo mbili kilichofanyika kwa siku tatu jijini Dodoma.

Mhe. Suleiman amesema kikao hicho kiongeze tija katika utendaji kazi ikiwemo kubadilishana uzoefu kuhusu masuala mbalimbali ya kiutumishi pamoja na kujadili changamoto mbalimbali zitakazosaidia kuimarisha utumishi  kwa ufanisi mkubwa kwa maendeleo ya taifa.

Aidha, Waziri Suleiman amewataka washiriki wa kikao hicho kuwa wazalendo, waaminifu na waadilifu, kusimamia walio chini yao na kutii maagizo ya viongozi walio juu yao.

Kwa Upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu akimwakilisha Waziri wa Ofisi hiyo, Mhe. George Simbachawene amesema kikao hicho  kitawajengea uwezo mkubwa katika kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kuzingatia miongozo na kanuni za Utumishi wa Umma. 

Awali, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amesema kikao hicho kitasaidia kuimarisha mashirikiano mazuri baina ya ofisi hizo mbili na kuahidi kuendelea kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa majukumu kwa masilahi mapana ya nchi.

Katika Kikao hicho cha siku tatu moja ya maazimio yaliyopitishwa ni kutoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kusimamia vema masuala ya Utumishi na Utawala Bora.

Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman (kushoto) akizungumza wakati wa kikao baina ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (aliyesimama) akizungumza wakati wa kikao baina ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman (aliyevaa tai nyeusi) akiwasili katika eneo la kikao kilichofanyika baina ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi.


Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakiwa kwenye kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akitoa maelezo ya awali kabla ya kuanza rasmi kwa kikao baina ya ofisi yake na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia kikao  kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi baina ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman (kulia) akizungumza jambo na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu (katikati) kabla ya Mhe. Suleiman kufunga kikao baina ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI (SJMT) na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.  Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi.

Viongozi na Watendaji wa Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakifuatilia kikao cha ofisi hiyo na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (SJMT) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman (wa tano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (SJMT) na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) baada ya kufunga kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi.


 

Thursday, February 6, 2025

MAKATIBU WAKUU OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA AFISI YA RAIS, KATIBA, SHERIA, UTUMISHI NA UTAWALA BORA (SMZ) WAONGOZA KIKAO CHA MASHIRIKIANO KATIKA SEKTA YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA

 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (wa kwanza kushoto) akizungumza wakati wa kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kati ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.


Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakiwa kwenye kikao kilicholenga   kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa ofisi hizo mbili kilichofanyika jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ), Bi. Mansoura Kassim (kulia) akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kushoto) wakati wa kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa ofisi hizo mbili kilichofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kati ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu, Utumishi na Utawala Bora, Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ), Bw. Omar Gora (wa kwanza kushoto) akiwasilisha hoja kuhusu ajira wakati wa kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kati ya ofisi hiyo na Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilichofanyika jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyrus Kapinga (aliyesimama) akisoma taarifa ya kikao cha wataalam kuhusu Sekta ya Watumishi wa Umma na Utawala Bora wakati wa kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kati ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.


Wakurugenzi kutoka Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakifuatilia kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kati ya ofisi hiyo na Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilichofanyika jijini Dodoma.

Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kati ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.


Wakurugenzi kutoka Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakifuatilia kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kati ya ofisi hiyo na Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilichofanyika jijini Dodoma.


Wakurugenzi Wasaidizi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kati ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.

Wakurugenzi kutoka Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakifuatilia kikao kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kati ya ofisi hiyo na Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilichofanyika jijini Dodoma.




Wednesday, February 5, 2025

OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA AFISI YA RAIS, KATIBA, SHERIA, UTUMISHI NA UTAWALA BORA (SMZ) YAFANYA KIKAO KAZI CHA MASHIRIKIANO KUHUSU MASUALA YA UTUMISHI



Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyrus Kapinga akizungumza wakati wa kikao kazi cha kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kati ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Mipango, Sera na Utafiti, Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ), Bw. Said Salim akizungumza wakati wa kikao kazi cha kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kati ya ofisi hiyo na Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilichofanyika jijini Dodoma.


Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakiwa kwenye kikao kazi kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Musa Magufuli (aliyenyoosha mkono) akichangia hoja wakati wa kikao kazi cha ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kilichofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakifuatilia kikao kazi kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kati ya ofisi hiyo na Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilichofanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) wakifuatilia kikao kazi kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kati ya ofisi hiyo na Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilichofanyika jijini Dodoma.


Katibu Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma – Zanzibar, Bi. Asma Jidawy (wa kwanza kushoto) akiwasilisha hoja wakati wa kikao kazi kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia kikao kazi kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kati ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi akifafanua hoja wakati wa kikao kazi kilicholenga kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kiutumishi kati ya ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Priscus Kiwango akielezea kuhusu mifumo mbalimbali ya kiutumishi inayotumika katika utendaji kazi wakati wa kikao kazi cha ofisi hiyo na Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma.