Wednesday, January 17, 2024

KAMATI YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA IKIPOKEA NA KUJADILI TAARIFA YA OFISI YA RAIS-UTUMISHI KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAAZIMIO YA MKUTANO WA BUNGE

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akiongoza kikao cha kamati yake, Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge kilichofanyika katika ofisi za Bunge jijini Dodoma.


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao cha kamati hiyo na Viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watendaji wa taasisi za Wakala ya Ndege za Serikali, Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma zilizo chini ya ofisi hiyo.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa neno la utangulizi katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma kabla ya kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya Bunge kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na Kaimu Katibu Mkuu, Bw. Xavier Daudi wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge kilichofanyika jijini Dodoma.


Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Majula Mahendeka akifafanua jambo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge kwa Wakala ya Ndege za Serikali, Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Mashimba Ndaki akichangia hoja wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Viongozi na watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge.

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) Capt. Budodi Budodi akitoa ufafanuzi wa utekelezaji wa maelekezo na ushauri uliotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati ilipofanya ziara katika ofisi hiyo.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) Eng. Benedict Ndomba akifafanua kuhusu utendaji wa mifumo ya TEHAMA Serikalini wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilichofanyika katika ofisi za Bunge jijini Dodoma.

Kaimu Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Bw. Innocent Bomani akifafanua hoja kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kuhusu mifumo ya ajira portal wakati wa kikao cha kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kilichofanyika katika ofisi za Bunge jijini Dodoma.

Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Wakala ya Ndege za Serikali, Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma wakiwa katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilichofanyika katika ofisi za Bunge jijini Dodoma.


Maafisa wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Wakala ya Ndege za Serikali, Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama (hayupo pichani) wakati wa kikao cha kamati na ofisi hiyo kilichofanyika katika ofisi za Bunge jijini Dodoma

 


 

No comments:

Post a Comment